Tujifunze biashara kidogo

Tujifunze biashara kidogo

Hata mimi ndio niliwaza kama wewe.
Ile concept aliyoitoa mtoa mada ipo kinyume.
Yaani mteja anayechukua bidhaa nyingi ndio umkomoe kwa kumuongezea bei sasa mteja gani ni mjinga atakayekubali kuchukua vitu vingi kwa bei iliyozidi thamani halisi.
Na ile ya mteja kusema achukue bidhaa moja apeleke kwenye gari arudi tena mpaka mara 3 ni nani atakubali huu usumbufu kwani hakuna wafanyabiashara wengine kama wewe.
Labda kama mkoa mzima matikiti unauza peje yako hapo sawa lkn kama kuna wauzaji wengine inakula kwako.
Na ile concept ya 2 ya kusema mchina ameleta magari kama yako na akauza kwa bei ya chini halafu mkurugenzi akashauri kwamba wazidi kuongeza bei bado practically haiwezi kufanikisha.
Nasema haiwezi kufanikisha kwa sababu utawapata watu wachache ambao hawajui kutofautisha kitu bora na kisicho bora.
Ila wale wenye uwezo wa kutofautisha bidhaa bora na isiyo bora hautawapata kwenye ule mtego.
Na pia wale ambao hawajui kutofautisha utawapata siku za mwanzoni ila wakishaanza kutumia na kujua kwamba zile gari za kampuni zote mbili ni sawa wataambiana na hutawaona tena.
Jamaa kayumba sana pale eti uende kwenye gari malatatu kupelela tikitimaji yaani hayo matikiti yamaana sana.

Kafosi sana kuwa applicable.
 
Hizo ni theories walikaririshwa chuo lakini ukija kwenye uhalisia unaangukia pua.
Jamaa kayumba sana pale eti uende kwenye gari malatatu kupelela tikitimaji yaani hayo matikiti yamaana sana.

Kafosi sana kuwa applicable.
 
Nilikuwaga na duka la nguo Dodoma nilicho kuwa nakifanya nikienda kufunga mzigo let say jins 50 basi nazigawa nusu kwa nusu harafu nazipa bei tofaut kundi la kwanza nitaziuza bei nusu ya elf 25 na kuziita copy na kundi la nitaziuza 45 na kuziita original hivyo mteja ataangalia quality yake na kuchagua inayo mfaa
wee jamaa uko smart sana asee
 
Hizo mbinu alizotoa mleta mada hazifunction kabisa huku kitaa, watu wengi wanajali quantity zaidi kuliko quality hii ndio falsafa ya sisi masikini.
 
IMG_20220423_165334.jpg
 
Hizo mbinu alizotoa mleta mada hazifunction kabisa huku kitaa, watu wengi wanajali quantity zaidi kuliko quality hii ndio falsafa ya sisi masikini.
Mifano hiyo miwili, japo sio halisi inafundisha mambo mawili;

MFANO WA KWANZA:

Mzee ametumia mbinu hiyo ili kuwafanya wateja waridhike na bei ya TZS 3,000/= kwa tikiti moja. Anachotaka mzee ni kwamba asipoteze hata mia (Kupunguza uwezekano wa mteja kuomba punguzo la bei).

Kwahiyo, ame-overprice fungu la matikiti matatu ili mtu aone bei ya tikiti moja ni nafuu sana.

Wengi huwa wanapunguza bei: Mfano, tikiti moja anauza TZS 3,000/=, matikiti matatu anauza TZS 8,000/=. Kwa mbinu hii wateja wengi watanunua matikiti matatu.

Tupige hesabu: Tuseme wote wana matikiti 21

Mzee: akiuza moja moja atapata TZS 63,000/=, na akiuza matatu matatu atapata TZS 70,000/=

Mtu anaetumia mbinu iliyozoeleka: akiuza moja moja atapata TZS 63,000/=, akiuza matatu matatu (Na ndivyo itakavyokuwa) atapata TZS 56,000/=

UWEZEKANO: Kuna uwezekano mkubwa wa Mzee kuondoka na TZS 63K, wakati huyu mwingine uwezekano ni mkubwa kuwa ataondoka na TZS 56K!

Pointi ya msingi ni kucheza na saikolojia za watu, kwa kuzingatia uhitaji, upatikanaji na aina ya wateja wako.

SWALI: Ki-mtaani mtaani, kipi ni nafuu... kujenga nyumba kidogo kidogo kwa kutumia mafundi wa mitaani au kuilipa kampuni ya ujenzi kwa mkupuo? (Watu wa serikalini mnaita Force Procurement kama sijakosea)


MFANO WA PILI:
Kampuni ya Apple inatumia hii saikolojia, na sababu ni moja: wanawajua vizuri wateja wao. Wateja wa kampuni zinazotumia mbinu hii (Kampuni zinazotengeneza bidhaa za kifahari, ambazo zinaaminika kuwa ni imara, bora, na za kipekee) ni wateja ambao hawajali kuhusu bei, wanachojali ni "status".

Ndio maana ni vigumu kukuta tangazo la gari la Lamborghini Tanzania, au Zimbabwe au Somalia, au kwenye TV kwasababu wateja wa Lamborghini hawapo Tanzania, wala hawana muda wa kuangalia TV!

Kuna mtu atabisha...., ngoja nijaribu hivi;

Kwa mfano: Ukisikia Landcruiser V8 mpya inauzwa TZS 25,000,0000/= utanunua? Au tuseme wazo gani litakujia kichwani?

Sasa tuseme ni Landcruiser V8 hiyo hiyo inauzwa bei hiyo hiyo 25m lakini ukaambiwa inatoka China... utaridhika na bei au la?

Akili mtu wangu!

Haaiiyaaaaa.... tawanyikaaaaaa! (In Soudy Brown's voice).

Mjadala na uendelee.
 
Madini mazuri sana ,mm nikiendaga kununua vitu sokon mara nasikia muuza genge anasema ukinunua nyanya Tano atauza Kwa mia Tano,ukinunua tatu mia na hamsini.,wengi tuta angalia quanty automatically tutachukua za mia Tano .
 
Back
Top Bottom