Trump ana dharau huyu mwamba

Trump ana dharau huyu mwamba

Anawaambia Congo na Rwanda ole wenu atakaekiuka mkataba huu. Hii ni baada ya kuwasainisha mkataba. Trump ana dharau mpaka anakera.
Si ni afadhali alivyotoa maelekezo hayo ili amani ipatikane?
 
Ukinunua kitu china unatumia sarafu gani?
Sasa hayo ndiyo maagizo? Mbona China inafanya cross border transaction na mataifa mengine kwa kutumia yuan?

Na kwa sasa kwenye cross border transactions na China, mataifa mengi yanatumia Yuan kuliko USD

Labda nikupe mfano sahihi na wenye mashiko kwa nini China haifuati maagizo.

Iran iko kwenye vikwazo vya kimataifa vya kibiashara kwa miaka kadhaa sasa

Kabla ya vikwazo mataifa mengi yalikuwa yakinunua mafuta Iran ila baada ya Iran kuwekewa vikwazo mataifa yote yaliacha kununua

Unajua ni taifa gani pekee ambalo linaendelea kununua mafuta ya Iran tangu vikwazo viwekwe?

China ndiyo taifa pekee linalonunua 90% ya mafuta ya Iran licha ya vikwazo.

Na hadi China imejenga reli kutoka China hadi Iran kwa ajili ya kusafirisha mafuta

China haina habari na mikwara ya Trump na nchi za Magharibi. Kuna mifano mingi ukitaka nitakupa.

Hakuna taifa la kuiendesha China au Russia dunia hii


20250701_210734.jpg


Kida ze great
 
Back
Top Bottom