kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 17,025
- 16,711
Watanzania wenzangu tuwaondoe vijana wetu kandokando ya barabara kuuza machungwa 20 mezani badala yake twende tukawagawie ardhi iliyoboreshwa wazalishe kabla ardhi yao haijaisha kabisa.
Ningetamani hizo bil 200 zooote zingewekwa kama chambo kwa vijana kwenye kilimo kuwavuta vijana waende kwenye kilimo, ufugaji na uvuvi.
Tunawadanganya sana vijana wetu kama tukiwaacha kandokando ya barabara, na kuendesha bodaboda huku tukijua kuwa tunawadanganya ili kesho ifike.
Lakini siku itafika ambapo kando ya barabara pia kutajaa na kuanza kugombana wenyewe kwa wenyewe kuwania nafasi za mbele barabarani au kugombana na serikali pale watakapogundua kuwa mliwadanganya kuwa hata kuuza mafenesi 2 ni kazi pia.
Barabara zinaharibika na njia za majitaka zinazibwa na takataka wanazozalisha vijana wetu. Pelekeni fedha nyingi kwenye ardhi kabla ardhi hii haijamezwa na matajiri wa ndani na nje ya Tanzania.
Ningetamani hizo bil 200 zooote zingewekwa kama chambo kwa vijana kwenye kilimo kuwavuta vijana waende kwenye kilimo, ufugaji na uvuvi.
Tunawadanganya sana vijana wetu kama tukiwaacha kandokando ya barabara, na kuendesha bodaboda huku tukijua kuwa tunawadanganya ili kesho ifike.
Lakini siku itafika ambapo kando ya barabara pia kutajaa na kuanza kugombana wenyewe kwa wenyewe kuwania nafasi za mbele barabarani au kugombana na serikali pale watakapogundua kuwa mliwadanganya kuwa hata kuuza mafenesi 2 ni kazi pia.
Barabara zinaharibika na njia za majitaka zinazibwa na takataka wanazozalisha vijana wetu. Pelekeni fedha nyingi kwenye ardhi kabla ardhi hii haijamezwa na matajiri wa ndani na nje ya Tanzania.