Tuikubalie DR Congo kujiunga na EAC?

Ujamaa ni umasikini na udikteta.

Afrika tuachane na ujamaa tukumbatie ubepari.

Ndio suluhu ya matatizo yetu.
 
Kwenye hili tunaweza fanikiwa kama tukianza kwanza kuwa na Sera Moja ya Kilimo (Common Agricultural Policy) kama walivyofanya Umoja wa Ulaya mwaka 1962. Nikipata wasaa ntalielezea vizuri hili.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwenye hili tunaweza fanikiwa kama tukianza kwanza kuwa na Sera Moja ya Kilimo (Common Agricultural Policy) kama walivyofanya Umoja wa Ulaya mwaka 1962. Nikipata wasaa ntalielezea vizuri hili.

Sent using Jamii Forums mobile app
Tatizo bajeti zetu zimetofautiana vipaumbele, sasa unafikiri ni rahisi kuwa na sera moja ya kilimo.
 
Yale yale ya Umoja wa Ulaya na Uturuki na Sasa Uturuki imegeuzwa kambi ya kuzuia wakimbizi wasifike Ulaya kwa kulipwa mamilioni ya Euro na kuahidiwa ahadi hewa za kukubaliwa uanachama siku za usoni.

Kumbuka pia hii DRC hali yake tete ya kiusalama imechangiwa kwa kiasi kikubwa na baadhi ya nchi wanachama wa EAC (Uganda & Rwanda) kwa kufadhili uasi.

Huoni kuwa mwanachama kamili wa EAC ni fursa kwa nchi jirani (zenye makundi ya waasi huko) kuhusika kikamilifu kuimarisha usalama hasa huko Mashariki?
 
Tatizo bajeti zetu zimetofautiana vipaumbele, sasa unafikiri ni rahisi kuwa na sera moja ya kilimo.
Kwanini isiwe rahisi ? Sera ni mwongozo wa kisiasa ambao umeandikwa kitaalamu ili kutimiza malengo fulani ya kimaendeleo kwenye nchi wanachama. Tatizo lako hapa lipo wapi ?
 
Huoni kuwa mwanachama kamili wa EAC ni fursa kwa nchi jirani (zenye makundi ya waasi huko) kuhusika kikamilifu kuimarisha usalama hasa huko Mashariki?
Wapi nimeandika kwamba Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo awe mwanachama kamili wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ? Nadhani hujaelewa nilichokiandika hapo au aidha umeninukuu vibaya.
 

Kwa hiyo kujiunga kwao ni kwa sababu ya rasilimali zao? Vipi SADC? Kwa nini na wao wasijiunge? Au tutafute nchi nyingine yenye rasilimali nyingi? Watanzania chapeni kazi waswahili walisema mtegemea cha nduguye hufa masikini. Rasilimali tulizonazo Tanzania hatuna sababu ya kutafuta miungano ya kishenzi. Tuchape kazi na kujikwamua kwenye matatizo yetu hatuna mjomba wa kumtegemea. Ushirikiano sawa sio kuwa tegemezi au kungoja vya bure maana siku zote vya bure vina gharama.
 
Kwanini isiwe rahisi ? Sera ni mwongozo wa kisiasa ambao umeandikwa kitaalamu ili kutimiza malengo fulani ya kimaendeleo kwenye nchi wanachama. Tatizo lako hapa lipo wapi ?
Mazingira yetu ya kisiasa yametofautiana baina ya nchi na nchi.

Utekelezaji wa hizo sera utategemea zaidi utashi wa kisiasa wa mtawala ndani ya nchi husika, je kama uongozi ukibadilika na mtawala mpya asizipende?
 

Kwa faida yao.
 
Wapi nimeandika kwamba Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo awe mwanachama kamili wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ? Nadhani hujaelewa nilichokiandika hapo au aidha umeninukuu vibaya.
Umeandika asiwe mwanachama kamili ila mimi na mtizamo tofauti yaani kama akiwa mwanachama kamili ndio uwezekano wa hizo nchi jirani kuhusika kudumisha usalama huko Drc Mashariki utapanuka zaidi kuliko Sasa.
 
Ujamaa ni umasikini na udikteta.

Afrika tuachane na ujamaa tukumbatie ubepari.

Ndio suluhu ya matatizo yetu.


Mkuu suluhu ya matatizo yetu sio itikadi ya ujamaa au ubepari. Angalia vizuri nini kinaitafuna Afrika? Kwa nini Wazungu hawaishi kuwakopa wamatumbi na kuwapa misaada kila uchwao?
 
Mazingira yetu ya kisiasa yametofautiana baina ya nchi na nchi.

Utekelezaji wa hizo sera utategemea zaidi utashi wa kisiasa wa mtawala ndani ya nchi husika, je kama uongozi ukibadilika na mtawala mpya asizipende?
Mazingira ya kisiasa ya nchi zote duniani hayako sawa, hata yale ya nchi zenye viwanda duniani za G7 zimetofautiana lakini kuna baadhi ya mambo wamekubaliana.

Ndani ya Umoja wa Ulaya kwenyewe wametofautiana sehemu lakini walitengeneza Sera moja ya kilimo (Common Agricultural Policy) ambayo mbali na changamoto za hapa na pale ilifanya kazi mpaka leo.

Nchi za Benelux (Belgium, Netherlands and Luxembourg) zipo ndani ya Umoja wa Ulaya lakini huwezi kuzilinganisha kisiasa na kiuchumi na nchi kama Ufaransa, Ujerumani na Italia. Sasa hawa wenzetu waliwezaje kufanya hivi na kwanini sisi tushindwe ?

Jibu ni rahisi sana: The Principle of Relative Advantage, ambapo hata kama tutasaini hiyo sera ya pamoja ya kilimo haimaanishi kwamba kila nchi itakuwa inafanya shughuli za kilimo bali ni kwamba kila nchi itatoa mchango ambao utainufaisha kwa kile ilichotoa. Sera moja ya kilimo (Common Agricultural Policy) haimaanishi kwamba kama Tanzania wanazalisha Korosho basi na Kenya ni lazima wazalishe korosho.

Mfano mzuri: Tanzania na Uganda zinaweza kuwa ndiyo sehemu ambazo shughuli za kilimo zinafanyika kwa wingi ambapo hata nchi ambazo hazitakuwa zinafanya kilimo kwa wingi kama Rwanda, Kenya na Burundi zitakuwa zinatoa mchango wa ruzuku kwa wakulima walioko kwenye nchi zote wanachama.

Lengo kubwa la Sera moja ya kilimo (Common Agricultural Policy) kwa nchi wanachama siyo kuzalisha mazao kwasababu ya ushindani, bali malengo makuu ni Ulinzi wa chakula (Food Security) na kuzuia utegemezi wa mazao na bidhaa muhimu kutoka nchi za nje (Reducing Dependence on foreign imports).
 
Umeandika asiwe mwanachama kamili ila mimi na mtizamo tofauti yaani kama akiwa mwanachama kamili ndio uwezekano wa hizo nchi jirani kuhusika kudumisha usalama huko Drc Mashariki utapanuka zaidi kuliko Sasa.
Hapa sijakuelewa vizuri, hebu elezea zaidi.
 
Hapa sijakuelewa vizuri, hebu elezea zaidi.
Hizi nchi za Rwanda na Uganda (wanachama wa EAC) zimekuwa zikitajwa kuhusika na mzozo wa huko Mashariki mwa Drc kwa muda sasa na pia kuna makundi ya waasi kutoka hizo nchi yanayoendesha Vita huko Drc.

Kama Drc itakuwa mwanachama kamili wa EAC ina maana ni rahisi zaidi kwa hizi nchi kujitolea zaidi kushiriki kumaliza mzozo huko mashariki mwa Drc na zile shutuma za wao kuhusishwa na huo mgogoro zitapungua au kukosa nguvu.
 
Needless to read. Kwanza hii jumuia ya Afrika Mashariki ina faida gani kwa wananchi. Ni siasa tu za pwagu na pwaguzi.

Ukinunua kitu ktk nchi moja kuingiza kwenye nchi nyingine unapambana na vikwazo vya tariff kibau, ukitaka kusafiri hadi passport na kwenda hiyo Congo hadi ununue Visa. Hamna kitu ni siasa tu.
 
Rwanda na Burundi wako ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki lakini migogoro yao imetushinda Tanzania, Kenya na Uganda mpaka leo. Imetuletea gharama kubwa na upotezaji mwingi wa muda na rasilimali, unadhani Kongo ambayo ni nchi kubwa ndiyo tutaiweza ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…