TRA sasa mmeanza kuingiza siasa katika taaluma yenu, yani mkusanye kodi ya pango kupitia mpangaji badala ya mwenye nyumba?

Wazolee

JF-Expert Member
Sep 1, 2018
2,702
3,091
Hii nchi inavituko sana kwa hiyo TRA mmeshindwa kupita mitaani kuzisajili nyumba zote zinazofanya biashara na kuamuru wamiliki wa nyumba hizo walipe kodi ya pango badala yake mnataka mkusanye kodi hizo kupitia wapangaji, hichi ni kichekesho!

Eti kifungu cha sheria (82)2(a) kinamtaka mpangaji apeleke kodi ya pango TRA

Hivi kweli wasomi wa Tanzania mnakutana na kutunga sheria mbovu kama hii mbona nyinyi wasomi wa hii nchi mnatutia aibu?!

Vipi huyu mpangaji asipolipa hiyo kodi ya pango, mtampa adhabu gani kwa kutolipa kodi ya pango ya jengo ambalo yeye si mmiliki bali mmiliki wake yupo amekunja 4 sebuleni anaangalia TV?

Ubovu wa sheria zenu mmefanya wafanya biashara wote hapa nchini walipe hiyo kodi ya pango kutoka mifukoni mwao, na sio kama hamjui mnajua sana kuwa hizo kodi mnazowakamua wafanya biashara na wala sio wenye nyumba.

Sasa hawa wafanya biashara hawana jinsi ndio maana mkiwalazimisha walipe hiyo kodi ya pango wanalipa ili kukubali yaishe.

Sasa kwa umbumbu wenu mnadhani na kwa wapangaji wa vyumba vya kulala itakuwa hivyo hivyo, haya ngoja tuone?!

In nature mpangaji huwa anamuomba mwenye nyumba ampangishe nyumba yake, na mwenye nyumba ni uwamuzi wake amkubalie au amkatalie. Kwa hiyo akimkubalia apewe pesa 90% na risiti ya TRA, yani huo mkataba ndio utakuwa umeishia hapo hapo na chumba/Nyumba hatopata, huo ndio ukweli.

Sent from my TECNO Camon CX using JamiiForums mobile app
 
Fremu za biashara wafanyabiashara wanalipia sana hii kitu, sijui wanaita gani vilee nimesahau. Yani kabla TRA hawajakupa leseni ya biashara, lazima upeleke mkataba wa fremu yako, kisha unalazimika kulipia 10% ya gharama ulolipia hilo pango.

Sasa wanachofanya mwenye pango na anayepangishwa, kwenye mkataba wanaandika pesa kiduchu kuliko ile aliyolipa. Kama pango ni laki 1, basi mkataba unaandikwa hata elfu 30 tuu.

Nachojiuliza huku kwenye wapangaji sijui watawabana vipi sababu hawana cha kufuata TRA, na hakuna mjinga wa kupeleka hii pesa. Labda watoke kwenye viyoyozi waje field.
 
Fremu za biashara wafanyabiashara wanalipia sana hii kitu, sijui wanaita gani vilee nimesahau. Yani kabla TRA hawajakupa leseni ya biashar...
Hela anayetaka kukupa mpangaji

Yeye anaikata kabisa hiyo kodi ya zuio

Analipa anakuletea risiti

Wenye apartments, waliyowekeza kwenye maeneo ya watu wanalipa sana hii miaka nenda rudi.

Hii siyo kodi ngeni sema wabongo si wafuatiliaji

Ova
 
Fremu za biashara wafanyabiashara wanalipia sana hii kitu, sijui wanaita gani vilee nimesahau. Yani kabla TRA hawajakupa leseni ya biashara, lazima upeleke mkataba wa fremu yako..
Hiyo sio kodi mpya inaitwa withholding tax, wafanya biashara wamekuwa wakiilipa pale wanapokuwa wamekodi frem/nyumba ya kufanyia biashara.Unapokwenda TRA, kufuatilia number ya TIN, lazima tu utatakiwa kupeleka mkataba wa pango.

Hii kodi anatakiwa kulipa mwenye nyumba ila wao wanashindwa kumfikia mwenye nyumba ndio wanambana mpangaji, ila kwa nyumba ambazo ni za makazi tu na hazina fremu za biashara itakuwa ni ngumu kidogo kuzifikia, labda hili zoezi wawatumie viongozi wa mtaa kuzitambua, japo nako ni ngumu,
 
Hii kwa wafanyabiashar ailikuwepogo na uzuri ilikuwa wanakamatiwa wakifuata leseni hupewi leseni hadi ulipe hii sasa kwa watu binafsi sijui serekali itafanyaje sasa sijui
 
Hii nchi inavituko sana kwa hiyo TRA mmeshindwa kupita mitaani kuzisajili nyumba zote zinazofanya...
Hii nchi uwezo wa kufikiri umefika mwisho,waliopo kwenye madaraka, kuanzia Raisi, mawaziri, wabunge, wakurugenzi na viongozi waandamizi kwenye mashirika ya umma,uwezo wao umefika mwisho kabisa.
 
Watajua hawajui. Kama kodi ni 200,000 nitaandika mkataba wangu kuwa napangisha nyumba yangu kwa kiasi cha 50,000. hiyo laki na nusu namwambia mpangaji anipatie mkononi. Halafu tuone sasa watapata nini.
GAAR(General Anti-avoidance Rule) inawaruhusu Tra kufanya 'assumption' ya Kwamba nyumba hio inatakiwa kupangishwa at a 'Market Value',watafanya assumption ya nyumba Kama hio kwa hadhi yake wenye nyumba wengine wanalipwaje Kodi then na wewe utaambiwa Rent unayostahili kulipwa na amount ya mpangaji ku-withhold.
 
Nazani Sasa ndio mda muafaka wa mabadiliko ambayo vyama vya upinzani walikuwa wanatuaadaa wanataka kwa sababu mama kawarambisha asali wapinzani wametula hawana kelele zao kama enzi za mwenda zake huu ujinga wa tozo ulikuwa haupo ila wapinzani walipiga kelele wanaonewa wanabanwa ila Sasa upo ujinga wa wazi wazi ambao unaibua hisia za mtu kwakua wapinzani wametula na jamii ndio Ina feel the bit ipo siku litaibuka jambo hawatamini Kila mtu atatoka barabarani bila mbiu ya jamani tuandanane
 
Kodi ya pango si imeshakatwa kwenye LUKU, mbona haya mambo sasa yanakuwa too much...
Na Bado Kuna Kodi ya kiwanja ambayo inalipwa kwa mwaka nadhani, hivo kwenye nyumba tunalazimishwa kulipa Kodi mara tatu
 
TRA inahangaika na vikodi vidogo kama hivi!tumekosea wapi kama nchi?Botswana na Tanzania tumepata uhuru wa benders within 5yrs, mbona kuna tofauti kubwa mno kati yetu?what's went wrong kwa nchi yetu?,hizi vikodi vilitakiwa kukusanywa na metros na municipalities, TRA wajibu wao ni kukusanya super taxes
 
Hii nchi inavituko sana kwa hiyo TRA mmeshindwa kupita mitaani kuzisajili nyumba zote zinazofanya biashara...
Wenye nyumba kodi wanakatwa kwenye luku wanaponunua umeme na nyumba nyingi wapangaj ndio tunaonunua umeme kwahiyo tunawalipia wenye nyumba kodi ya pango na bado tena wanasema tulipe asilimia kumi nani atatutetea sisi wanyonge??
 
Back
Top Bottom