Trump aahirisha mkutano baada ya ukosoaji

Trump aahirisha mkutano baada ya ukosoaji

Influenza

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2018
Posts
1,565
Reaction score
4,009
Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza kuahirisha mkutano wake wa kwanza mkubwa wa kampeni baada ya kuandamwa na ukosoaji kwa kuandaa mkutano huo katika siku ya kukumbuka kukomeshwa kwa utumwa nchini Marekani

Trump amesema uamuzi wa kusogeza mbele mkutano huo umefikiwa baada ya mazungumzo na wafuasi wake kutoka jamii ya wamarekani weusi waliopendekeza kubadilishwa tarehe kwa lengo la kutoa heshima kwa Juni 19 inayotambulika kuwa siku ya maadhimisho ya kumalizika utumwa

Uamuzi wa Trump wa kuandaa mkutano hasa katika eneo la Tulsa mjini Oklahoma ulisababisha ghadhabu miongoni mwa wakosoaji wake waliosema ilikuwa ni tusi kwa kumbukumbu ya George Floyd , mmarekani mweusi aliyeuliwa wiki chache zilizopita kutokana na ukatili wa polisi

Makundi ya wamarekani weupe yaliwauwa mamia ya wamarekani weusi katika kitongoji cha Tulsa wakati wa vurugu za mwaka 1921 na mipango ya Trump kufanya mkutano kwenye eneo hilo imetafsiriwa kuwa tendo la kuenzi ukatili wa mabeberu wa kizungu.
 
Trump kiti kinatema cheche.. Ni muda siasa kuanza kutii utu na sio utu kutii siasa
 
Bado ana muda mrefu wa kujipanga kwa miezi iliyobaki kuelekea uchaguzi.
 
Ata afanyeje ameshajulikana kuwa ni mbaguzi mkubwa
Amembagua nani? Kafanya nini? Ama unajiandikia tu.

Hakuna rais wa Marekani aliewabeba na muwakomboa watu weusi zaidi ya Trump.

Sasa mtu unajiandikia tu mbaguzi, kabagua nini?

Eti hata afanyeje ashajulikana, kajulikana na nani?

Kabla hujaandika uharo uwe unajiongeza kidogo kuleta ushahidi basi wa uharo wako.
 
uliupigia sana kampeni ule mkutano saa hii naona umemgeuka

afanye arejee WH tunamngojea tumpongeze kwakishindo.....
Kusema wewe utapinga ndo kampeni? [emoji23][emoji23] Onyesha hizo kampeni nilizopiga usipoonyesha wewe ni muongo kama waongo wengine
 
Back
Top Bottom