Traffic Anapochukua Leseni Yako, Nini cha Kufanya?!

Traffic Anapochukua Leseni Yako, Nini cha Kufanya?!

Goodluck Mshana

JF-Expert Member
Joined
Aug 7, 2011
Posts
1,272
Reaction score
1,128
Msaada unahitajika kidogo hapa wana JF

Leo nimekamatwa na askari wa barabarani/trafic nikiwa natoka kwenye pilika zangu za maisha. Alinikamata kwa madai nilikuwa nipo speed/overdriving. Niliposimama akaniuliza Leseni nikatoa kumpa! Nilimpa nikisubiri majibu yake. Chakushangaza akaniambia nenda maana una haraka, kesho uje kulipa fine ndipo uchukue Leseni Yako!

Sikutaka mabishanao na yeye maana naheshimu utawala wa sheria. Sikutaka kuvutana naye maana niliheshimu kazi na umri wake. Nilitumia uungwana halisi wa Mtanzania kuondoka baada ya kugomea leseni yangu. Hakuwa ameniandikia nonification/charge yoyote ile. Alitengeneza mazingira ya mimi kumpa RUSHWA lakini kwa hilo kwangu niligoma. Hivyo akaamua kwa mamlaka aliyojipa kuhodhi leseni yangu!

Hivyo nawaombeni wasomi wa taaluma mbalimbali hasa sheria kunisaidi kwenye hili. Je, nifanyaje!? Kabaki na leseni yangu na sijaandikiwa kosa lolote?!
 
Unamfaham jina? au umechukua namba ya kazi? Au amekwambia yupo kituo gani?
 
Ujanja ni kumfahamu tu, then mwachie hiyo leseni akae nayo. Baada ya siku 2-3 nenda kwa boss wake kwani leseni si mali ya polisi ni mali ya TRA
 
Nimepata maoni mazuri sana ndugu zangu. Asanteni mnoo. Huyo trafic yupo kituo cha Mbezi kwa Msuguli FIDA
 
Last edited by a moderator:
Siku nyingine Mkuu usimpe leseni yako! Dawa ni kama wadau walivyoshauri unatoa photocopy unabandika stamp duty na unaifanyia lamination kabisa unakuwa unatembea nayo, original inakuwa mbali kwenye wallet! Akidai original unaichomoa unamwonesha huku umefunga kioo anaisomea kwenye kioo! Akiamua kuondoka na photocopy wala huhangaiki kumfuata tena unafotokopisha nyingine!
 
Chukua kadi ya gari na lesseni toaa kopi za kutosha, akihitaji mpe kopi na si original.

Akileta za kuleta washa gari sepa. Hatakuwa na muda wa kukufuatilia
 
dawa yao ni kuwabamiza makofi, uzuri kama vijjn huwa wanajibanza kwenye vikona hivi tena hawana siraha, akikuletea za kuleta tia makofi ndo dawa ya kuzuia rushwa. hawa jamaa kwa rushwa wanaongoza
 
Hawa jamaa wameendekeza njaa sana ndiyo shida. Ogopa mtu anaye toka nyumbani hajapata chai, anaitegemea barabarani.
 
Ndio shidao yao kma mwanza ndio stail yao akisimamisha gari tu utasikia leseni na kadi ya gari ukishaampa tu ndio ujinga unaanzia hapo wanasumbua saana
 
Unampa leseni yako?anabaki nayo?!!!mbona tayari kafanya kosa!mropoti kwa trafiki Mkuu mpinga!naamini una namba yake ya kazi au ili mselfie ki aina?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom