Wameangalia uhitaji wa soko au wameingia tu sababu wenzao wameanzisha hiyo huduma?
Sijaona mtu atakae weza watoa Tigo na Voda na Airtel kwenye hili soko la pesa
Ukizingatia kuwa TTCL hata line zake tu kuonaekana ni nadra sana
KWanini wasingekuja na kitu kingine ambacho kingerahisisha sana upatikanaji wa huduma ya pesa kwa gharama nafuu zaidi ili tuwakwepe hawa ambao ukitoa milioni unakatwa 8000
Aliye washauri kuwa ukiwa kampuni ya simu lazima uwe na money transfer service kawapoteza, wamechelewa sana...
Wao wangeanzisha huduma nyingine ambayo ni bora kuliko hii ya sasa ya ssid,