Ta Kamugisha
JF-Expert Member
- May 17, 2011
- 3,547
- 2,194
Kiukweli nimekubali kuwa mzalendo na kurudi nyumbani ila sasa milango yenu bado umefungwa, kwa nini hamtaki kutufungulia Milango wakati Mmetuita wenyewe?
1. Nilirudi nyumbani pale arusha mjini na mambo yalikuwa poa sana tena nikapewa chakula kitamu cha 4G na mboga za kutosha yaani bundle za maana, kwakuwa natumia line ya chuo nikasema isiwe tabu ngoja nikale na masela wangu.
2. Nikatoka mjini kwenda tu USA river sikuamini macho yangu, nyumba ya Tengeru imefungwa, nyumba ya USA ndio hata kuruka ukuta huwezi, nikaona isiwe tabu, nikaja kwa Mromboo, nako hivyo hivyo, Unga limited nako hivyo hivyo, njiro nako hivyo hivyo dah nikachoka....
3. Kazi yangu ikaisha nikapanda bus, njia nzima toka Arusha mpaka Mwanza hakuna hata nyumba ya kuchimba dawa zote zimefungwa, labda mpaka ukifika stand kuu za mikoa, toka Mwanza kuja Mkoani kwangu ndio hata Nyumba ya kupata chakula cha mchana aipo kabisaaa....
4. Nimerudi wilayani kwangu uku Mkoa mmoja karibia na Burundi, hata kipeperushi cha Rudi nyumbani kumenoga sikioni, zaidi zaidi najifariji na tangazo la kwenye Azam Tv tu.
5. Hivi kwa style hii TTCL mtatushawishi turudi nyumbani, kama nyote mmeamua kuishi mjini tu, nyumba za pembeni mwa mji mmezifunga, au mnategemea wote tuhamie mjini kwenye nyumba moja, tutatosha kweli.
6. Hapa nipo Wilayani na Line yangu kwenye wallet, hata sijui nitarudi lini mjini ili nikafaidi TTCL, kiukweli ampo makini au mna kasi ya konokono, sidhani kama mna wilaya hata moja ya mikoani ambayo mmefika.
7. Mnashindwa na Halotel kampuni ya juzi? Wapo mpaka uku ndani kabisa kijijini kwetu tena tunapata H+, hacheni utani jipangeni
8. Nyumba yenu ya hapa wilayani imefungwa, mimi nipo nje hapa nasubiria mnifungulie, kwa kifupi siwezi kuwaangusha, nimeamua kurudi nyumbani ila mlango bado ina kufuli la chuma SOLEX
9. Tena hapa kwetu kuna mashirika mengi ya wakimbizi, mnaweza hata kujenga nyumba nyingine ikajaa wateja tena wateja wanaolipa kwa fedha za kigeni,
10. Fanyeni haraka mimi nipo hapa mlangoni la sivyo nitalala nje ya nyumba mpaka mtakapokuja kunifungulia, mmeniita wenyewe Nirudi nyumbani, kwanini hamfungui milango hasa nyumba zenu za wilayani? Tupeni taarifa ni Nyumba zipi zipo wazi za wilayani ili tusije lala nje tukienda uko.
RUDI NYUMBANI KUMENOGA
1. Nilirudi nyumbani pale arusha mjini na mambo yalikuwa poa sana tena nikapewa chakula kitamu cha 4G na mboga za kutosha yaani bundle za maana, kwakuwa natumia line ya chuo nikasema isiwe tabu ngoja nikale na masela wangu.
2. Nikatoka mjini kwenda tu USA river sikuamini macho yangu, nyumba ya Tengeru imefungwa, nyumba ya USA ndio hata kuruka ukuta huwezi, nikaona isiwe tabu, nikaja kwa Mromboo, nako hivyo hivyo, Unga limited nako hivyo hivyo, njiro nako hivyo hivyo dah nikachoka....
3. Kazi yangu ikaisha nikapanda bus, njia nzima toka Arusha mpaka Mwanza hakuna hata nyumba ya kuchimba dawa zote zimefungwa, labda mpaka ukifika stand kuu za mikoa, toka Mwanza kuja Mkoani kwangu ndio hata Nyumba ya kupata chakula cha mchana aipo kabisaaa....
4. Nimerudi wilayani kwangu uku Mkoa mmoja karibia na Burundi, hata kipeperushi cha Rudi nyumbani kumenoga sikioni, zaidi zaidi najifariji na tangazo la kwenye Azam Tv tu.
5. Hivi kwa style hii TTCL mtatushawishi turudi nyumbani, kama nyote mmeamua kuishi mjini tu, nyumba za pembeni mwa mji mmezifunga, au mnategemea wote tuhamie mjini kwenye nyumba moja, tutatosha kweli.
6. Hapa nipo Wilayani na Line yangu kwenye wallet, hata sijui nitarudi lini mjini ili nikafaidi TTCL, kiukweli ampo makini au mna kasi ya konokono, sidhani kama mna wilaya hata moja ya mikoani ambayo mmefika.
7. Mnashindwa na Halotel kampuni ya juzi? Wapo mpaka uku ndani kabisa kijijini kwetu tena tunapata H+, hacheni utani jipangeni
8. Nyumba yenu ya hapa wilayani imefungwa, mimi nipo nje hapa nasubiria mnifungulie, kwa kifupi siwezi kuwaangusha, nimeamua kurudi nyumbani ila mlango bado ina kufuli la chuma SOLEX
9. Tena hapa kwetu kuna mashirika mengi ya wakimbizi, mnaweza hata kujenga nyumba nyingine ikajaa wateja tena wateja wanaolipa kwa fedha za kigeni,
10. Fanyeni haraka mimi nipo hapa mlangoni la sivyo nitalala nje ya nyumba mpaka mtakapokuja kunifungulia, mmeniita wenyewe Nirudi nyumbani, kwanini hamfungui milango hasa nyumba zenu za wilayani? Tupeni taarifa ni Nyumba zipi zipo wazi za wilayani ili tusije lala nje tukienda uko.
RUDI NYUMBANI KUMENOGA
