Tujiandae kisaikolojia katiba ya CCM itapita

Tujiandae kisaikolojia katiba ya CCM itapita

Huey freeman

JF-Expert Member
Joined
Sep 20, 2013
Posts
593
Reaction score
248
Wengi mnajiuliza CCM wanapata wapi kiburi cha kuchakachua kila sheria na kanuni tangia mchakato huu wa katiba uanze.

Intelijensia yangu inaniambia ndani ya bunge la katiba wale wajumbe wa kundi la 201 wamekua wakilelewa kama yai wamefanywa marafiki na viongozi wakubwa na wamekua wakiekwa ktk mazingira rafiki yani ahadi za mbeleni hii ni ili kufanya waone aibu kusema hapana.

Kundi kubwa pale ndani ni CCM hivyo katiba itaegemea upande wao na UKAWA kutoka nje ndio chance yao, na hata maridhiano yakitokea leo kazi yote ya uchakachuzi itaingia dustbin na ukawa watapawa headline hivyo tusahau habari za ukawa kurudi bungeni CCM hawawataki Ukawa bungeni.

CCM hawataichezea hii chance 2/3 watahonga wajumbe hata jengo la makao makuu yao waliuze ili ipatikane pesa ya kuhonga wajumbe.

Kwa wananchi ndo watatumia vitisho ..." blackmail...". Wakiwaambia wanashida ya maji ,madawati, vitanda mahospitalini na blah blah nyingine pili watawapa hesabu za mabilioni yaliyotumika kuandaa katiba ya kichina tatu watawaambia msipo kubali hii itatengenezwa nyingine ila mtakula majani kwani serikali haitakua na pesa za kutosha kuwapa huduma za kijamii kuwajengea barabara hivyo chagueni moja katiba au huduma za kijamii kutokana na woga na ujinga wa watanzania watapitisha katiba ya CCM.


KIGUMU CHAMA CHA MAPINDUZI.
 
Mi naona wangetoka bungeni sisi wananchi wenyewe wenye uchungu na taifa tukaijadili hiyo katiba kwani hata sisi tuna utashi kama wao na tuna uwezo wakuijadili hiyo katiba wasizani wao kwa vile tumewachagua basi wao ndio wao hapana
 
Duuu kama ukweli hivi, ila hapo kwenye 2/3 ndo naona MAGAMBA yatagonga mwamba lazima
 
Wale waliotoka bungeni ni chanzo;
Wangepingana kwa hoja huko huko mjengoni.
 
Unafikiri ccm ni wajinga kiasi hicho, 2/3 zanzibar itapatikana hata kwa mtutu.
Sitta hawezi kua careless hivyo, urais wake utaamuliwa kutokana na upatikanaj wa katiba ya ccm
 
Urais mbona naona Mh.sana mzee WA viwango na speed ameshindwa hata kabla ya kuchukua fomu.Hivi bado anauota?.BMK Limemchapa mweleka WA jumla asahau safari ya MAGOGONI
 
katiba ya ccm itapita, kura nyingi hupatikana vijijini ambako leo huko ukimwambia zanzibar wanakunyonya, atakushangaa, ukimwambia mafisadi wanakula hela yako, atakushangaa na kusema hana hela hiyo ya kuliwa aitoe wapi! hata maana ya katiba hajui, japo hata ndani ya kundi la 201 wapo hasio jua hilo!
 
Tuko Tayari kabisaaa! Lakini wakae wakijua kwamba hapo watakapokamilisha kazi yao wakatoa katiba ya ccm ndio mwanzo wa mapambano mapya na makali ya kudai sio katiba mpya pekee bali katiba bora na tanganyika yetu ambayo haikuvaa koti la muungano!

wengi mnajiuliza ccm wanapata wapi kiburi cha kuchakachua kila sheria na kanuni tangia mchakato huu wa katiba uanze.

Intelijensia yangu inaniambia ndani ya bunge la katiba wale wajumbe wa kundi la 201 wamekua wakilelewa kama yai wamefanywa marafiki na viongozi wakubwa na wamekua wakiekwa ktk mazingira rafiki yani ahadi za mbeleni hii ni ili kufanya waone aibu kusema hapana.

Kundi kubwa pale ndani ni ccm hivyo katiba itaegemea upande wao na ukawa kutoka nje ndio chance yao, na hata maridhiano yakitokea leo kazi yote ya uchakachuzi itaingia dustbin na ukawa watapawa headline hivyo tusahau habari za ukawa kurudi bungeni ccm hawawataki ukawa bungeni.

Ccm hawataichezea hii chance 2/3 watahonga wajumbe hata jengo la makao makuu yao waliuze ili ipatikane pesa ya kuhonga wajumbe.

Kwa wananchi ndo watatumia vitisho ..." blackmail...". Wakiwaambia wanashida ya maji ,madawati, vitanda mahospitalini na blah blah nyingine pili watawapa hesabu za mabilioni yaliyotumika kuandaa katiba ya kichina tatu watawaambia msipo kubali hii itatengenezwa nyingine ila mtakula majani kwani serikali haitakua na pesa za kutosha kuwapa huduma za kijamii kuwajengea barabara hivyo chagueni moja katiba au huduma za kijamii kutokana na woga na ujinga wa watanzania watapitisha katiba ya ccm.


kigumu chama cha mapinduzi.
 
Back
Top Bottom