Jaji Mfawidhi
JF-Expert Member
- Feb 20, 2016
- 14,047
- 20,411
Hawa TTB [Tanzania Tourist Board] walikana kumtuma huyu Mwijaku nchini Ufaransa na kutuandikia barua ndefu ya kanusho huku Mwijaku naye akifuta post yake aliyojirekodi siku akiondoka na kuwataja sponsors wake Hawa anayemiliki HAWA TOURS.
Walichosahau ni kuwa Teknolojia ni kitu kipo mbele kuliko akili zao na haisahau wala haidanganyiki.
Wakanushe na hii basi! Cha kushangaza hakuna atakayechukuliwa hatua kwa uongo ule akitumia nembo ya serikali na kula mshahara wa walipa kodi wa TZ ili awadanganye waTZ.
Nchi imekuwa ya kushangaza na mambo ya ajabu ajabu. Nchi ya chawa. Rais alienda India na Chawa, leo wapo Manyara kumpokea tena Rais kwa gharama za serikali yaani kodi za Mama Lishe,Bodaboda,Machinga.
Siku mbili zilizopita Rais Samia Suluhu akipokea ripoti ya Wizara Mambo ya nje, amekiri matumizi mabaya ya Wizara hiyo na utalii kujitangaza nje, huku akisema tulitumia mabilioni kujitngaza CNN na hakuna mtalii aliyeongezeka kutokea MAREKANI.