Treni ya abiria yapata ajali Dodoma

Treni ya abiria yapata ajali Dodoma

Sekenke

Senior Member
Joined
Mar 3, 2008
Posts
132
Reaction score
30
Jumapili, 29 Machi 2009, Saa Mbili na Robo Asubuhi. TBC wametoa taarifa hii fupi kimaandishi kwenye luninga:

Treni ya abiria imegongana na treni ya mizigo katika eneo la Msagali na Gulwe wilaya ya Mpwapwa. Tayari waokoaji wameanza kupasua behewa moja la treni ya abiria ili kutoa watu waliomo ndani.
 
Lets hope hakuna maafa.But it sounds odd...no journey planning or it is because of poor communication
 
Jirani yangu katumiwa ujumbe wa simu toka kwa rafiki yake aliyeko Dodoma kuwa kuna uvumi watu 100 wamefariki ktk ajali hiyo. walioko karibu wajaribu kufuatili kutapa ukweli wa kina wa taarifa hii..
Nawasilisha
 
Inahuzunisha -- hasa vifo vya raia wasiokuwa na hatia. nauliza: Hizo treni ziligongana zikiwa zinarudi kinyumenyume? na hivyo madereva hawakuonana? Msishangae kwani miaka kadha iliyopita watu 300 walikufa kwa ajali ya treni ya abiria iliyokuwa inarudi kinyumenyume!
 
Ajali nyingi za Tanzania ni matokeo ya uzembe. Kinachosikitisha ni kuwa hakutakuwa na hatua zitakazochukuliwa kwa wahusika. Kilio kinabaki tu kwa wale wahanga waliokumbwa na ajali hizi.

Mungu na atunusuru.
 
Lets hope hakuna maafa.But it sounds odd...no journey planning or it is because of poor communication

Yani Tanzania inamatatizo sana, mpaka Treni zinagongana! mawasiliano hakuna kabisa kati ya Railway station moja na nyingine. Mh lakini kama waokoaji ndio wanakata behewa la treni ya abiria ili kuwatoa walioko ndani ya behewa hilo basi impact itakuwa ni kubwa sana na kuna uwezekano wa kuwa na Fatality.
 
Asilimia kubwa ya ajali zetu ni uzembe tu, kwa impact ya aina hiyo fatality ni lazima
we needs changes
 
Uzembe ambao pia umechangiwa na mwekezaji mbovu. Baada ya kupata mwekezaji mpya tulitumaini ajali hizi za treni za abiria zingetoweka -- kama vile wakati wa ukoloni -- kulikuwa hakuna, au nadra mno, kwani treni za abiria kuleta ajali na kuua kwani zilikuwa zinaangaliwa sana kiusalama.

Hakuna sababu kwa nini hicho kisifanyike hivi sasa. Siku hizi mambo ni bora twende -- treni za abiria zinaendeshwa kama vile ni za mizigo.

Waziri husika -- Shukuru Kawambwa, inapasa ajiuzulu. Ni kweli, hakuwa anaendesha treni hizo au kuwepo katika eneo la ajali, lakini ni bora sasa afungue njia kwa serikali ya JK kuwajibika -- kumsaidia swahiba wake kuleta heshima ktk utawala wake. Najua kuna watu watamtetea kwa hili! Hawa wanaendeleza tu hali ya kutokuwepo utamaduni wa uwajibikaji.

Ubinafsishaji wa TRC kwa mwekezaji huyu umekuwa unalalamikiwa sana, kutokana na huduma duni katika uendeshaji wa shirika hilo na kwamba kuna dalili nyingi ubinafsishaji ulikuwa ni wa kifisadi.

Hivyo ajali hii itaongeza kuwasha moto. Na bila shaka kuna watu humu ktk JF hivi sasa wanaanza kuchonga kalamu zao kuzidi kutetea ufisadi huo na hata ajali yenyewe, kwamba ni ajali tu, haihusiani kabisa na mwekezaji mpya.
 
Imegongana na tren ya mizigo kwenye mabehewa mawili ya nyuma mpaka sasa ni watu wawili comfirm kufa...majeruhi wapo...na kuna behewa jingine ndio wametuma mafundi kwenda kulikata kuona nini....kitajiri
 
kwa nini uzembe unagharimu maisha ya watu wasio na hatia?inatia sana hasira yaani treni kugongana?ina maana hakukuwa na mawasiliano?
Yaani inaudhi sana tena sana!
 
Inahuzunisha sana tena mno train zigongane?Hakuna mawasiliano?Zinaenda kwa kuviziana nyingine ipack au ndo hivyo mastetion master wanasikiliza mlio wa mataruma kuwa ipo jirani?Tutaendelea kuwakumbatia wazembe mpaka lini jamani?Amkeni jamani.
 
Wakuu atakaepata data za ziada atupe. Huu msiba wa wote. Haina haja kulaumiana kwa sasa.
 
Mods unganisha na ile ingine ambayo ipo tayari.
 
Kun utata hapo,nilikuwa nafuatilia Clouds FM wanasema inawezekana zaidi ya 5 wamekufa papo hapo.
 
Hatari nyingine tena.
Hivi suala la mawasiliano kwa nini linapuuzwa? Ni kwa nini treni mbili zigongane? Ama ndo kusema kuna njama imepangwa?

Asikufiche mtu maximum speed ni 50km/h kwa maeneo mazuri ambayo yako sehemu za Tabora tu. Sehemu nyingine max speed ni 30kph. Kwa kuangalia tu kanuni za mwendo na fatality za ajali utagundua kuwa mambo yanaenda kienyeji mno.

Kwa nini watanzania tunauana???
 
i58_1.JPG


i59_3.JPG


i60_41.JPG



Source: Mzee wa Sumo
 
..inasikitisha sana.

..huu ni uzembe wa hali ya juu.
 
Back
Top Bottom