Tabia za trafiki kukamata magari na kudai pesa katika siku za karibuni zimekithiri,tena Dar wamejazwa kila kona ni wengi,si ajabu wananchi nao wanaanza kuja juu,hiyo ni reaction!mengi yatafuatia as long as kuna action,reaction itaendelea kuwepo.Tujiulize,ni kwa nini vyombo vya sheria vikose ushawishi katika kuwaongoza wananchi kusimamia sheria?Hivi raia wameamua kuwa "toto tundu" ghafla tu,bila sababu?
Msichokiona watawala ni kuwa wananchi wakichoshwa na sehemu ya mfumo,wanauona mfumo wote mbaya!
Jk and co,hili jeshi lenu la Polisi litawaponza sana msipokuwa makini.Nawaangalieni tu,haya!