Tuache kudharau Watanzania wenzetu

Determinantor

Platinum Member
Joined
Mar 17, 2008
Posts
61,371
Reaction score
100,422
Hii biashara ya kusema Watanzania ni Wavivu, hawana akili sijui hawana njaa ni udhalilishaji! Hawa ndio walitusomesha kwa kuchoma mkaa, kwa kutembea kwa miguu zaidi ya 20km kwenda sokoni kuuza uwele,.mahindi au mtama, hawa ndio wanaoamka asubuhi na kwenda Shamba wakimuomba Mungu mvua japo inyeshe. Hawa hawa ndio waliowapigia kura baada ya kuwarubuni, eti Leo tunawaita Wavivu?

Inauma sana Aisee, tumewanyima elimu, tukawaacha na magonjwa yao, wakafiwa wakalia wakazika wakasahau, kisha Leo tunawaita Wavivu!!!! Mungu atuepushe.
 
Your talking nonsense bro
 
Your talking nonsense bro
Asante kwa kusoma Nonsense, si mmeshapata kura! Njaa haifichiki, sema utakachosema ila njaa haifichiki, acheni kudharau Watanzania. Hakuna mpuuzi hata mmoja kati yenu nyote anayemlisha Mtanzania zaidi ya yeye mwenyewe
 
Hebu nambie ni nani ambaye hafanyi kazi? Nani? Yale mahindi yanayonyauka kule Shamba yamejipanda Yale??? Hii kodi mnayosema imeongezeka imetoka wapi kama watu hawafanyi kazi? Tuache dharau Aisee
Wenye lugha yao usema no gain without pain
 
Watanzania tuwavivu, that's true. Wala huhitaji mjadala juu ya hili.
 
usiwasahau na wale wanaosema
................vitu vingine muwe mnauliza.
yaani kuna makabila wanajiona wako bright, perfect na wajanja kuliko makabila mengine.
Andika na mifano basi wa hayo makabila kiongozi
 
Your talking nonsense bro
Weye ndio unaongea visivyositahiri, mshahara na marupurupu unayolipwa na gharama zote unazotumia, chanzo chake ni kwa hao unaowaita wavivu! Wavivu wanaweza kulipa kodi kwa kila kitu wanachonunua na huduma zote wanazotumia na bado wakawa wapole tu! hata Mungu anawaoneni! Kwani hata farao alikuwa kiburi lakini siku moja aliangamia yeye na wapanda farasi wake!
 
Zoeeni tu si mnataka utamu wa maisha lazima upitie shida... Fighting for survivor
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…