TRA mmekutwa na nini?

TRA mmekutwa na nini?

UrbanGentleman

JF-Expert Member
Joined
Jun 19, 2016
Posts
2,584
Reaction score
1,886
Hi kitu sasa imekua kero na imefikia hatua inachosha kiasi uvumilivu umenishinda kabisa.

Nilikua najua hapa kazi ni kazi kweli kumbe Hakuna lolote ni ubabaishaji wa hali ya juu kiwango cha kukatisha tamaa.

Tarehe 17 mwezi wa 9 nilipeleka leseni yangu kurenew pale samora house sababu ilishapitwa na wakati nisije tengeneza kisababisho cha vyeti vya kipuuzi.

Sasa tangu tarehe 17/9/2017 mpaka leo tarehe 7/11/2017 means huku ni kukomoana huwezi chukua duplication fee af nusubiri miezi mitatu ndio nipewe huduma huu ni uzembe kuanzia uongozi wa juu mpaka chini.

Kweli hii ni hapa kazi au maneno ya mdomoni kufurahishana tu?
 
hapo ni samora.... nambie alieenda tawi la nanjilinji huko ndani ndani!!!

kuna taasisi haziko serious
 
Kuwa na subira mzee. Au wafate huko huko.
 
Nimelipa tarehe 20/7/2017 mpaka jana tarehe 6/11/2017 sijapata leseni mpya
 
Pole kwa usumbufu,ila dawa ya yote haya ni kurudisha utoaji wa leseni hizi kwa mamlaka husika,driving licences zirudishwe traffic dept.na za biashara ndogo ndogo serikali za mitaa ndio wajibu wao,TRA wao wahusike na kodi kubwa na sidhani kama tuna kitengo cha VIP kinachojihusisha zaidi na viongozi wa kitaifa including our no 1(sijawahi kusikia tax returns zake,na hii ni haki yangu kama mlipa kodi wa nchi),TRA wadeal zaidi na makampuni makubwa ,offshore accounts;sio kukimbizana na driving licences
 
Pole kwa usumbufu,ila dawa ya yote haya ni kurudisha utoaji wa leseni hizi kwa mamlaka husika,driving licences zirudishwe traffic dept.na za biashara ndogo ndogo serikali za mitaa ndio wajibu wao,TRA wao wahusike na kodi kubwa na sidhani kama tuna kitengo cha VIP kinachojihusisha zaidi na viongozi wa kitaifa including our no 1(sijawahi kusikia tax returns zake,na hii ni haki yangu kama mlipa kodi wa nchi),TRA wadeal zaidi na makampuni makubwa ,offshore accounts;sio kukimbizana na driving licences
Jamaa amefail big time
 
Yangu nimelipia tarehe 11/09/2017 hadi leo. Labda hizi material za leseni zinatengenezwa na chembechembe za Bombadier iliyoshikiliwa kule Canada.

Hawana wasiwasi wanajibu "material hamna"
Sasa najiuliza sijui anampango gani huyu jamaa
 
Si msemaji wa serikali kasema nidhamu na ufanisi serikalini vimepanda, au vipi?
 
Kwakweli ni kero sana haswa kwa madriver wanaenda Kenya mkuu tunawaomba mshuhulikie hili jambo mara moja
 
Back
Top Bottom