Nyakijooga
JF-Expert Member
- Dec 9, 2018
- 427
- 666
Kwa kweli huduma ya TTCL Fiber imekuwa changamoto kubwa katika maeneo mbalimbali Dar es Salaam. Wananchi tunafuata taratibu zote za kuomba huduma, tunajaza fomu na kusubiri, lakini kuna Watu zaidi ya miezi sita hawajafungiwa wala kupewa maelezo yanayoeleweka.
Mimi binafsi nimekamilisha taratibu zote, lakini mwaka unaelekea kuisha bado wako kimya. Kama inavyosomeka hapo pichani (uliomba huduma leo tunakufungia leo) hilo halina ukweli halisi, sijui labda kwa watu maalumu.
Wengine wanalipia huduma kila mwezi, lakini internet inaweza kukatika zaidi ya wiki nzima bila suluhu. Kila wakipiga simu kwa customer care, majibu yanayotolewa hayaeleweki na hayasaidii kabisa. Mara wanasema kuna changamoto za vifaa sasa mtu anauliza, mnaingiaje sokoni bila kujipanga vizuri kimfumo na kimiundombinu?
TTCL ni shirika la umma linalotegemewa na wananchi, lakini huduma ya customer care ni dhaifu mno, hasa kwenye kitengo cha Fiber. Tunahitaji uwazi, uwajibikaji, na huduma bora zinazolingana na gharama tunazolipa. Tafadhali boresheni huduma zenu kwa wateja.
Kama mnaelemewa na mahitaji ya Huduma ya TTCL Fiber, basi karibisheni wawekezaji kutoka sekta binafsi ili kuongeza ufanisi na kufanikisha utatuzi wa changamoto zilizopo pamoja na kufikia soko kubwa.
Mwisho, nitoe wito kwa TTCL kujitafakari juu ya utendaji wao katika huduma hii. Ni muhimu wafanye ufuatiliaji wa karibu ili kubaini changamoto zinazowakumba wateja wao na kutafuta namna rafiki na shirikishi ya kuzitatua.
Vilevile, Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ifuatilie kwa ukaribu changamoto hii, kwa sababu wananchi wengi tunakumbana na usumbufu badala ya kufurahia huduma.
Pia soma ~ Mnaotumia TTCL fiber mlifanyaje kuunganishiwa?
Malalamiko ya Wananchi wengine kwenye page ya Instagram ya TTCL kuhusu huduma ya Fiber:
Ufafanuzi wa TTCL upo hapa ~ TTCL: Kufungiwa Huduma za Fiber ni bure, wanaodaiwa kuchukua rushwa hatua zitachukuliwa
Wengine wanalipia huduma kila mwezi, lakini internet inaweza kukatika zaidi ya wiki nzima bila suluhu. Kila wakipiga simu kwa customer care, majibu yanayotolewa hayaeleweki na hayasaidii kabisa. Mara wanasema kuna changamoto za vifaa sasa mtu anauliza, mnaingiaje sokoni bila kujipanga vizuri kimfumo na kimiundombinu?
TTCL ni shirika la umma linalotegemewa na wananchi, lakini huduma ya customer care ni dhaifu mno, hasa kwenye kitengo cha Fiber. Tunahitaji uwazi, uwajibikaji, na huduma bora zinazolingana na gharama tunazolipa. Tafadhali boresheni huduma zenu kwa wateja.
Kama mnaelemewa na mahitaji ya Huduma ya TTCL Fiber, basi karibisheni wawekezaji kutoka sekta binafsi ili kuongeza ufanisi na kufanikisha utatuzi wa changamoto zilizopo pamoja na kufikia soko kubwa.
Mwisho, nitoe wito kwa TTCL kujitafakari juu ya utendaji wao katika huduma hii. Ni muhimu wafanye ufuatiliaji wa karibu ili kubaini changamoto zinazowakumba wateja wao na kutafuta namna rafiki na shirikishi ya kuzitatua.
Vilevile, Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ifuatilie kwa ukaribu changamoto hii, kwa sababu wananchi wengi tunakumbana na usumbufu badala ya kufurahia huduma.
Pia soma ~ Mnaotumia TTCL fiber mlifanyaje kuunganishiwa?
Malalamiko ya Wananchi wengine kwenye page ya Instagram ya TTCL kuhusu huduma ya Fiber:
Ufafanuzi wa TTCL upo hapa ~ TTCL: Kufungiwa Huduma za Fiber ni bure, wanaodaiwa kuchukua rushwa hatua zitachukuliwa