OLS
JF-Expert Member
- Oct 12, 2019
- 419
- 670
UCHUMI KWA WASIO WACHUMI
Sio neno geni, lakini kama ilivyo kawaida kwa watu wasio na utaalamu wa somo husika kutumia maana zinazowafanya wachanganye maneno. Uchumi ni ile hali ya kufanya rasilimali kuendelea kuwepo kwa matumizi kwa muda mrefu bila kuathiri kwa ukubwa rasilimali nyinginezo. Mchumi ni mtu anayeelekeza rasilimali katika hali ya kukuza rasilimali husika. Rasilimali zinazoheshimiwa katika uchumi ni pamoja rasilimali pesa, rasilimali watu, rasilimali muda, mazingira nk.
TOFAUTI YA MCHUMI NA BAHILI
Kutokana na kukosa namna ya kutofautisha maneno husika, watu wengi wamekuwa wakichanganya maneno hayo. Nimeeleza awali kuwa nia ya mchumi ni kukuza rasimali inayokuwa haba wakati husika, japo rasilimali zote ni haba, ila hazina usawa katika uhaba wake. Hivyo mchumi huangalia rasilimali zote ili kujua rasilimali ipi ni ya kuikuza (maximize) kwa wakati husika.
Tofauti kubwa kati ya mchumi na mbahili ni kuwa, mbahili huangalia pesa kama rasilimali pekee na hivyo hupoteza rasilimali nyingine au mara nyingine hupoteza hata pesa aliyonayo.
Mfano wa kawaida ni kwa baadhi ya watu wa serikali kukataa baadhi ya miradi kutokana na gharama, kwa kuwa wao huona pesa ni rasilimali pekee, huweka miundombinu ya gharama nafuu ambayo inawafanya(kwenye long run) kuingia gharama kubwa kuliko walioikwepa mwanzo. Mfano ni ujenzi wa barabara ambazo kila mwezi zimekuwa zikikarabatiwa, hii ni kwa sababu wanatamani kuiweka hela ila wanakosa ufahamu wa namna nzuri kuiweka, hivyo basi utaona wazi kuwa wanaoitwa wachumi walioko katika idara husika ni wabahili, kama si wabahili basi ni wala rushwa ambao hawaoni umuhimu wa kutumia ujuzi wao katika kutengeneza miundombinu iliyobora badala yake hugawana hela.
Moja kati ya swali ambalo linamtofautisha mchumi na mbahili ni lile ambalo linauliza ipi ni njia ya kiuchumi Zaidi ya kusafiri kutoka Dar hadi Mwanza, kwa kutumia gari, treni au ndege? Hili swali ukiliangalia kiubahili utaangalia usafiri wenye nauli kidogo bila kuangalia kitu gani unataka kukikuza(maximize) kwa wakati husika. Taarifa za swali hazijakamilika hivyo wakati wa kujibu swali kama hilo ni lazima uweke scenarios au kiuchumi wanaita assumptions ili kutetea kwa nini kusafiri kwa usafiri Fulani ni ya kiuchumi Zaidi kuliko nyingine.
Katika swali kama hilo, mchumi hatoangalia gharama za nauli bali kitu anachotaka kukikuza kwa wakati husika. Huwezi kupanda treni wakati una mgonjwa wa dharura, kwa hiyo kama hela ipo ili kukuza rasimali mtu, itabidi upande ndege.
Ni mfano kama huu naweza kuutoa kutofautisha, inawezekana mtu yuko anakula chakula cha elf 15 lakini anapigiwa simu na kutakiwa kuwepo mahali kwenye kazi ya shilingi laki mbili, hapo mchumi ataacha chakula na kuiwahi hiyo kazi ikiwa anataka kukuza rasimali muda, yaani kama kula kunaweza kumchelewesha, ili afuate hiyo kazi basi mchumi ataacha chakula hata kama amelipa.
Lakini mbahili atabaki amalize chakula hata kama itaathiri muda wa yeye kufika kwenye kazi ya laki mbili na Zaidi.
Signed
Oedipus
Sio neno geni, lakini kama ilivyo kawaida kwa watu wasio na utaalamu wa somo husika kutumia maana zinazowafanya wachanganye maneno. Uchumi ni ile hali ya kufanya rasilimali kuendelea kuwepo kwa matumizi kwa muda mrefu bila kuathiri kwa ukubwa rasilimali nyinginezo. Mchumi ni mtu anayeelekeza rasilimali katika hali ya kukuza rasilimali husika. Rasilimali zinazoheshimiwa katika uchumi ni pamoja rasilimali pesa, rasilimali watu, rasilimali muda, mazingira nk.
TOFAUTI YA MCHUMI NA BAHILI
Kutokana na kukosa namna ya kutofautisha maneno husika, watu wengi wamekuwa wakichanganya maneno hayo. Nimeeleza awali kuwa nia ya mchumi ni kukuza rasimali inayokuwa haba wakati husika, japo rasilimali zote ni haba, ila hazina usawa katika uhaba wake. Hivyo mchumi huangalia rasilimali zote ili kujua rasilimali ipi ni ya kuikuza (maximize) kwa wakati husika.
Tofauti kubwa kati ya mchumi na mbahili ni kuwa, mbahili huangalia pesa kama rasilimali pekee na hivyo hupoteza rasilimali nyingine au mara nyingine hupoteza hata pesa aliyonayo.
Mfano wa kawaida ni kwa baadhi ya watu wa serikali kukataa baadhi ya miradi kutokana na gharama, kwa kuwa wao huona pesa ni rasilimali pekee, huweka miundombinu ya gharama nafuu ambayo inawafanya(kwenye long run) kuingia gharama kubwa kuliko walioikwepa mwanzo. Mfano ni ujenzi wa barabara ambazo kila mwezi zimekuwa zikikarabatiwa, hii ni kwa sababu wanatamani kuiweka hela ila wanakosa ufahamu wa namna nzuri kuiweka, hivyo basi utaona wazi kuwa wanaoitwa wachumi walioko katika idara husika ni wabahili, kama si wabahili basi ni wala rushwa ambao hawaoni umuhimu wa kutumia ujuzi wao katika kutengeneza miundombinu iliyobora badala yake hugawana hela.
Moja kati ya swali ambalo linamtofautisha mchumi na mbahili ni lile ambalo linauliza ipi ni njia ya kiuchumi Zaidi ya kusafiri kutoka Dar hadi Mwanza, kwa kutumia gari, treni au ndege? Hili swali ukiliangalia kiubahili utaangalia usafiri wenye nauli kidogo bila kuangalia kitu gani unataka kukikuza(maximize) kwa wakati husika. Taarifa za swali hazijakamilika hivyo wakati wa kujibu swali kama hilo ni lazima uweke scenarios au kiuchumi wanaita assumptions ili kutetea kwa nini kusafiri kwa usafiri Fulani ni ya kiuchumi Zaidi kuliko nyingine.
Katika swali kama hilo, mchumi hatoangalia gharama za nauli bali kitu anachotaka kukikuza kwa wakati husika. Huwezi kupanda treni wakati una mgonjwa wa dharura, kwa hiyo kama hela ipo ili kukuza rasimali mtu, itabidi upande ndege.
Ni mfano kama huu naweza kuutoa kutofautisha, inawezekana mtu yuko anakula chakula cha elf 15 lakini anapigiwa simu na kutakiwa kuwepo mahali kwenye kazi ya shilingi laki mbili, hapo mchumi ataacha chakula na kuiwahi hiyo kazi ikiwa anataka kukuza rasimali muda, yaani kama kula kunaweza kumchelewesha, ili afuate hiyo kazi basi mchumi ataacha chakula hata kama amelipa.
Lakini mbahili atabaki amalize chakula hata kama itaathiri muda wa yeye kufika kwenye kazi ya laki mbili na Zaidi.
Signed
Oedipus