Trump aishambulia Afrika, Haiti na El Salvador adai ni 'nchi chafu'

Nalendwa

JF-Expert Member
Aug 9, 2016
7,467
13,024
180106-trump-republican-leadership-ew-537p_5600f3ea8e7a0b3f4d99537a51311732.nbcnews-ux-2880-1000.jpg


Kwa nini tunawaruhusu watu hawa kutoka mataifa 'machafu''?.

Rais Trump aliwaambia wabunge siku ya Alhamisi kulingana na gazeti la The Washington Post.

Tamko hilo lilidaiwa kuwalenga watu kutoka Afrika, Haiti na El Salvador.

Ikulu ya Whitehouse haikukana tamko hilo ambalo lilithibitishwa na vyombo vyengine vya habari.

''Wanasiasa fulani wa Washington hupendelea kupigania mataifa ya kigeni, lakini rais Trump atawapigania raia wa M arekani pekee,taarifa iliotoka katika msemaji wa Ikulu Raj Sha ilisema.

Iliendelea: Kama mataifa mengine ambayo yana wahamiaji wanaofaa kuwa nchini humo, rais Trump anapigania suluhu ya kudumu inazofanya taifa hilo kuwa thabiti kwa kuwakaribisha wale ambao wana mchango katika jamii ,hukuza uchumi wetu na kuingiliana na raia wa taifa letu.

Kamwe hatakubali mkakati wa muda mfupi ulio hafifu na hatari ambao unahatarisha maisha ya raia wa Marekani, mbali na kutowaruhusu wahamiaji wanaotaka maisha mazuri Marekani ijapokuwa kupitia njia halali.

Matamshi hayo ya rais Trump yanajiri huku wabunge kutika vyama vyote wakimtembelea kupendekeza mpango wa wahamaiji usiopendelea upande wowote.

Seneta wa Democrat Richard Durbin alikuwa akizungumza kuhusu vibali vya muda wa kuishi vinavyotolewa kwa raia wanaotoka katika mataifa yaliokumbwa na majanga, vita ama milipuko ya magonjwa, vilisema vyombi vya habari.

Kulingana gazeti la Washington Post , bwana Trump aliwaambia wabunge kwamba Marekani badala yake inachukua wahamiaji kutoka Norway, ambayo waziri wake mkuu alimtembelea rais Trump siku ya Jumatano.

Seneta Lindsey Graham, ambaye ni mwanachama wa chama cha Republian kutoka Carolina Kusini pia alikuwa katika mkutano huo lakini hakuweza kuzungumzia kuhusu matusi hayo yaliotolewa na rais Trum.

Gazeti la The New York Times liliripoti miaka mitatu iliopita kwamba bwana Trump alisema kuwa raia wa Haiti wote wana ''ukimwi'' wakati wa mkutano wa mwezi Juni kuhusu wahamiaji.

Na kufuatia matamshi hayo rais Trump hakusazwa katika mitandao ya kijamii.

Elijah Cummings, mbunge wa Democrat katika eneo la Maryland alichapisha ujumbe katika mtandao wa twitter akisema: Nayashutumu matamshi hayo yasiosameheka na yanayoshusha hadhi ya afisi ya rais.

Mbunge mwengine mweusi kutoka chama cha Democrat. Cedric Richmond, alisema matamshi ya bwana Trump ni dhihirisho tosha kwamba sera yake ya kuliimarisha taifa la Marekani ni sawa na kulifanya taifa la Marekani kuwa la watu weupe pekee.

Mia Love, raia wa chama cha Republican katika eneo la Utah ambaye pia ni mbunge wa pekee mwenye mizizi ya Haiti nchini Marekani amemtaka rais Trump kuomba msamaha kwa maneno hayo yalio na chuki na yenye kugawanya watu.

Muungano unaopigania haki za watu weusi NAACP ulimshutumu rais Trump kwa kuzidi kuegemea katika ubaguzi wa rangi.

Lakini Ikulu ya Whitehouse imepuuzilia mbalia shutuma hizo zinazomkabili rais.

Afisa mmoja wa Trump alinukuliwa na chombo cha habari cha CNN akisema: Ijapokuwa hili litawakasirisha watu wa Washington, wafanyikazi wanadhani kwamba matamshi hayo yanatokana na mizizi yake, sawa na matamshi yake dhidi ya wachezaji wa NFL waliopiga goti wakati wa kuimbwa kwa wimbo wa taifa.

Msemaji wa ubalozi wa El Salvador mjini Washington alikataa kuzungumzia kuhusu matamshi hayo.




======================================================



President Trump grew frustrated with lawmakers Thursday in the Oval Office when they floated restoring protections for immigrants from Haiti, El Salvador and African countries as part of a bipartisan immigration deal, according to two people briefed on the meeting.

“Why are we having all these people from shithole countries come here?” Trump said, according to these people, referring to African countries and Haiti.

He then suggested that the United States should instead bring more people from countries like Norway, whose prime minister he met yesterday.

The comments left lawmakers taken aback, according to people familiar with their reactions. Sens. Lindsey O. Graham (R-S.C.) and Richard J. Durbin (D-Ill.) proposed cutting the visa lottery program by 50 percent and then prioritizing countries already in the system, a White House official said..

Trump attacks protections for immigrants from ‘shithole’ countries
 
View attachment 673602

President Trump grew frustrated with lawmakers Thursday in the Oval Office when they floated restoring protections for immigrants from Haiti, El Salvador and African countries as part of a bipartisan immigration deal, according to two people briefed on the meeting.

“Why are we having all these people from shithole countries come here?” Trump said, according to these people, referring to African countries andHaiti.

He then suggested that the United States should instead bring more people from countries like Norway, whose prime minister he met yesterday.

The comments left lawmakers taken aback, according to people familiar with their reactions. Sens. Lindsey O. Graham (R-S.C.) and Richard J. Durbin (D-Ill.) proposed cutting the visa lottery program by 50 percent and then prioritizing countries already in the system, a White House official said..
asante kwa habari maana namiliki blog ya kizungu
 
View attachment 673602


President Trump grew frustrated with lawmakers Thursday in the Oval Office when they floated restoring protections for immigrants from Haiti, El Salvador and African countries as part of a bipartisan immigration deal, according to two people briefed on the meeting.

“Why are we having all these people from shithole countries come here?” Trump said, according to these people, referring to African countries andHaiti.

He then suggested that the United States should instead bring more people from countries like Norway, whose prime minister he met yesterday.

The comments left lawmakers taken aback, according to people familiar with their reactions. Sens. Lindsey O. Graham (R-S.C.) and Richard J. Durbin (D-Ill.) proposed cutting the visa lottery program by 50 percent and then prioritizing countries already in the system, a White House official said..

Trump attacks protections for immigrants from ‘shithole’ countries


Please please, lets just call it what it is, mnaogopa hata kuandika Urrgh
 
Exodus!
African leadears should stand-up to this madness!

According to News outlets in America, one of them CNN, The White President has called our continent a "SHITHOLE"

I wonder who takes the shit in this hole? Anybody?
Kua mpole , ujinga wa kutawala bila kikomo, kuminya demokrasia na ukiukaji wa haki za binadamu ndio kunapelekea kuitwa a.r.s.e hole countries.
 
Back
Top Bottom