TRA na malipo ya Fire extinguisher.

TRA na malipo ya Fire extinguisher.

kerubi afunikaye

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2013
Posts
1,183
Reaction score
1,061
Wadau wenzangu humu Jf naomba mnielimishe labda mimi sijaelewa.Nimekwenda kulipia road licence ya gari yangu TRA.

Kufika pale nikapewa figure kubwa mno.Nauliza naambiwa ni road licence, penalty ya miezi miwili na makato ya fire extinguisher.

Nikawaomba hiyo fire extinguisher wakasema hawatoi.Nikawauliza kama wao hawatoi niifuate wapi, wakasema nikanunue madukani zimejaa tele.

Nikawauliza kwa nini sasa wanatoza hii kitu kwenye road licence wakaniambia nikaiulize serikali, wao ni watekelezaji tu.

Sasa kabla sijafika ikulu kwa serikali, nimeonelea nije humu jf kwenu watanzania wenzangu niwaulize kuhusu hii kitu, hivi hii ni haki jamani? Ulipie kitu usichopewa halafu bado huko barabarani sheria inakubana uwe nacho, na ukienda dukani unakinunua elfu 12, 15 huku TRA wameshakulipisha 30000 bila kukupa? Sasa hizi elfu 30 za nini? Wengine tayari tulishakuwa nazo hizi kitu tumenunua huko previously, sasa kwa nini nazilipia? Hebu naomba elimu kwa mlipa kodi hapa.
 
Pole sana mkuu hii nchi ina usengerema mwingi sana.. Hili suala mi nilishaamua kulikaushia tu nikisubiri tuwangoe hawa mambwiga madarakani kwanza..
 
Wadau wenzangu humu Jf naomba mnielimishe labda mimi sijaelewa.Nimekwenda kulipia road licence ya gari yangu TRA.

Kufika pale nikapewa figure kubwa mno.Nauliza naambiwa ni road licence, penalty ya miezi miwili na makato ya fire extinguisher.

Nikawaomba hiyo fire extinguisher wakasema hawatoi.Nikawauliza kama wao hawatoi niifuate wapi, wakasema nikanunue madukani zimejaa tele.

Nikawauliza kwa nini sasa wanatoza hii kitu kwenye road licence wakaniambia nikaiulize serikali, wao ni watekelezaji tu.

Sasa kabla sijafika ikulu kwa serikali, nimeonelea nije humu jf kwenu watanzania wenzangu niwaulize kuhusu hii kitu, hivi hii ni haki jamani? Ulipie kitu usichopewa halafu bado huko barabarani sheria inakubana uwe nacho, na ukienda dukani unakinunua elfu 12, 15 huku TRA wameshakulipisha 30000 bila kukupa? Sasa hizi elfu 30 za nini? Wengine tayari tulishakuwa nazo hizi kitu tumenunua huko previously, sasa kwa nini nazilipia? Hebu naomba elimu kwa mlipa kodi hapa.
Wewe ndo kati ya wale wakwepaji kodi za Serikali, sasa umeshapewa majibu kamuulize Serikali, sasa humu unamuuliza nani? Na hiyo taarifa uloeleza sio ya kweli kwamaba imekutokea wewe, wewe umeskia watu ukaona uje kuiweka humu ndani, acha uongo na uache kupotosha umma!
 
Pole sana mkuu hii nchi ina usengerema mwingi sana.. Hili suala mi nilishaamua kulikaushia tu nikisubiri tuwangoe hawa mambwiga madarakani kwanza..
Wewe na mtoa taarifa mnapokwepa kulipa kodi mkibanwa mnaisema vibaya serikali mnategemea nini? Lipeni kodi muone kama mtabanwa! Acheni wehu humu ndani
 
Wewe na mtoa taarifa mnapokwepa kulipa kodi mkibanwa mnaisema vibaya serikali mnategemea nini? Lipeni kodi muone kama mtabanwa! Acheni wehu humu ndani

Acha upuuzi wewe.. Unajua hata kinachoongelewa hapa au umekurupuka tu?
 
Ndio Makongoro anawaita vibaka. Home Shopping Centre halipi kodi. Wenye magari wanakamuliwa hadi tone la mwisho.
Kulipia vitu hewa. Na kodi zenyewe wanatafuna
 
Wewe ndo kati ya wale wakwepaji kodi za Serikali, sasa umeshapewa majibu kamuulize Serikali, sasa humu unamuuliza nani? Na hiyo taarifa uloeleza sio ya kweli kwamaba imekutokea wewe, wewe umeskia watu ukaona uje kuiweka humu ndani, acha uongo na uache kupotosha umma!
Ndio maana nikasema nielimishe mkuu.Kama una taarifa sahihi weka hapa kwa faida yangu na wananchi wengine waliosikia huu uzushi.Au sio?
 
Wewe na mtoa taarifa mnapokwepa kulipa kodi mkibanwa mnaisema vibaya serikali mnategemea nini? Lipeni kodi muone kama mtabanwa! Acheni wehu humu ndani
Mkuu, hii elfu 30 ya fire extinguisher kwenye road licence ni ya nini? Hebu nielimishe mkuu inaonekana wewe ni mwandani wa serikali.
 
Ndio maana nikasema nielimishe mkuu.Kama una taarifa sahihi weka hapa kwa faida yangu na wananchi wengine waliosikia huu uzushi.Au sio?

Kwa kweli kodi hizi feki zinauma sana hasa kwa sisi wafanya kazi wa serikali ambao tunalipa kodi kubwa sana wakati wenzetu wafanya biashara wanajitahidi kukwepa.

Siku hizi mbali ya hiyo fire 'tingisha' ukichelewa hata kwa siku moja baada ya mwezi wa kuexpire road licence basi hiyo faini hutasahau tena mwaka wa pili.

Mimi mwaka jana nilichelewa kama siku tatu baada ya deadline ya mwezi mmoja basi nililipa faini ya elfu sabini, sitini kwa road licence na kumi kwa huyo 'tingisha'. Can you imagine, fire extinguisher yenyewe unalipia feki, halafu ukichelewa unapigwa faini ya hiyo feki.
 
Wakuu mngemwelimisha sio kumkashifu. Hiyo pesa uliyolipa tulikuwa tunailpa kule fire baada ya kupeleka fire extinguisher yako kukaguliwa (annually). Sasa wameichanganya na road licence. Mimi sina shida ila mbona tunalipa na haikaguliwi kwanza?
 
Kinachofanyika ni kwamba hiyo tozo si ya TRA Bali in huduma ya ukaguzi wa gari kuhusu usalama dhidi ya ajali za moto ambayo huko nyuma ilikuwa inalipwa kikosi cha zima moto. Serikali iliamua TRA wakusanye ada hiyo pamoja na road licence kwa niaba ya idara ya zima moto.

Ukiishalipa unatakiwa kununua kifaa cha zimamoto na kisha kwenda kikosi cha zimamoto ili chombo chako kikaguliwe na kupewa nadhani stika ambayo utsbandika kwenye gari yako.
 
Kinachofanyika ni kwamba hiyo tozo si ya TRA Bali in huduma ya ukaguzi wa gari kuhusu usalama dhidi ya ajali za moto ambayo huko nyuma ilikuwa inalipwa kikosi cha zima moto. Serikali iliamua TRA wakusanye ada hiyo pamoja na road licence kwa niaba ya idara ya zima moto.

Ukiishalipa unatakiwa kununua kifaa cha zimamoto na kisha kwenda kikosi cha zimamoto ili chombo chako kikaguliwe na kupewa nadhani stika ambayo utsbandika kwenye gari yako.

Jay milionea, unajua ni watz wangapi wameelimika na wataendelea kuelimika kwa bandiko kama hili la mkuu Theo? Wakati mwingine tujifunze mbinu mbalimbali za kutumia ili kuelimisha wananchi.Sasa nendeni mitaani mkasikie jinsi watu wanavyolalamikia hiyo kitu.

Ahsante sana Theo.I wish majibu kama haya yangekuwa yanatolewa na wale jamaa wa reception pale TRA badala ya kutoa majibu ya mkatomkato.We unaingia kwenye simu unauliza KADIRIA unakutana na figure za ajabu bila maelezo, kwa nini watu wasilalamike? Vitu vingine vinahitaji elimu tuu, sio nguvu.
 
Back
Top Bottom