Wanajeshi wetu hata wangelikuwa huko bila mandate ya vita kupewa na Umoja wa mataifa hawawezi kusaidia kitu.
Mikataba ya kiulizi ya Umoja wa mataifa inamizengwe sana.
Ukisimuliwa masharti wanayopewa walinzi hao wa amani utabakia kinywa wazi na kukosa maana ya nia halisi ya kupelekwa kwa wanajeshi hao.
Ndiyo maana raia wa Kongo wamepaza sauti zao kulaani uwepo wa walinzi wa kimataifa ambao hawajawasaidia lolote na adha za hayo machafuko ya umwagikaji damu yaliyochukua miaka nenda rudi.