Toyota Duet

Toyota Duet

Wanajamvi,
Nipo mbioni kumiliki gari aina ya Toyota duet,ninaomba kwa wazoefu waliokwisha litumia gari hilo wanijuze ufanisi wake pamoja na mapungufu yake.
Nawakilisha.

Wewe ni mwanafunzi? Kama sio mwanafunzi itabidi utafute cha kuwaeleza wanafunzi kwa nini unaanzia gari yao. Usianzie chini hivyo mkuu, anza walau na Mark II.
 
Hahahahahahàaaaaaaaaa kwikwikwiiiiiiii mwenye carina nae anajiona ana gari, mwenye vx atasemaje? ana kifaru au? acheni ufala. Mshikaji kauliza ili ashauriwe acha kumkashifu sababu una carina hujui mwenye vx anakuona boya tu barabarani? Mimi binafsi siwezi endesha carina man lol.
 
Mdukuzi,Duh!Umeongea kwa madharau sana,kumbuka tunatofautiana kwa kipato.Heri yako unayetembelea gari za ma-officer.Uwezo wangu kwa sasa ni hapo (magari ya mahouse girl)

dah mwana umeongea kinyonge mpaka nimejiskia vbaya.ucjal kaza tu hata Baresa alianza kwa kupiga kiwi
 
Iyo gari bei yake ikoje ukiagiza nje na hapa bongoland inasimamia ngapi vile maana naona inanivutia mimi mjasiriamali mgumu
 
tofauti ya masikini na tajiri ni mtazamo tu tofauti ni jinsi ya kutafuta pesa na jinsi ya kuzitumia unaweza kupata corola kwa bei hiyohiyo ya duet mind you kitu aset sio cha kubadili kila siku.nataka nikupe falsafa ya gari ndugu yangu,gari inaweza kukupaisha au kukushusha status imagine leo upite na volkswagon kobe na mimi nipite kwenye taxi safi nani zaidi,au jibaba na likitambi lake na tai shingoni lipo kwenye kigari kama cha mr bean,ndio maana nikasema tulia waweza kupata corola safi kwa bei hiyo achana na vigari kama viberiti hata ukipigiwa simu ya dharura hapo morogoro unajiuliza mara mbili upande abood au utumie gari
 
mkuu chukua tu hiyo gari mimi mwenyewe walinitisha sana wadau wa humu jf lakini ubishi wangu ulinifanya niagize na huu ni mwaka unaenda wa tatu, nilikuwa natumia chevrolet suv nilinunua ughaibuni nimetumia kama miezi sita hapa bongo kwa safari za mjini na nyumbani lakini nikaona nalifanyia kazi gari kwani lilikuwa linakula sana mafuta,nikaamua niwe nalitumia kwa safari za mbali sana na nikanunua Duet, niliifanyia modifications kama kuinyanyua juu pamoja na kuifunga sports tires na rims za size kumi na nne,uwezi amini nasafiria Tanga kila week ends na gari iko stabble barabarani hata ukipishana na roli haiyumbi na ulaji wake wa mafuta ni mzuri sana,km 14 hadi 20 kwa lita moja, cha muhimu ni service tu na spare zake zinapatikana sana siku hizi tofauti na zamani.
 
toyota carina,naishi kimara shida ya maji kila siku naweka madumu manne nikienda kazini nakuja na maji ya kuoga na kupikia ,ingekuwa hiyo duet si itakuwa majanga

kwa style hiyo nina uhakika una no za maduka ya spare za magari kama 20 hivi, lazma uwe mteja wao mkubwa wa kununua showcups :smile-big:
 
kwa kuwa unaanza kutumia magari anza na duet mpaka ukijua gari vizuri ndio ununue gari poa la ela ndefu
 
mh humu ndani unaweza usiombe msaada! hahahahhaa
 
Kuna jirani yangu mmoja hapa anayo tangu mwaka jana june gari inakua na miss mpaka AC hawezi kuwasha, na kashazunguka sana kwa mafundi kila wakipima diagnosis inasema plague, lakin akibadili plague mziki ni hule hule.......na watu wengi niliojaribu kuwauliza wanasema zile gari nzuri lakin ukishaanza kuigusa engine ujue itakuua na mawazo,
So far chukua kama ndio umeshailipia maana hata tukikwambia ni kimeo haitasaidia
 
Kuna jirani yangu mmoja hapa anayo tangu mwaka jana june gari inakua na miss mpaka AC hawezi kuwasha, na kashazunguka sana kwa mafundi kila wakipima diagnosis inasema plague, lakin akibadili plague mziki ni hule hule.......na watu wengi niliojaribu kuwauliza wanasema zile gari nzuri lakin ukishaanza kuigusa engine ujue itakuua na mawazo,
So far chukua kama ndio umeshailipia maana hata tukikwambia ni kimeo haitasaidia

Hao mafundi aliowapata wanakula pesa yake tu miss ya hizo gari hazisababishwi na plug,nozzle kama chafu lazima itakuwa na miss na kuhusu kugusa injini ndio gari inakufa sio kweli ya kwangu niliifanyia overhaull baada ya kuanza kutoa moshi mweupe na sa hivi iko poa sana nasafiria nayo kama kawaida haijawahi kunisumbua tena.
 
gari ya mahouse gal kwendea markit ongeza kidogo tafuta corola hivi vigari visivyo na boot nyuma mimi huwa naona vimekaa kitoto au kihouse gal siwezi kuendesha bora nipande taxi

Mkuu unatumia gari gani vileeeeeeeeeeee
 
mkuu chukua tu hiyo gari mimi mwenyewe walinitisha sana wadau wa humu jf lakini ubishi wangu ulinifanya niagize na huu ni mwaka unaenda wa tatu, nilikuwa natumia chevrolet suv nilinunua ughaibuni nimetumia kama miezi sita hapa bongo kwa safari za mjini na nyumbani lakini nikaona nalifanyia kazi gari kwani lilikuwa linakula sana mafuta,nikaamua niwe nalitumia kwa safari za mbali sana na nikanunua Duet, niliifanyia modifications kama kuinyanyua juu pamoja na kuifunga sports tires na rims za size kumi na nne,uwezi amini nasafiria Tanga kila week ends na gari iko stabble barabarani hata ukipishana na roli haiyumbi na ulaji wake wa mafuta ni mzuri sana,km 14 hadi 20 kwa lita moja, cha muhimu ni service tu na spare zake zinapatikana sana siku hizi tofauti na zamani.

Nashukuru kwa kunitia moyo.
 
Back
Top Bottom