TRA hawajui maana ya shortlisting ?

TRA hawajui maana ya shortlisting ?

Usilalamikie shortlist hilo ni bomu litalipuka siku moja maana hiyo ni indicator kwamba hakuna ajira na viongozi wetu wanalichukulia simple wameshindwa kuwa wabunifu na ku explore more jobs. Nawaomba tuache ushabiki wa kisiasa tuzisome ilani za vyama vyetu vya siasa tuchague chama chenye ilani itakayotutoa kwenye umaskini wakujitakia na ukosefu waajira.
.
 
Hakunaa! Survival of the fittest ndio mpango mzima. Mnataka wafanye shortlisting alafu baadaye muanze kusema walipendelea ndugu zao?
 
hivi t.r.a kuna nini wakati wafanyakazi wa forever wameacha nyie mnakimbilia(hii kauli huwa inaboa sana sana tena sana
 
Mi navofaham.. inpendekezwa shortlisting ifanyike kwa ratio ya 1/3 or 1/4.. yaani kama unahitaji watu 20 hardly unaweza kuita watu for interview kama 60 had 80... lkn kuita watu 1000 is inefficiency .. labda kuwepo na justfication nyingine
 
hiyo ni indicator kwamba hakuna ajira na viongozi wetu wanalichukulia simple wameshindwa kuwa wabunifu na ku explore more jobs.
.

Nani kakwambia Tanzania hakuna ajira kwa wasomi? Hiyo mistari mirefu unayoona ya wasio na ajira tatizo ni wao wenyewe.Wanasomea vitu ambavyo sio kipau mbele KWENYE SOKO LA AJIRA

Nenda kaangalie waliosomea fani zifuatazo kama waajiri wanapata shida ku-shortlist

1.UALIMU kuanzia wa msingi hadi vyuo vikuu
2.Udaktari
3.Mainjinia wa fani mbali mbali
4.Wataalamu wa kilimo na mifugo
5.Wasomi wanaotaka kujiunga na majeshi

Pia Tatizo liko kubwa masomo ya arts (wasanii) Ukisomea usanii (ARTS) waajiri wengi hawapendi wasanii hata wawe na phd in arts subjects!!!!!

MTU ASISOME TU ILI MRADI AWE NA DIGRII aangalie nchi na ajira zinataka nini kwenye soko la ajira.
Watui wanapenda masomo laini kusoma ni kweli yanakuwa laini kusoma lakini baadaye yanakuwa magumu kupata kazi.Ndio unakuta watu elfu ishirini wanagombea nafasi 10 TRA!!!!
 
wanasema majibu yanatoka baada ya saa 24 toka umemaliza kufanya mtihani..

Unaweza kutoa majibu ya zaidi ya watu 1000 waliofanya mitihani ndani ya 24 kweli..? Hii imeshapangwa matokeo.. Wamefanya hivi ili ionekane machoni mwa umma kwamba ajira imefuata abc.. Lakini majibu tayari wanayo..
 
Mi navofaham.. inpendekezwa shortlisting ifanyike kwa ratio ya 1/3 or 1/4.. yaani kama unahitaji watu 20 hardly unaweza kuita watu for interview kama 60 had 80... lkn kuita watu 1000 is inefficiency .. labda kuwepo na justfication nyingine
Hiyo yaweza kuwa kweli kama unatakaka kuajiri proffesionals with experience n.k Lakini kama unataka direct from univercity labda utumie vigezo vya kuwagawa kama umri usizidi miaka labda 20,class ya degree zao na performance zao at secondary and primay level,gender,marital status,etc vigezo ambavyo ni discriminatory Lakini kama unataka equal opportunity for all inatakiwa uwaite wote wajaribu bahati zao kwenye interview
 
Siku hizi wamebalisha mfumo zamani ukiwa una jina la Mmari,Mrema ,Kimario,Lema una ajiriwa bila inaterview!
 
Usilalamikie shortlist hilo ni bomu litalipuka siku moja maana hiyo ni indicator kwamba hakuna ajira na viongozi wetu wanalichukulia simple wameshindwa kuwa wabunifu na ku explore more jobs. Nawaomba tuache ushabiki wa kisiasa tuzisome ilani za vyama vyetu vya siasa tuchague chama chenye ilani itakayotutoa kwenye umaskini wakujitakia na ukosefu waajira.
.

Umenena mkuu...
 
Back
Top Bottom