Tuitazame Falsafa ya Kauli ya Askofu Pengo

Tuitazame Falsafa ya Kauli ya Askofu Pengo

Socratic

JF-Expert Member
Joined
Dec 18, 2014
Posts
568
Reaction score
308
Kauli ya askofu Pengo kwa maoni yangu inaweza kuangaliwa kwa falsafa tofauti kama ifuatavyo.

1.Kiimani-Alichosema kuhusu free will ( uhuru wa kuamua) ni sahihi na hakuna mkristo wa kweli awezaye kupinga hili kimaandiko (irrefutable) katika ulimwengu wa kiroho, wanaopinga wanatumia nadharia nyingine.

2.Kisiasa-Alichosema askofu Pengo si sahihi kwa vile kina maslahi kwa makundi fulani kisiasa. wapo wanaodai katiba inayopendekezwa ilishachakachuliwa na kwa hiyo haifai na ndiyo maana wanaona maaskofu waliotoa waraka wako sahihi kuwashawishi waumini wao waipigie kura ya hapana.

3.Kijamii-Askofu Pengo yuko sahihi kwa alichokisema maana kikatiba kila mtu anayo haki na uhuru wa kutoa maoni yake bila kubughudhiwa na mtu yeyote. Na Askofu ametumia haki na uhuru wake wa kutoa maoni yake kama mtanzania yeyote. Kuwa askofu hakumpokonyi uhuru huo. Hapa JF watu wana mitazamo tofauti kuhusu mambo mengi lakini ndio msingi wa kuwepo jukwaa hili. Kila mtu anao uhuru kuchangia na kutoa mawazo yake.

4. Kisheria- Alichosema askofu Pengo si sahihi kwa vile kuna sheria ya collective responsibility kwenye canon law. Yeye kama mjumbe wa TEC hakufanya vema kupingana na tamko lililotolewa na maaskofu wenzake maana linaweza kuwachanganya waumini ambao husikiliza na kufuata maelekezo kutoka kwa viongozi wao na pia kuwaembarass maaskofu wenzake.

Kwa minajili hiyo askofu Pengo ametumia falsafa namba 1 na namba 3 katika kile alichosema na hivyo yuko sahihi na watu wengine wanampinga kwa kutumia falsafa namba 2 na 4 na hivyo hayuko sahihi.

Swali ni je? Askofu Pengo alikuwa na haki kutumia falsafa alizotumia kutoa kauli yake? kama ndiyo kwa nini? na kama sivyo alipaswa kutumia falsafa gani na kwa nini? Wapi ulipo mpaka kati ya falsafa moja na nyingine?

karibuni tuchangie.
 
Mada hii ni nzuri, ila haijapata wachangiaji tangu ilipopostiwa siku mbili zilizopita,nimenote pengine sababu imekaa kimzani zaidi na,kwa maana haina tuhuma wala utetezi.

Mada nyingi za humu JF zinazopata wachangiaji wengi ni zile zenye tuhuma za moja kwa moja au shambulizi fulani kwa mtu,hapo ndipo asili ya mtanzania inapofahamika!

Turudi kwenye mada, Sina tatizo na mhadhama kardinali,japo ni mmojawapo wa watanzania tusioikubali rasimu ya katiba iliyochakachuliwa kutoka katika rasimu ile iliyokusanywa kutoka kwa maoni rasmi ya watanzania.

Sina uhakika na msimamo wa kisiasa wa baba askofu Pengo kama mojawapo ya haki zake za kikatiba(hana zuio hilo kwa nafasi yake),ila nikiitazama hotuba yake kwa undani,kazungumza kwa nafasi yake kama polycarp pengo raia wa Tanzania, si mwadhama polycarp kardinali pengo askofu mkuu wa jimbo la Dsm. Kwa maana kama mmojawapo wa wajumbe wa baraza la maaskofu alishiriki wala hakususia vikao vilivyoandaa na kupitisha waraka wa kuipinga katiba mpya.

Kwa upande wa pili amefafanua madhara yawezayo kutokea kutokana na kampeni hizi mbili zinazosigana(ikumbukwe hakuna mahala niliposikia aidha kwa kauli ya moja kwa moja au lugha ya mkato, aliposema kwamba wananchi tuipigie kura ya ndiyo katiba pendekezwa)pengine kosa alilofanya ni kutozungumzia upande wa serikali unaofanya kampeni za kuhamasisha kura ya ndiyo.

Haina sababu ya kumtukana hadharani mzee huyu kwa ajili ya hilo
 
Kiongozi wa kanisa katoliki nchini Tanzania mwadhama kadinali Polcarpy Pengo ameligawa vibaya kanisa hilo nchini humo, imethibitika.

Pengo alitoa matamshi yanayolenga kuikubali katiba inayopendekezwa ambayo ilianzishwa kwa mizengwe mikubwa na lililokuwa bunge maalum la katiba hivi karibuni.

Wengi wa waumini wa kanisa hilo wanaipinga katiba hiyo pendekezwa huku wakidai kuwa haifuati na kutoa mwongozo wa misingi ya utawala bora pamoja na kutatua fumbo gumu la muundo wa muungano unaounda Tanzania.

Kutokana na matamshi hayo ya kadinali Pengo, waumini wengi wa kanisa hilo nchini Tanzania wamemuona kama msaliti.

Pengo pia alishambuliwa vikali na baadhi ya wasaidizi wake pamoja na askofu wa kanisa la ufufuo na uzima nchini humo.

Kadinali Pengo anatarajiwa kutoka na kutoa tamko katika ibada ya pasaka wiki ijayo kuhusu mustakabali wa kanisa hilo pamoja na sontofahamu kwa viongozi wengine wa dini ya kikristu waliomshitumu kutokana na kauli yake hiyo. Aidha anatarajiwa kuomba radhi kutokana na mgawanyiko huo mkubwa uliojitokeza.
 
Mkuu kwani uko nje ya nchi yetu?
Naona kama umeandika ukiwa nje.
Je unaweza kuweka source?
 
Ushauri wangu juu ya Escrow haukueleweka - by Werema, Frederick
Je Pengo atasema, "Ushauri wangu kuhusu Katiba haukueleweka"
 
Usahihi hajaligawa kanisa katoliki bali amejigawa yeye mwenyewe na kulisaliti kanisa kwa ajili ya siasa za chama kibovu cha magamba.
Amegeuka kuwa Yuda Iskarioti. Anapaswa kutubu.
 
hivi rukwa watu wanamatatizo ya akili sana eti, kwanza arfi, pinda, now pengo duuuuhh labda ni chakula wanakula huko kinaharibu uwezo wa kufikiria
 
Pengo alitoa matamshi yanayolenga kuikubali katiba inayopendekezwa ambayo ilianzishwa kwa mizengwe mikubwa na lililokuwa bunge maalum la katiba hivi karibuni.

Wengi wa waumini wa kanisa hilo wanaipinga katiba hiyo pendekezwa huku wakidai kuwa haifuati na kutoa mwongozo wa misingi ya utawala bora pamoja na kutatua fumbo gumu la muundo wa muungano unaounda Tanzania. .
Sasa kama wengi wa waumini wa kanisa hilo hawakubaliani na Pengo, iweje useme ameligawa? Nilidhani utasema karibu nusu ya waumuni wanampinga na nusu nyingine wanamkubali, hapo ndipo kuligawa. Hivi mnataka kusema kwamba kama isingetoka kauli ya Pengo, hakuna wakatoliki ambao wangeipigia kura ya NDIYO? Akina Pinda na Membe ni wakatoliki, wangeipigia kura ya HAPANA?
 
Kiongozi mkuu wa kanisa katoliki nchini Tanzania mwadhama kadinali Polcarpy Pengo ameligawa vibaya kanisa hilo nchini humo, imethibitika.

Pengo alitoa matamshi yanayolenga kuikubali katiba inayopendekezwa ambayo ilianzishwa kwa mizengwe mikubwa na lililokuwa bunge maalum la katiba hivi karibuni.

Wengi wa waumini wa kanisa hilo wanaipinga katiba hiyo pendekezwa huku wakidai kuwa haifuati na kutoa mwongozo wa misingi ya utawala bora pamoja na kutatua fumbo gumu la muundo wa muungano unaounda Tanzania.

Kutokana na matamshi hayo ya kadinali Pengo, waumini wengi wa kanisa hilo nchini Tanzania wamemuona kama msaliti.

Pengo pia alishambuliwa vikali na baadhi ya wasaidizi wake pamoja na askofu wa kanisa la ufufuo na uzima nchini humo.

Kadinali Pengo anatarajiwa kutoka na kutoa tamko katika ibada ya pasaka wiki ijayo kuhusu mustakabali wa kanisa hilo pamoja na sontofahamu kwa viongozi wengine wa dini ya kikristu waliomshitumu kutokana na kauli yake hiyo. Aidha anatarajiwa kuomba radhi kutokana na mgawanyiko huo mkubwa uliojitokeza.

Hakuna mgawanyiko wowote. Hata article yenyewe imeshindwa kuthibitisha.
Pengo kachemsha. Na wala sio mara ya kwanza yeye kufanya "u-zito kabwe".
 
Kiongozi mkuu wa kanisa katoliki nchini Tanzania mwadhama kadinali Polcarpy Pengo ameligawa vibaya kanisa hilo nchini humo, imethibitika.

Pengo alitoa matamshi yanayolenga kuikubali katiba inayopendekezwa ambayo ilianzishwa kwa mizengwe mikubwa na lililokuwa bunge maalum la katiba hivi karibuni.

Wengi wa waumini wa kanisa hilo wanaipinga katiba hiyo pendekezwa huku wakidai kuwa haifuati na kutoa mwongozo wa misingi ya utawala bora pamoja na kutatua fumbo gumu la muundo wa muungano unaounda Tanzania.

Kutokana na matamshi hayo ya kadinali Pengo, waumini wengi wa kanisa hilo nchini Tanzania wamemuona kama msaliti.

Pengo pia alishambuliwa vikali na baadhi ya wasaidizi wake pamoja na askofu wa kanisa la ufufuo na uzima nchini humo.

Kadinali Pengo anatarajiwa kutoka na kutoa tamko katika ibada ya pasaka wiki ijayo kuhusu mustakabali wa kanisa hilo pamoja na sontofahamu kwa viongozi wengine wa dini ya kikristu waliomshitumu kutokana na kauli yake hiyo. Aidha anatarajiwa kuomba radhi kutokana na mgawanyiko huo mkubwa uliojitokeza.



Chanzo cha habari??
Huna chanzo cha habari habari yako inakuwa porojo tu na si vinginevyo!
Hivi mbona wabongo tunapenda kuropoka sana (kujenga dhana ya kufikirika zaidi kuliko ukweli)..?

Je lini umeonana na Pengo akakueleza yote hayo?
Au ni kwa vile una tarakilishi na uwezo wa kuchapa herufi ndio ukaamua kuleta habaari zisizo na chanzo?
Au ni ufupisho wa uliyoyasoma humu JF..?

Hebu tujaribu kufikiria juu ya kile tunachotaka kupost angalau kwa dk 2 kabla ya kufanya hovyo!

Samahani kama ntakuwa nimekuboa ila ndio nimewasilisha maoni yangu!
 
Sasa kama wengi wa waumini wa kanisa hilo hawakubaliani na Pengo, iweje useme ameligawa? Nilidhani utasema karibu nusu ya waumuni wanampinga na nusu nyingine wanamkubali, hapo ndipo kuligawa. Hivi mnataka kusema kwamba kama isingetoka kauli ya Pengo, hakuna wakatoliki ambao wangeipigia kura ya NDIYO? Akina Pinda na Membe ni wakatoliki, wangeipigia kura ya HAPANA?
mkuu kwa nn usingeopt kukaa kimya tu?hapa ndo umeandika nn?
 
Kiongozi wa kanisa katoliki nchini Tanzania mwadhama kadinali Polcarpy Pengo ameligawa vibaya kanisa hilo nchini humo, imethibitika.

Pengo alitoa matamshi yanayolenga kuikubali katiba inayopendekezwa ambayo ilianzishwa kwa mizengwe mikubwa na lililokuwa bunge maalum la katiba hivi karibuni.

................
.

Ni vizuri ieleweke Kardinali Pengo siyo kiongozi mkuu wa kanisa Katoliki Tanzania bali ni Askofu mkuu wa jimbo kuu la DSM tu.
Aliyosema kwa ujumla wake natofautiana nae. Kuna wakati govt ilitaka kuongeza kwny mitaala ya shule ya msingi topic ya mambo ya kujamiana na Kanisa likatoa tamko la kuwataka waamini walipinge. Sasa mamlaka waliyotumia kupinga hilo ndio hayohayo jukwaa la Wakristo walitumia kuipinga "kijarida cha Chenge" a.k.a katiba pendekezwa
 
Rejea namba 2 " alichosema Pengo kina maslahi ya makundi" hivyo hayuko sahihi. Swali. Je walichosema maaskofu na baraza si kwa maslahi ya makundi? Tuondolee ukichaa wenu wa viroba hapa
 
Tupe ushahidi wa kugawanyika kwa kanisa Takatifu Katoliki mkuu,naamini hili ndilo kanisa halali la Kristu,kwani Herode mwakilishi wa kanisa hakuona kosa la kumsulubu Kristo Msalabani lakini alilazimishwa amhukumu
 
Mada hii ni nzuri, ila haijapata wachangiaji tangu ilipopostiwa siku mbili zilizopita,nimenote pengine sababu imekaa kimzani zaidi na,kwa maana haina tuhuma wala utetezi.

Mada nyingi za humu JF zinazopata wachangiaji wengi ni zile zenye tuhuma za moja kwa moja au shambulizi fulani kwa mtu,hapo ndipo asili ya mtanzania inapofahamika!

Turudi kwenye mada, Sina tatizo na mhadhama kardinali,japo ni mmojawapo wa watanzania tusioikubali rasimu ya katiba iliyochakachuliwa kutoka katika rasimu ile iliyokusanywa kutoka kwa maoni rasmi ya watanzania.

Sina uhakika na msimamo wa kisiasa wa baba askofu Pengo kama mojawapo ya haki zake za kikatiba(hana zuio hilo kwa nafasi yake),ila nikiitazama hotuba yake kwa undani,kazungumza kwa nafasi yake kama polycarp pengo raia wa Tanzania, si mwadhama polycarp kardinali pengo askofu mkuu wa jimbo la Dsm. Kwa maana kama mmojawapo wa wajumbe wa baraza la maaskofu alishiriki wala hakususia vikao vilivyoandaa na kupitisha waraka wa kuipinga katiba mpya.

Kwa upande wa pili amefafanua madhara yawezayo kutokea kutokana na kampeni hizi mbili zinazosigana(ikumbukwe hakuna mahala niliposikia aidha kwa kauli ya moja kwa moja au lugha ya mkato, aliposema kwamba wananchi tuipigie kura ya ndiyo katiba pendekezwa)pengine kosa alilofanya ni kutozungumzia upande wa serikali unaofanya kampeni za kuhamasisha kura ya ndiyo.

Haina sababu ya kumtukana hadharani mzee huyu kwa ajili ya hilo

Nimependa sana mchango wako mkuu...ni kweli post hii imechukua muda kupata wachangiaji. Nafurahi kwa kufungua ukurasa. Nia yangu kubwa ni kutaka wanaJF tufike mahali tuchangie mawazo kama great thinkers. (Great people discuss ideas) na sio kuchangia kishabiki tu au kwa kulinda itikadi zetu za kidini au kisiasa.
 
Back
Top Bottom