Sobangeja
JF-Expert Member
- Apr 10, 2011
- 401
- 354
Akijigamba waziri wa fedha na uchumi alidai mamlaka ya mapato Tanzania TRA wamekusanya kodi ya zaidi ya asilimia 106%.Je, kiasi hicho cha kodi kilichokusanywa kinalinganishwa dhidi ya kiasi kipi? Wakati tunaambiwa TRA imeshindwa kukusanya kodi toka makampuni ya madini kwa takribani bilioni moja kila mwezi.Makampuni ya simu yaliyoko Tanzania yamelipa kodi ya trilioni 1.7 kwa wateja milioni 15 wakati Rwanda yenye wateja 4.4 milioni imekusanya kodi inayozidi trilioni 32,Je wizi huu TRA wameubaliki na kukubaliana nao?Mbunge wa jiji moja gari lake halijalipiwa kodi ya mapato kwa zaidi ya mwaka mmoja.Je watu wa aini hii wapo wangapi na ni kiasi gani hakijakusanywa? Nionavyo mimi hicho kiasi walichokusanya hakilingani na kiasi halisi walichopaswa kukusanywa.Hii ni kiini macho kuonesha serikali hii inafanya kazi kumbe hakuna lolote.Karibuni wa JF wenye data za kina tuchangie juu ya hili la kukusanya kodi 106% wakati kodi kibao bado hazijakusanywa.