Tofali juu ya Paa la Ocean Road Hospital

namimih

Member
Jan 4, 2012
64
20
Jamani kuna vioja huwa naviona hapa mjini vyengine nanyamazia kwa kuamini wahusika labda hawana uwezo wa kugundua uzembe huo au ni uwezo wao mdogo.
Lakini hebu tuliangalie hili la tofali kuwekwa juu ya paa la jengo la Hospitali ya Ocean lile jengo kubwa linaloangalia baharini, naamini tofali hilo limewekwa kuzuia Antenna ya Tv au ya mawasiliano yao humo ndani, sasa kinachonisumbua ni kweli Hospitali ya Ocean Road haina watu wenye uwezo wa kufikiri kuwa kuweka tofali kule juu siyo sawa, au hakuna njia ya kitaalamu ya kuifunga hiyo antenna mpaka kuwekwe tofali ambalo naamini kazi ilikuwa ni ya kujengea na siyo ya kuwekwa juu ya paa tena ya moja ya hospitali kubwa Tanzania, wahusika hebu angalieni ulalaji wa akili zenu.
 
Back
Top Bottom