Tuition Chuo Kikuu cha Dar es Salaam

 
Kwa kweli mtoa maada alichokisema ni kweli kabisa kwani pale anapofundishia huyo mwalimu, amepanga majengo na ndugu yangu ambaye ana day care yake hapo. Its a great shame kwa mwanafunzi wa chuo kikuu kwenda tution, hiyo inadhihirisha jinsi gani watanzania tulivyo wavivu wa kusoma vitabu na kufikiria. Mkapa pamoja na ufisadi wake wote anawajua watanzania vizuri sana na hii inadhihirishwa na ule usemi aliousema kuwa watanzania ni wavivu wa kufikiria na wanafunzi wa chuo kikuu cha dar es salaam ambacho ndio chuo chenye hadhi kubwa nchini kwetu wanalihakiki hilo kwa kwenda tution.
 
tatizo ni madesa ndo maana hao wana X UDSM wanadiriki kufundisha Tution.Thank God sio wahadhiri maana nilianza kuona nyota nyota
 
wafanyeje wakati wananyimwa mikopo...............acha wafundishe tuition pengine itawasaidia kwani wengine wanategemewa kwao................
 
wafanyeje wakati wananyimwa mikopo...............acha wafundishe tuition pengine itawasaidia kwani wengine wanategemewa kwao................
Kwani tutition inaweza kuwa tofauti na discussion? Maana kuna discussion watu wengine huwa mabubu wanaandika kinachosemwa tu hata kama ni KASA.
Mie nadhani tuition as tuition haina tatizo kama uandaaji wa mtihani utamfanya mwanafunzi ajue alichofundishwa. Uelewa wa mwanafunzi unaweza kupimika vizuri na utungwaji wa mtihani wenye uwezo wa kupima maarifa. Kama mtu haelewi kitu na akaamua kukariri hata ende tuishen ya namna gani km mtihani ni mzuri lazima atapimika anapoishia.
Binafsi nimeshuhudia tuitiona hata vyuo vya Ulaya tena vyuo bora. Unapewa pesa unamfundisha mtu hususan wale wanaoresit. Hii si tuition?
 

Shukrani kwa kuleta hoja hii. Ni kweli wanafunzi waliomaliza BCom mwaka jana wanafundisha tuition kwa wanachuo wa mwaka wa pili wanaosoma Economics/Accounting...

Sidhani wanachuo kusoma tuition wanatatua tatizo sanasana ni kuanza kujenga tabia ya kutafuta workarounds badala ya kutafuta chanzo cha tatizo.

Kwa uelewa wangu mwanafunzi anayekubaliwa kuingia elimu ya juu ana uwezo (at least theoretically) wa kupigana na masomo anayokutana nayo. Kama wanachuo hawa wanashindwa kutumia fursa za lectures, tutorial sessions na group discussions na ku-resort kwenye tuitions then wameshindwa kutumia fursa ya uelewa wao kutatua chanzo cha matatizo yao....
 
Dear All Academician do not give them materials,the new generation at the Hill and other institutions at the higher learning they like spoon feeding and they are distorting the meaning of university.The library is the source of knowledge and at the hill there are very good Library and committed Lectures,the problem of this young generation they do not like to read but they like to pass examinations without reading,that is why when they complete their studies,they fail to compete in the job market.

I would like to challenge those students who are attending Tuition at that level to stop that shameful practice and real engage themselves in real academic arena.At university level a student supposed to be critical in analyzing different issue.

Elisante Yona - Former UDSM student - I was there for a number of years but I have never seen any student demanding tuition classes.This practice is a negative impact of cultural imperialism.

Thank you
 

Mabuba, nakushukuru sana kwa kutoa ufafanuzi. Kuna tatizo la watu humu jamvini kuanza kumjadili mtoa mada badala ya hoja. Wanaamini kitu kama kimeletwa na mtu fulani na siyo wengine. Kwa hiyo humu ndani kuna tatizo jingine mithili ya tuition ulizoongelea.

Hao vijana hawawezi kuacha tuition. Wengi wameingia vyuoni na alama za kulazimisha (kwa kusoma tuition huko sekondari) au za kupika (kwa kuiba mitihani. Baada ya kufika chuo, wanakutana na starehe isiyo na mfano (baada ya kupata mafweza kutoka Bodi ya mikopo) na wengine, tena wengi sasa wanafanya siasa (wanafurahi na kukenua meno wakivaa uniform za kijani na kuitwa Diamond kuongea na wasanii). Ukiongeza na matatizo ya miundobinu na walimu, vijana hawana jinsi. Watatafuta tuition tu! Hapa hakuna mtu wa kuwazuia kwani wanataka kupasi kwa gharama yoyote. Namwomba Mungu anipe angalau miaka 10-20 zaidi ili nione hawa vijana wetu watamudu vipi huu utandawizi!!!😕
 

SUA ndo pale mnaposoma mambo ya uchumi wa nyumbani na lishe then mnaenda kuwa Ma bank teller??!!! nyie hamuhitaji tuisheni vitu vyenu laini vinaeleweka hata ukiwa umelelala pale Hostel 5 karibu na round top unaelewa tuu...hahaaaa
 
SUA ndo pale mnaposoma mambo ya uchumi wa nyumbani na lishe then mnaenda kuwa Ma bank teller??!!! nyie hamuhitaji tuisheni vitu vyenu laini vinaeleweka hata ukiwa umelelala pale Hostel 5 karibu na round top unaelewa tuu...hahaaaa

Kigogo,

Naomba uhamishie hii post yako kwenye jokes. Watu wana familia, zinazokula na kuishi kwa sababu ya hiyo shule na kazi unazojaribu kuzidhalilisha. Tafadhali sana watendee haki wenzio kama ambavyo ungependa kutendewa. Tukianza kuzichambua shule na ajira za watu sina hakika kama wewe mwenyewe utapona!!
 
Afadhali na wewe umeliona hilo. Kuna watu hujadili vitu visivyo na tija kabisa. Pitia mjadala wa Chuo cha Morogoro. Binafsi naona hizi hasa ndio sababu za nchi yetu kuwa hivi. Maana unaweza ukasoma hoja ukakumbana na matusi au kebehi. Watu hawajadili facts. Inasikitisha na pia inawezekana ndio mfumo wa elimu uliotufikisha hapa.
 
Jamani ninachokiongelea hapa ni jambo la ukweli na sio uzushi. Pia lazima tutofautishe programme na tution. Pre entry ni programme na sio tution. WanaJF tafadhari kama yupo yoyote anayeishi Changanyikeni akaulize hilo. Hii ni aibu kuu kwa UDSM.

Mimi nitaenda kuuliza. Hilo bango la chuo cha takwimu nililichukua wakati nikihoji ile 'as' ni domain gani ya tovuti hapa duniani, ingawa sikupata jibu. Ila nikuulize swali; Kwa kuwa kuna watu wamesema ni program maalum ya kuwainua pre-entry female students, je wewe ulikutana na wasichana tu au na wavulana walikuwepo?
 
hapa mtaumiza vichwa bure. hakuna hakuna namna chuo kikuu cha daresalaamu kinaendesha masomo ya ziada (tuition) kwa wanafunzi wake. mtapiga kelele ,hamtapata jibu, wasiwasi wenu unaondolewa mkienda hapo chuoni mtaupata ukweli, ukweli haupo ktk kuona kundi kubwa la watu wanasema wanatoka tuition ndyo kuwa ni wanafunzi wa UDSM., wengi mumesoma chuo hicho, na munajua ukweli nini tofauti kati ya chuo kikuu na shule zilizo chini ya level ya chuo kikuuu- yaani sekondari.
ni juavyo mimi ni kuwa wakati madarasa ya udsm yakiwa wazi, kuna watu wa mtaani huyatumia kufundishia wanafunzi wa sekondari. lakini yote ya yote, ivi kweli wana JF wote hakuna mwenye ndugu ambaye yupo pale UDSM anasoma ukamwuliza na akakupa ukweli juu ya hilo???. mtoa maada nae anazungumza kwa hisia tu - na kuweka lugha za kisanii kwa jambo analoliita makini- eti "watoto wa mukandara" hamuoni analeta usanii hapo.

suala la pre- entry ni kweli lipo na limeanza siku nyingi tangu 1997. ni kwamba kulikuwa na utaratibu wa kuangalia wanafunzi wa kike wanaosoma masomo ya sayansi, waliokuwa na maendeleo mazuri , lakini hawakufaulu vizuri form six, hao huitwa na hukaa chuoni wansoma kwa muda kama wa miezi 2 kabla ya mwaka wa masomo kuanza ,baadae huungana na wale wenzao ktk kozi za sayansi.kundi hilo huwezi kuliona wakati huu, utaweza kuwaona wakati ambao wanachuo wote wapo likizo ya mwisho wa mwaka. hata hivyo hilo kundi huishi kweye mabweni ya chuo na si vinginevyo. suala la kwanini watoe upendeleo huo, lipo wazi. hakuna asiyejua uchache wa wanawake ktk fani za sayansi. binafsi nina ushahidi, nilisoma mlimani 1998, na niliona hao watu wa pre- entry, kati yao, ninawajua wawili ambao tayari wana PhD sasa ivi. anateyaka kuni PM naweza mpa details karibu
 

Jamani pamoja na kukubaliana na hali hii inawezekana kabisa ikawepo hapo UDSM, naomba niseme kitu ambacho nina uhakika nacho kwa vile kuna watu ninawafahamu ambao wanafanya kazi na wanasaidia katika hili kwa malipo kabisa.

Chuo kikuu kishiriki cha madaktari Muhimbili hili suala lilianza siku nyingi huenda ni miaka 3 au 4 sasa. Mwenye nafasi afanye uchunguzi. Pale Aga khan kuna Dr Shaffik ana madarasa ya tution kabisa ambayo wateja wake wengi ni mabinti wa MD pale Muhimbili na imekuwa muda mrefu tu!

Natumaini kwa MD yeyote aliyepo hapa JF atakubaliana na mie kuhusu viwango vya madaktari wanaotoka Muhimbili sasa vikoje. Sijui tunajenga taifa la namna gani lakini kwa ujumla nchi yetu inahitaji overhaul ya nguvu ndani ya system mfumo wetu ni mchafu umekuwa na CCM haitaweza kwa vile haina dhamira tena inafaidika nayo.. Nawakilisha
 
Kaka tuition ina madhara makubwa sana ktk jamii.. Huku ulaya haya mambo ya tuition ni kama vile hakuna. Ila kwa Tanzania imekuwa kama sehemu mojawapo ya maisha (Kujiongezea kipato). Yani bila tuition hujafaulu. Moja ya madhara ya tuition ni kwamba inapelekea walimu kutofundisha vizuri darasani ili wanafunzi waende tuition. Je kwa wasio na uwezi inakuwaje?....Hii issue ya kwamba Tz hadi university wanasoma tuition ni kali kwa kweli, i cant imagine situation kama hiyo.. Tuko nyuma sana kitaaluma ingawa siku zote tunaamini kwa ulimu ya bongo iko nondo.. Lakini kwa waliosoma expecially engineering ulaya nadhani wananielewa material yanayopatikana huku...MAMBO YA TUITION HAKUNA KAKA ...
 
Je wewe ni mojawapo wa wanafunzi? If yes then the discussion ends.
 
Nadhani hukuwaelewa, labda walikuambia wanatoka kufanya TUTORIAL na sio tution,
Sikubaliani nawe hata kwa asilimia 1, kwamba kunakitu kama hicho hapo UD na hata kwenye any tertiary institution.
 
Mkubwa siku hizi hakuna Chuo kikuu kishiriki... ni fully fledged university na inaitwa MUHAS kwa kifupi.
Huyo Dr. Shafiki inamaana anafundisha mabinti tu? wanamlipa hela au ni kitu ingine...
Ni kweli kiwango kimeshuka kutokana na intake ni kubwa sana ( ≥200) na walimu ni wachache sana! Weill-Bughando nadhani ipo juu cku hizi in terms of quality ya product zao.
 
Weye washangaa tuition? Waijua pass mark ya mitihani udsm? Ulizia!
Pass mark ya Udsm ni 40%,wewe unataka kusema nini au unataka kuharalishaTuition chuo kikuu kwa hiyo 40%?
nakupatia wasiwasi kama umefika chuo kikuu wewe!!!!
au unasoma secondary ya kata?
 
Pre entry Udsm imefutwa mwaka huu 2009,hakuna wanafunzi walioingia mwaka wa masomo 2009-2010 kwa kupitia programu hiyo ya pre-entry!!!
kwa kawaida pre-entry ilikuwa inafanyika miezi hata kabla ya chuo kufunguliwa na si kipindi ambacho chuo kipo kwenye masomo,mtoa mada katoa mada kipindi ambacho chuo kipo wiki ya 6.
Hiyo hiyo si pre-entry!!!na Tutorial au seminar tunajua zinakofanyikia kwa pale UDSM,nadhani walipita Udsm tunajua kule Yombo sio sehemu ya kufanyia seminar wala hizo tutorial.
Nimetaja Yombo(Sio yombo vituka) hii ni jina ya moja ya Jengo la mihadhara ambalo liko karibu kabisa na barabara iendayo Changanyikeni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…