MwanaFalsafa1
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 5,565
- 836
TIOT yatajwa kinara wa kukwepa kodi
2009-04-30 14:39:27
Na Hamisi Kibari
Bunge limeambiwa kwamba kuna udanganyifu mkubwa katika ulipaji wa kodi za mafuta kwa baadhi ya makampuni, huku kampuni la TIOT Limited likitajwa kuwa kinara wa kukwepa.
Aidha, serikali imeombwa kulichunguza kampuni hilo kupitia taasisi kama Takukuru ili kujua usugu wake wa kukwepa kodi unatokana na nini.
Akiwasilisha bungeni taarifa ya kazi ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kwa mwaka 2008/2009, mwenyeketi wa kamati hiyo, John Cheyo, alisema kwamba kamati yake ilielezwa na wahusika kwamba udanganyifu uliofanywa na makampuni ya mafuta ulikuwa na thamani ya sh. bilioni 38.4
``Kati ya hizo fedha, hoja yenye thamani ya sh. 35.5, sawa na asilimia 92.5 zilihusu kampuni moja tu ya TIOT,`` alisema Cheyo.
Alisema kamati yake ilielezwa kwamba kampuni hiyo ya TIOT ni sugu kwa ukwepaji wa kodi za mafuta.
``Aidha Kamati inaipongeza TRA kwa kuweza kukusanya sh. bilioni 29.8 ya hoja zote na kubakiwa na bakaa ya sh. bilioni 8.4 ambapo sh. Bilioni 5.6 pekee zinahusu kampuni ya TIOT,`` alisema Cheyo.
Alisema, Kamati yake ilielezwa kwamba njia inayotumiwa na kampuni hiyo ili kuzuia TRA kupata mapato yake kukimbilia mahakamani.``
``Kamati inapendekeza kwa serikali kufanya uchunguzi wa kina kwa kutumia vyombo vya serikali kama vile Takukuru ili kubaini msingi na ujeuri wa kampuni hii,`` alisema Cheyo.
Akihimitisha hoja yake baada ya Bunge kujadili ripoti yake, Cheyo aliomba ikiwezekana wakati kamati yake itakapokuwa ikiwahoji maofisa wa serikali, basi mambo yawe yanafanyika mbele ya kamera, ili baadaye yarushwe hewani na wananchi kusikia.
Alisema hivyo ndivyo inafanyika hata katika baadhi ya mabunge mengi ikiwemo Uganda.
SOURCE: NIPASHE
2009-04-30 14:39:27
Na Hamisi Kibari
Bunge limeambiwa kwamba kuna udanganyifu mkubwa katika ulipaji wa kodi za mafuta kwa baadhi ya makampuni, huku kampuni la TIOT Limited likitajwa kuwa kinara wa kukwepa.
Aidha, serikali imeombwa kulichunguza kampuni hilo kupitia taasisi kama Takukuru ili kujua usugu wake wa kukwepa kodi unatokana na nini.
Akiwasilisha bungeni taarifa ya kazi ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kwa mwaka 2008/2009, mwenyeketi wa kamati hiyo, John Cheyo, alisema kwamba kamati yake ilielezwa na wahusika kwamba udanganyifu uliofanywa na makampuni ya mafuta ulikuwa na thamani ya sh. bilioni 38.4
``Kati ya hizo fedha, hoja yenye thamani ya sh. 35.5, sawa na asilimia 92.5 zilihusu kampuni moja tu ya TIOT,`` alisema Cheyo.
Alisema kamati yake ilielezwa kwamba kampuni hiyo ya TIOT ni sugu kwa ukwepaji wa kodi za mafuta.
``Aidha Kamati inaipongeza TRA kwa kuweza kukusanya sh. bilioni 29.8 ya hoja zote na kubakiwa na bakaa ya sh. bilioni 8.4 ambapo sh. Bilioni 5.6 pekee zinahusu kampuni ya TIOT,`` alisema Cheyo.
Alisema, Kamati yake ilielezwa kwamba njia inayotumiwa na kampuni hiyo ili kuzuia TRA kupata mapato yake kukimbilia mahakamani.``
``Kamati inapendekeza kwa serikali kufanya uchunguzi wa kina kwa kutumia vyombo vya serikali kama vile Takukuru ili kubaini msingi na ujeuri wa kampuni hii,`` alisema Cheyo.
Akihimitisha hoja yake baada ya Bunge kujadili ripoti yake, Cheyo aliomba ikiwezekana wakati kamati yake itakapokuwa ikiwahoji maofisa wa serikali, basi mambo yawe yanafanyika mbele ya kamera, ili baadaye yarushwe hewani na wananchi kusikia.
Alisema hivyo ndivyo inafanyika hata katika baadhi ya mabunge mengi ikiwemo Uganda.
SOURCE: NIPASHE