Tonge
JF-Expert Member
- May 7, 2010
- 696
- 12
- Thread starter
- #21
Hii ndio Tanzania zaidi ya uijuavyo,ni kwamba hilo goma ni famba na hasara kwa Taifa,marekani waliyarudisha Tanzania tunangoja nini basi na yako kama 12 hivi maana jana tu JK alikuwa analitumia moja hapa moshi, jiulize limetoka dar tupu kumfuata mkulu moshi, na hilo wese lililo kula si chini ya lita 500 toka dar to moshi bado kurudi. Wanasema ni bullet proof, kwani ukitaka kumtungua raisi unasubiri awe kwenye gari? Mbona yule muungwana wa mwanza alimkata mtama jukwaani? Sielewi kama ni kweli moshi hakuna gari ambalo rais anaweza kutumia wakati wa ziara yake, hii bado ni matumizi mabaya ya fedha za serikali. Tubadilike wajameni.