Tujikumbushe wahenga

Tujikumbushe wahenga

Ipi dot com

JF-Expert Member
Joined
Mar 28, 2011
Posts
306
Reaction score
166
Mwaka 1997 nilikuwa nafanya kibarua cha ujenzi ktk wilaya moja mkoani Mbeya

Wakati naendelea na kazi siku moja alikuja ndugu yangu ambae awali tulikuwa tukiishi wote ilala mtaa wa bungoni kabla sijaenda mbeya kwa ajili ya kibarua.

Baada ya kunisabahi alinieleza kuwa ana mpango wa kwenda south africa wakati huo ilikuwa kama fashen kwa vijana kwenda South

Kwa vile nilikuwa na fedha kidogo nikaona hii fursa ya kutoka na mimi haraka na mimi nikamshirikisha jamaa yangu john(nadhani yumo jumu JF)

Sikumbuki tarehe rasmi lakini ulikuwa mwezi desember haraka nikafanya maandalizi na jamaangu john nae alifanya maandalizi tukawa watatu tayari kuanza safari

Mala kaja jamaa yetu mwingine katoka dar tukawa wanne siku moja kabla ya safari jamaa mwingine kajiunga nasi tukawa watano

Mtihani wa kwanza ni kibali cha wazazi baba alikubali japo kwa shingo upande mama kagoma ilibidi nikamuone mjomba ambaye amesafiri sana Afrika ili amshawishi mama anikubalie lakini nilishaamua kusafiri hata wakigoma

Baada ya mama kuonana na mjomba akanikubalia hapo sasa tukapanga siku inayofuata tuanze safari rasmi.

Asubuhi tukaondoka kwenda tunduma safari kama masaa mawili tukafika pale na kuanza procces za uhamiaji nakumbuka mimi nilikuwa ma pass ya muda baada ya kukamilisha ilibidi tutafute chumba tulale maana kulikuwa na shida ya usafiri kwenda lusaka si kama sasa
Wakati tunasubiri kesho ifike huyu jamaa alieongezeka ambaye wa tano katika kuzunguka tunduma akakutana na jamaa yake ambae alikuwa mwenyeji pale tunduma ghafra jamaa kabadili mawazo hataki tena kusafiri tukaona poa katupunguzia mzigo.

Asubuhi ilipofika ndugu yangu alienishawishi kwenda SA kaanza kusuasua na yeye tulikua tukimtegemea maana aliwahi kwenda kabla,na tulijua angekuwa mwenyeji wetu.

Hapo bado masaa machache tuanze safari likawa pigo kwetu tumebaki watatu.

Wakati huo mabasi yalikua yanaanza safari jioni yakiwa yamebaki masaa mawili jamaa wa tatu akajitoa tukabaki wawili mimi na jamaangu John.

Tukaona poa tuu ngoja tukapambane wanaume tukachanganya hela zetu tukachenji tupate kwacha,kisha tukaenda kukata tiket tayari kwa safari.

Hapo ugumu wa safari unaanza ni kaanza kujuta nimeanzaje mimi.

Itaendelelea...
 
Inaendelea....
Siku hiyo kumbe basi moja halikufanya safari kati ya mawili ambayo yalikua yanaenda lusaka mpk Harare hivyo ilibidi abiria wa
Basi nyingine tuingie kwenye basi
Moja.
Kwa kweli hali ilikuwa mbaya sana maana basi lilijaa sijawai ona maana kama unavyojua wafanya biashara wanakuwa na mizigo mingi mno ilikuwa huwezi hata kusogeza mguu ukizingatia hatukupata siti.
Tulisafiri usiku kucha tukiwa tumesimama takribani km 800 kwa kweli hali ilikuwa mbaya sana asubuhi tukafika mji wa kapili pale ndio tukapata siti zilibaki kama km 200 tufike lusaka kwa jinsi tulivyochoka ilikuwa kama km moja tu mpaka lusaka.
Tukafika asubuhi ile tukauliza wenyeji malazi ya bei rahisi tukapata pa kulala,nilipata usingizi mzito haijawai tokea.
Baada ya siku moja tukakata tiketi tayari kwa safari ya harare,kesho yake mapema tukawa ndani ya basi kuelekea zimbabwe.

Tukasafiri hadi mto zambezi ni mpakani ikabidi tuchenji kwacha kuwa zimdorar(pesa ya zimbabwe)
Kama kawaida pale boda kuna utaratibu wa kujaza fomu za uhamiaji kuna kipengere unajaza show money ndugu yangu john akaandika kiasi chote tulichokua nacho, kumbe kisheria za kwao ilikuwa kosa
Wakamwambia hebu lete hiyo hela tuone loo kumbe ilikuwa bonge la kosa alipo itoa tuu wakachuku hela zote na kuanza kutusomea sheria zao na kutuambia mnaruhusiwa kudai baada ya miezi sita.
Hapo nilihisi kuona nyota nyota maana hatubakiwa na hela yoyote kwa kweli tulichanganyiwa sana
Baada ya hapo safari iliendelea tunaenda ugenini hatuna hata senti
Itaendele...
 
Inaendelea....
Siku hiyo kumbe basi moja halikufanya safari kati ya mawili ambayo yalikua yanaenda lusaka mpk Harare hivyo ilibidi abiria wa
Basi nyingine tuingie kwenye basi
Moja.
Kwa kweli hali ilikuwa mbaya sana maana basi lilijaa sijawai ona maana kama unavyojua wafanya biashara wanakuwa na mizigo mingi mno ilikuwa huwezi hata kusogeza mguu ukizingatia hatukupata siti.
Tulisafiri usiku kucha tukiwa tumesimama takribani km 800 kwa kweli hali ilikuwa mbaya sana asubuhi tukafika mji wa kapili pale ndio tukapata siti zilibaki kama km 200 tufike lusaka kwa jinsi tulivyochoka ilikuwa kama km moja tu mpaka lusaka.
Tukafika asubuhi ile tukauliza wenyeji malazi ya bei rahisi tukapata pa kulala,nilipata usingizi mzito haijawai tokea.
Baada ya siku moja tukakata tiketi tayari kwa safari ya harare,kesho yake mapema tukawa ndani ya basi kuelekea zimbabwe.

Tukasafiri hadi mto zambezi ni mpakani ikabidi tuchenji kwacha kuwa zimdorar(pesa ya zimbabwe)
Kama kawaida pale boda kuna utaratibu wa kujaza fomu za uhamiaji kuna kipengere unajaza show money ndugu yangu john akaandika kiasi chote tulichokua nacho, kumbe kisheria za kwao ilikuwa kosa
Wakamwambia hebu lete hiyo hela tuone loo kumbe ilikuwa bonge la kosa alipo itoa tuu wakachuku hela zote na kuanza kutusomea sheria zao na kutuambia mnaruhusiwa kudai baada ya miezi sita.
Hapo nilihisi kuona nyota nyota maana hatubakiwa na hela yoyote kwa kweli tulichanganyiwa sana
Baada ya hapo safari iliendelea tunaenda ugenini hatuna hata senti
Itaendele...












Sent from my SM-J730G using JamiiForums mobile app
Hili Life ndo lakikamanda...
Hapo haina kukata tamaa wala kulegeza...
Walamba midomo wa humu JF wataona kama Geni sanaa na wata skizia sanaa muendelezo.

Any way hata mimi nina langu...
Siku ntadondosha
 
Inaendelea....
Tulifika harare saa 12 jioni kitu cha kwanza kilichonistua ni alama zikionyesha kuna vibaka maneo hayo ni kama alama hizi za barabarani
Hapo ni stendi tumeganda hatu jui tuelekee wapi baadae tukapata wazo twende kituo cha polisi tukajieleze huenda tukapata msaada. Tukajongea wakati huo tunaona vibaka wanatuundia kamati tukajivuta mpk polisi haikua mbali sana polisi wlikuwa bize hawakuwa na na maongezi marefu sana zaidi ya kutulekeza hoteli zilipo tena za bei kubwa.
Baadae tukamwona mama mmoja tukajieleza ma madhira yaliyotupata akatuelewa akatupeleka jumba moja la serikali ambalo gharama ilikuwa ndogo sana tunaweza kuita hostel tukamshuru akaenda zake kasheshe ikaja tutalipa nini?
Hapo inaelekea saa mbili usiku tukakubaliana tulale walipo walinzi ya kesho yatajisumbukia...
Baada kuongea na walinzi walituelewa lakini mmoja wao akakumbuka kitu akatoka spidi mala akaja na jamaa mmoja akamtambulisha kuwa ni mtanzania
Hapo akili ilitulia tukaslimiana na jamaa yeye alikuwa ajent wa mabasi yaliitwa twiga wahenga mnayakumbuka nadhani.
Jamaa alitufadhiri akatulipia malazi na chakula na akatukatia tiketi mbili mabasi ya kwenda Gaberon botswana (Mungu Mkubwa)
Asubuhi kumekucha tukaanza safari kwenda Botswana kupitia boda ya parmtree tukafika jioni mida kama saa 12 jioni kasheshe nyingine tena inaanza.
Mwenzangu alikuwa na pass kubwa ilimruhusu avuke bila kikwazo lakini kwangu ilikuwa mtihani kwa sababu nilikuwa na pass ndogo kwa hiyo ilinihitaji niwe na visa .
Kumbuka sina hata mia ghafra naambiwa rudi harare ukaombe viza sijapata hata dkk moja ya kuagana na john nikapitishwa kwenye maofisi ya gafra natokekea upande wa kutokea kwa mbali namuona jamaa yangu akifuta machozi hapo kumbuka rugha ya kiingereza ni shida.
Nikakabidhiwa askari nikapelekwa nje ya geti nikahisi kama nimechizika gafra kwa mbaali kagiza kanaanza....
 
Inaendelea..
Kwa wale waliofika ile boda pana kamwendo kama km mbili toka boda ya zimbabwe na botswana halafu kuna wanyama hatari huruhusiwi kutembea kwa mguu.
Muda ulipokuwa unaenda nikaona isiwe kesi liwalo na liwe nikiwa na kibegi changu huyoo naitafuta boda ya zimbambwe baada ya muda fulani nikafika boda ya zimbabwe.
Kumbuka sina hata mia mfukoni na lugha ilikuwa shida kidogo kila nikijieleza jamaa hawanielewi na wao wanataka show money na mimi nikajitoa ufahamu kidogo nikatafuta kona moja pale pale ofisi za uhamiaji nikakaa, moyoni nilijiwazia kuwa nitakaa hapo mpaka watu ha haki za binadàmu watakapo kuja kwa hiyo nikaondoa hofu nikajiegesha ukutani tayari kutafuta usingizi...
Hapo hata njaa siisikii na sijui jamaa yangu yupo katika hali gani hapo nawaza yangu tu. Ilipofika saa mbili na ushee ile shift ya wafanyakazi ikawa inatoka inaingia shift nyingine.
Mala namuona jamaa mmoja kanijia kaniuliza imekuaje nikajieleza,kwa nilipokuwa nimekaa nilikuwa kama nimewawekea kiwingu.
Basi akachukua pass yangu akanipa siku saba nikae zimbabwe kisha nitoke sasa najiuliza naenda wapi usiku huu? Kumbuka mfukoni sina hela yoyote.kumbuka toka hapo mpaka Harare ni kama km 500 hivi.
Nikaona isiwe nikatoka mpaka getini naangalia gari gani niombe lift mala naliona bus toka botswana nikkajisoheza mtt wa kiume nikaona jamaa nikajua ni muhusika wa hilo hasi, nikajieleza kidogo tuu kanielewa kanambia ingia nikashusha pumzi nikamshukuru Mungu safari ikaanza..
Lile basi lilikuwa linaishia Bulawayo km kama 100 hivi baada ya kufika Bulawayo kondacta kania mbia usishuke lala humu mpk kesho ndio uangalie utaratibu wa kwenda(asijue sina hata mia mfukoni)
Asubuhi inafika kwa haraka sana namshukutu Mungu naingia mtaani sina uelekeo sasa ndio nagundua njaa inauma,
Wazo linanijia gafra nakumbuka pale harare kuna mchungaji ambae ni rafiki yake baba anaweza kunisaidia lakini nitafikaje?
Na siku hiyo ilikiwa siku ya ibada nikajisemea moyoni hapa siraha yoyote lazima niitumie ili nifike kwa madiba(south) Wazo likaja ili nimpate huyu mchungaji nikatafuta kanisa pale bulawayo kwa msaada wa polisi wakanisaidia nikafika kanisani nikajieleza lakini hali ilikuwa tete maana vongozi wa kanisa walikuwa na wasiwasi na mimi,mala wanikague wakakagua begi halafu wanaenda kufanya kikao wananiita tena wananihoji nikaona loo nimeingia cha kike hapo njaa imepamba moto...
 
Twende kazi....
Baadae sana wale viongozi wakaniita nijieleze huyo mchungaji alieko harare namfahamu kivipi,nikawaeleza kuwa ni rafiki yake babaangu japo yeye hanifahamu mpaka nikajieleze.
Kumbe kati yao mmoja wao alikuwa na safari ya kwenda harare hivyo wakaniambia hawana imani na mimi hivyo nitakaa nyuma kwenye pick up yake nikaona fresh na gari yenyewe imefunikwa kwa hiyo nikakubali,jamaa kanipeleka kwake tukala kisha safari inaanza ya km 400 na ushee.
Usiku saa mbili tunafika kwa huyo mchungaji maeneo karibu harare university,jamaa kagonga hodi mala anatoka kijana mmoja anatusalimu kisha anatukaribisha ndani.
Ndani tunamkuta mwenyeji baada ya salamu(kwa kiingereza) jamaa anamwelekeza mchungaji (hapo jamaa alikuwa na hofu kuwa huenda nikakataliwa)
Jamaa akamueleza kuwa huyu mtu kapatwa na changamoto ya viza lakini kakutaja wewe kama ndugu yako hebu msikilize,mzee kaniuliza kwa kimombo unatoka wapi?
Mimi:Tanzania
Mzee; hujambo
Mimi; sijambo shikamoo
Mzee: unatoka mkoa gani?
Mimi :mbeya
Mzee; unaitwa nani?
Mimi; lukaa (si jina halisi?
Mzee: babaako?
Nikamtaja yaani kufumba na kufumbua nilikumbatiwa na familia nzima yaani mama mtoto na baba kumbe mama alikuwa sehemu anasikia kila kitu na aliposikia jina baba alifurahi mno kwa kweli nikasahau shida zangu kwa muda.
Yule jamaa alienileta alifadhaika sana kwa jinsi nilivyopokelewa...
 
Twende kazi....
Baadae sana wale viongozi wakaniita nijieleze huyo mchungaji alieko harare namfahamu kivipi,nikawaeleza kuwa ni rafiki yake babaangu japo yeye hanifahamu mpaka nikajieleze.
Kumbe kati yao mmoja wao alikuwa na safari ya kwenda harare hivyo wakaniambia hawana imani na mimi hivyo nitakaa nyuma kwenye pick up yake nikaona fresh na gari yenyewe imefunikwa kwa hiyo nikakubali,jamaa kanipeleka kwake tukala kisha safari inaanza ya km 400 na ushee.
Usiku saa mbili tunafika kwa huyo mchungaji maeneo karibu harare university,jamaa kagonga hodi mala anatoka kijana mmoja anatusalimu kisha anatukaribisha ndani.
Ndani tunamkuta mwenyeji baada ya salamu(kwa kiingereza) jamaa anamwelekeza mchungaji (hapo jamaa alikuwa na hofu kuwa huenda nikakataliwa)
Jamaa akamueleza kuwa huyu mtu kapatwa na changamoto ya viza lakini kakutaja wewe kama ndugu yako hebu msikilize,mzee kaniuliza kwa kimombo unatoka wapi?
Mimi:Tanzania
Mzee; hujambo
Mimi; sijambo shikamoo
Mzee: unatoka mkoa gani?
Mimi :mbeya
Mzee; unaitwa nani?
Mimi; lukaa (si jina halisi?
Mzee: babaako?
Nikamtaja yaani kufumba na kufumbua nilikumbatiwa na familia nzima yaani mama mtoto na baba kumbe mama alikuwa sehemu anasikia kila kitu na aliposikia jina baba alifurahi mno kwa kweli nikasahau shida zangu kwa muda.
Yule jamaa alienileta alifadhaika sana kwa jinsi nilivyopokelewa....
Sent from my SM-J730G using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom