Aizi Azma
JF-Expert Member
- Nov 30, 2016
- 553
- 1,151
Haya mambo sidhani kama yanafundishwa darasani. Hii ni street knowledge, real life situations ambazo zinatufunza mengi. Sasa kuna matukio mawili hapa ya kibiashara, naomba mwenye jibu la mojawapo au yote anipe.
1. MOJA TZS 3,000/=, MATATU TZS 10,000/=.
Mzee mmoja pale Magomeni Mapipa anauza matikiti maji. Tikiti moja anauza kwa TZS 3,000/=, matatu anauza kwa TZS 10,000/=. Mchana wa leo akapita kijana pale, akanunua tikiti la kwanza, akalipa TZS 3,000/=. Akanunua jingine tena, akalipeleka kwenye gari lake, akalipa TZS 3,000/=. Akarudi tena, akanunua tikiti la tatu, akalipa TZS 3,000/= halafu akamwambia yule mzee,''Ivo we mzee umeona? Nimenunua matikiti matatu kwa TZS 9,000/= tu badala ya TZS 10,000/=!!! Inaonesha we mzee ni mgeni kwenye masuala ya biashara eh?!?!?"
Wakati yule kijana anaondoka na gari lake, mzee akajisemea huku anacheka,"Watu bwana, yaani mtu amenunua matikiti matatu lakini bado anataka anifundishe masuala ya biashara! Hahahaha!!"
SWALI: Kwanini mzee ameweka bei zake kwa mtindo huu? Je, ni kweli mzee hajui biashara? Fafanua.
2. TUONGEZE BEI ILI KUSHINDANA NAO!
Kampuni moja ya magari nchini Ujerumani ilikuwa inafahamika kwa kutengeneza magari ya kifahari yanayouzwa ghali sana. Ghafla ikaibuka kampuni nyingine ya Kichina inayotengeneza magari kama yale ya Ujerumani, lakini wao sasa wanauza kwa bei ambayo ni nusu ya ile ya magari ya Ujerumani.
Kuona hivyo, meneja mauzo wa ile kampuni ya Kijerumani akamfuata Mkurugenzi wake ili kumweleza kuhusu ujio wa hii kampuni mpya inayotengeneza magari kama ya kwao na kuyauza kwa bei chee.
Meneja mauzo akamuuliza Mkurugenzi wake,"Tunafanyaje sasa kukabiliana nao sokoni?". Mkurugenzi akajibu,"Tuongeze bei ya magari yetu!"
SWALI: Kwanini mkurugenzi anafikiri kuongeza bei ya magari yao ndio njia bora ya kushindana sokoni? Fafanua.
NB: Kwa ambae yuko interested na tricks kama hizi, unaweza kuupitia uzi huu pia; GROWTH HACKING
#virus
1. MOJA TZS 3,000/=, MATATU TZS 10,000/=.
Mzee mmoja pale Magomeni Mapipa anauza matikiti maji. Tikiti moja anauza kwa TZS 3,000/=, matatu anauza kwa TZS 10,000/=. Mchana wa leo akapita kijana pale, akanunua tikiti la kwanza, akalipa TZS 3,000/=. Akanunua jingine tena, akalipeleka kwenye gari lake, akalipa TZS 3,000/=. Akarudi tena, akanunua tikiti la tatu, akalipa TZS 3,000/= halafu akamwambia yule mzee,''Ivo we mzee umeona? Nimenunua matikiti matatu kwa TZS 9,000/= tu badala ya TZS 10,000/=!!! Inaonesha we mzee ni mgeni kwenye masuala ya biashara eh?!?!?"
Wakati yule kijana anaondoka na gari lake, mzee akajisemea huku anacheka,"Watu bwana, yaani mtu amenunua matikiti matatu lakini bado anataka anifundishe masuala ya biashara! Hahahaha!!"
SWALI: Kwanini mzee ameweka bei zake kwa mtindo huu? Je, ni kweli mzee hajui biashara? Fafanua.
2. TUONGEZE BEI ILI KUSHINDANA NAO!
Kampuni moja ya magari nchini Ujerumani ilikuwa inafahamika kwa kutengeneza magari ya kifahari yanayouzwa ghali sana. Ghafla ikaibuka kampuni nyingine ya Kichina inayotengeneza magari kama yale ya Ujerumani, lakini wao sasa wanauza kwa bei ambayo ni nusu ya ile ya magari ya Ujerumani.
Kuona hivyo, meneja mauzo wa ile kampuni ya Kijerumani akamfuata Mkurugenzi wake ili kumweleza kuhusu ujio wa hii kampuni mpya inayotengeneza magari kama ya kwao na kuyauza kwa bei chee.
Meneja mauzo akamuuliza Mkurugenzi wake,"Tunafanyaje sasa kukabiliana nao sokoni?". Mkurugenzi akajibu,"Tuongeze bei ya magari yetu!"
SWALI: Kwanini mkurugenzi anafikiri kuongeza bei ya magari yao ndio njia bora ya kushindana sokoni? Fafanua.
NB: Kwa ambae yuko interested na tricks kama hizi, unaweza kuupitia uzi huu pia; GROWTH HACKING
#virus