Sasa mkuu, hayo marekebisho ndio kwanza leo yamechapishwa kwenye gazeti la serikali, na kuna baadhi ya sheria lazima zikabadirishwe bungeni leo tu unataka kuona mabadiriko?hata hivyo huo mzigo wa mafuta ulioingia lazima tozo zote hizo zimo, .kama kweli wana nia ya dhati kutakuwepo na mabadiriko fulani ya bei za mafuta nchi, kwani kuna tozo nyingine, za ajabu eti tozo ya TRA, ya kuchakata data!!tozo ya EWURA, ya kupima kina cha mafuta kwenye meli!!ndii maana tulikuwa miaka yote tunaulizana inakuwaje, MALAWI, DRC, ZAMBIA, mafuta yao yanapita hapa lakini kule kwao bei inakuwa chini zaidi kuliko hapa?!!wakiulizwa wanakimbilia ohooo soko la dunia mafuta yamepanda, kwani hao wengine wanayachukulia soko la angani??hii nchi na wanachi wake ni wakuhurumiwa tu!!