TRA yatakiwa kudhibiti ubadilishaji fedha mpakani

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,880
6,367
ashantu.jpg


Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji ameitaka Mamlaka ya Mapato TRA mkoa wa Mbeya kuhakikisha inaandaa mpango maalum kwa ajili kudhibiti mapato yanayopotea kutokana na biashara ya ubadilishaji wa fedha kiholela katika mpaka wa Tunduma.

Dk. Kijaji ametoa kauli hiyo mkoani Mbeya mara baada ya kutembelea Mamlaka ya Mapato (TRA) mkoani humo na kutoa tathmini ya ziara yake aliyoifanya katika mpaka wa Tunduma na Zambia.

Amesema serikali imekuwa ikipoteza mapato mengi hasa kutokana na kuwepo kwa biashara hiyo kiholela pasipo serikali kupata mapato yake hivyo ameitaka mamlaka hiyo kuhakikisha inaweka mpango kabambe utakao iwezesha serikali kupata mapato yake kutokana na biashara hiyo.

Dk. Kijaji amesema serikali lazima ijiendeshe yenyewe kwa kuongeza ukusanyaji wa mapato sanjari na kuzuia mianya yote ya ukwepaji wa kodi pamoja na watu wote kuhakikisha wanalipa kodi.

Chanzo:
EATV
 
Labda alitaka kujionea jinsi Vizuizi vya barabarani haswa NTB- Non Tarrif Barriers zilivyo nyingi na zinavyodumaza Biashara kati ya Nchi yetu na Majirani
 
Hapo kuna kazi kubwa inafanyika ya kubadilisha hela na wanajulikana wafukuzwe tu wakiendelea wafungwe
 
Bora tu wangepewa semina elekezi maana nahisi wanafanya kazi kwa kukisia kisia kwamba watamfurahisha bosi ama la!
 
Bora tu wangepewa semina elekezi maana nahisi wanafanya kazi kwa kukisia kisia kwamba watamfurahisha bosi ama la!
 
Safi sana
Kwa stahili hii ya kiongozi kudandia malori hata matrafic lazima washituke hawajui IGP aweza kuwa lori gani.Utendaji mabarabarani lazima utabadilika kuwa mzuri.Maana waweza kuta utingo wa lori au aliyekaa juu ya lori la Mkaa NI Magufuli .Sasa kama mkaa umepigwa marufuku wewe ukaruhusu lori la mkaa lipite kesho njia nzima hamna kazi na kesi juu.Hongerea Mama kijazi kuonyesha njia.Hapa kazi tu

Kwa stahili hili wala rushwa wengi barabarani watadakwa kuanzia matrafiki,maafisa misitu, Tra,Mizani NK Hongera sana mama
 
Hapo kuna kazi kubwa inafanyika ya kubadilisha hela na wanajulikana wafukuzwe tu wakiendelea wafungwe
Hujui unachokiongea. ...unadhani hao ni sawa na wamachinga wa Barabarani.

Kwa taarifa yako kuwafungia hao sawa na kusema unaifunga Tunduma, Nenda TRA kaulize kodi inayokusanywa kwa mkoa wa Mbeya Tunduma inachangia asilimia ngapi. ?
 
Bora tu wangepewa semina elekezi maana nahisi wanafanya kazi kwa kukisia kisia kwamba watamfurahisha bosi ama la!
Vitu vingine wangekuwa wanafanya uchunguzi kwanza kabla ya kutoa maagizo.
 
Mimi naamini hao wote mnaowaona wanafanya maagizo ya makufuli,kwahyo huo ndo mpango mpya wa kuendesha serikali kama kampuni fulani hivi !natumai umenielewa.
 
Back
Top Bottom