Kuna nini hapo kwenye kitengo cha makadirio mkuu, funguka zaidiJamani wafanyakazi wa TRA najua mnafanya kazi kubwa sana. Ila Kuna sehemu haijakaa sawa, Mamlaka husika embu fuatilieni kimya kimya, Hasa kwenye kitengo Cha Makadirio. Ahsante.
Mimi nina mauzo ya million 64 kwa mwaka wananambia kodi inabidi ipande kutoka million moja na elf 60 kufikia million mbili na laki mbili, wanasema mauzo ni makubwaHii nchi ukifanya biashara kiungwana aka 'kilokole" hutoboi leo wala kesho.
Asante kwa Taarifa ambayo tumeichukulia kwa uzito mkubwa sana na tunaifanyia kazi. Tunapenda kuwaomba wananchi ushirikiano hasa wanapoona taratibu hazipo sawa wasisite kutoa taarifa WhatsApp: +255 744 233333,namba za simu bure kituo chetu cha huduma 0800 750075 au 0800 780078,ukiukwaji wa maadili kwa kupiga 255 689 122 515 au ujumbe mfupi (sms) +255 689 122 516. Mwisho mtoa taarifa hii tunaomba ushirikiano wako kwa kututumia namba yako kwenye WhatsApp: +255 744 233333 ili tuweze kukusaidia na upate makadirio kulingana na biashara yako.Jamani wafanyakazi wa TRA najua mnafanya kazi kubwa sana. Ila Kuna sehemu haijakaa sawa, Mamlaka husika embu fuatilieni kimya kimya, Hasa kwenye kitengo Cha Makadirio. Ahsante.
Ukweli mtupu, mtu unatoa risiti kihalali ila ikija kwenye kodi utajuta kwa nn ulikua muaminifu kwenye utoaji risitiMimi nina mauzo ya million 64 kwa mwaka wananambia kodi inabidi ipande kutoka million moja na elf 60 kufikia million mbili na laki mbili, wanasema mauzo ni makubwa
Ukiangalia hiyo Million 64 kwa mwaka ni sawa na wastani wa mauzo 176,000 kwa siku
Nilichojifunza watu wanaokwepa kutoa risiti sio wajinga