TTCL washusha bei ya Internet

TTCL washusha bei ya Internet

Basi wamechelewa sana na hata walivyopunguza bado viwango vyao viko juu tu. Kwa mfano mimi nanunua 5gb ya vodacom tshs 20000 kwa mwezi mzima, na bado tu naweza kupata internet hata nikiwa vijijini tena kwa speed nzuri tu. Ni dhahiri bado wako juu, labda tu speed safi ila pia coverage yao ni ndogo sana. Tuwaombe waendelee kubadilika.
 
Hawa bado hawako serious yaani gb 1_6000 tena kwa cku wakati airtel 6000 g 3 tena kwa wiki na dk 275 kupiga mitano yote,cwapigii upatu ilathapa wameniweza
 
pamoja na kupunguza lakini bado viwango viko juu sana, hawawezi kushindana na packages kama za airtel tosheka nk !!!! Likiwa shirika la umma na ukizingatia kuwa wanamiliki mkongo wa taifa wa mawasiliano viwango vyao vilipaswa kuwa chini kuliko makampuni mengine!!!!
 
Airtel yatosha Bado iko Juuu sana. Kwani waweza kupAta 12GB kwa Tsh23,980 tu kwa Mwezi. Yaaani 3GB kwa week kwa Tsh5995 tu.

Na speed iko Makini. Ila kwa speed ya uhakika VODA Ndio wako JUU ki ukweli. Japo bundle zao nao zimekaa kiunyonyaji.

Kwa hiyo Airtel kwa Sasa ndio wenye Unafuu. Achilia mbali 3GB wanazo kupa kwa week, unapata pia zaidi ya Meseji 4000 na dakika 250 kupiga mitandao yote.

Wako Makini Airtel kwa sasa.

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
ttcl hawafai jamani wasitudanganye,hawana hela ya kutangaza hadi wanakuja humu!!MAKUBWA
 
Bundle hizo kwa matumizi ya kiofisi na kibiashara zinalipa ila kwa kusurf tarifa ndogondogo na kuchit chat bei ni kubwa bado
 
1GB kwa wiki sasa ni 6,000 badala ya 8,000.
1GB kwa mwezi sasa ni 10,000 badala ya 40,000/=
2GB kwa mwezi sasa ni 15,000 badala ya 60,000/=
4GB kwa mwezi sasa ni 25,000 badala ya 90,000/=
Pamoja na majibu mazuri ya mheshimiwa waziri, lakini kiukweli bado bei zao zipo juu sana.
mfano ni airtel bundle kwa Tshs 6000/- tu dakika 275 kuongea kokote SMS za kumwaga na 3GB Internet kwa siku Saba.
 
Mambo ya Internet kwa kweli yanategemea na mahali mtu alipo binafsi napokuwa kwenye miji mikubwa huwa natumia Airtel bila kujali gharama kwa kuwa speed ipo vizuri ila kwa bush huwa sina option zaidi ya TTCL kwani mitandao mingine hawajafunga mitambo yao kwa ajili ya internet zaidi ya kuishia kuunga kwenye GPRS tu ambayo unafungua email masaa 3
 
1GB kwa wiki sasa ni 6,000 badala ya 8,000.
1GB kwa mwezi sasa ni 10,000 badala ya 40,000/=
2GB kwa mwezi sasa ni 15,000 badala ya 60,000/=
4GB kwa mwezi sasa ni 25,000 badala ya 90,000/=
Zantel 5GB kwa 20,000/= Mwezi mzima!
 
speed uwa inazingua esp ktk kudownload ,nyimbo ya Mb 3 unaweza tumia hata dk 4 kuishusha,sijui kwa nyie mlio ktk miji mikubwa
 
TTCL waboreshe speed na Wapunguze bei za BROADBAND, waachane na hizo mobile internet!
 
Mimi bhabha nimehamia zantel kwa kale kabando ka kimaskini 1500/= MB 150 kwa mwezi baada ya Airtel kuondoa MB 400 2500/= kwa mwezi
 
Mimi bhabha nimehamia zantel kwa kale kabando ka kimaskini 1500/= MB 150 kwa mwezi baada ya Airtel kuondoa MB 400 2500/= kwa mwezi

ndugu mbona unalipia gharama sana kwanini usiwe unajiunga na kifurushi cha 500 kwa siku unadownload bila kikomo 24 hrs
 
Sina uhakika sana, lakini ningetegemea TTCL wawe cheap kuliko wengine lakini mbona they are more expensive than most?

Hiyo ya 4GB mi huwa natumia ya Vodacom ambayo nalipia 20,000 tu kwa mwezi na speed ni balaa kwa mimi ninayependa series kila episode mpya naidownload kwa dakika moja tu.

Bahati mbaya sana TTCL huwa wananidisapoint na ka mtandao kao tunakotumia ofisini ka hovyo kweli
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom