Fundi Madirisha
Senior Member
- Jun 30, 2020
- 184
- 987
Tuna imani kabisa kua Kamati Kuu ya CHADEMA si kikao cha mtu mmoja na wala si sauti moja. Kama haikukaa kujadili majina ya viti maalum ya kinamama 19 na ikathibika kua haikupokea Orodha ya majina kama alivyosema mkurugenzi wake Dr Mahela maana yake NEC imeudanganya umma na ni jinsi.
Mbowe na Mnyika ni wanasiasa wazoefu siyo wajinga, wanaelewa itifaki za kila utaratibu. Hivi wanawachukia kinamama hao kiasi gani mpaka wawakane? Dunia nzima inaona ni kama mchezo unachezwa kuwasingizia bila kujua huu mchezo ni wa jambo nyeti.
Ombi langu kwa CHADEMA ni kutumia wanasheria kuishtaki NEC ithibitishe na Dr Mahera amtaje huyo katibu mkuu aliyepeleka majina kwa ushahidi. Ilithibitika kua ni uongo na nyaraka zimeghushiwa basi NEC isitambilike ikataliwe, Makamishna waliohusika katika hii jinai washtakiwe mahakamani na wafungwe jela.
Mahakama yetu isimamie haki katika hili ijiepushe na siasa isije kulivuruga taifa.
Mbowe na Mnyika ni wanasiasa wazoefu siyo wajinga, wanaelewa itifaki za kila utaratibu. Hivi wanawachukia kinamama hao kiasi gani mpaka wawakane? Dunia nzima inaona ni kama mchezo unachezwa kuwasingizia bila kujua huu mchezo ni wa jambo nyeti.
Ombi langu kwa CHADEMA ni kutumia wanasheria kuishtaki NEC ithibitishe na Dr Mahera amtaje huyo katibu mkuu aliyepeleka majina kwa ushahidi. Ilithibitika kua ni uongo na nyaraka zimeghushiwa basi NEC isitambilike ikataliwe, Makamishna waliohusika katika hii jinai washtakiwe mahakamani na wafungwe jela.
Mahakama yetu isimamie haki katika hili ijiepushe na siasa isije kulivuruga taifa.