TRA yashusha VAT kutoka 18% hadi 16% ya biashara ndogo

TRA yashusha VAT kutoka 18% hadi 16% ya biashara ndogo

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
79,084
Reaction score
84,978
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imeshusha kiwango cha Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwa biashara ndogo kutoka asilimia 18 hadi asilimia 16, ili kuhamasisha ukusanyaji wa mapato kupitia malipo ya kielektroniki badala ya miamala ya fedha taslimu.

Kamishna Mkuu wa TRA, Yusuf Mwenda, alisema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa kampeni ya elimu kwa walipakodi, akizungumza na wafanyabiashara, wadau na wahariri wa vyombo vya habari.

Amesema uamuzi huo ni muhimu kwa kuwa utapunguza gharama za ununuzi wa bidhaa kwa wamiliki wa biashara ndogo kwa asilimia mbili, jambo linalotoa nafuu kubwa.

Chanzo: The Guardian

My Take
SSH ndio Rais anayejali watu waliojiajiri na kuhimiza kujiajiri na kulipa Kodi Kwa hiari.

Samia anatakiwa kulindwa Kwa wivu mkubwa.

View: https://www.instagram.com/p/DNIdir-MxA7/?igsh=MW5tcDhxZDdsM2VleA==
 
giphy.gif
 
hizi ndo nyakati za ng`ombe kunenepea mnadani...
akishakunya, uzito unarudi pale pale ...
Haujaanza Leo alishaunda Hadi jopo la kutathmini Kodi na kuleta mapendekezo Kwa Serikali na haya ndio matunda yake.

Samia ametumia miaka 4 tuu Kuzalisha Mapato ya Trilioni 120 hakuna mwingine amewahi.
 
..sheria za kodi zinatungwa na serikali na kuanza kutumika bila kupita bungeni?
Hilo la VAT kuwa na viwango viwili tofauti limo kwenye hotuba ya bajeti 2025/26?
Nadhani ni ulaghai tu ili TRA kupata wanachotaka lkn hakuna uhalisia.
 
..sheria za kodi zinatungwa na serikali na kuanza kutumika bila kupita bungeni?
Hilo la VAT kuwa na viwango viwili tofauti limo kwenye hotuba ya bajeti 2025/26?
Nadhani ni ulaghai tu ili TRA kupata wanachotaka lkn hakuna uhalisia.
Uwe unasikiliza Bunge la Bajeti
 
Back
Top Bottom