Timu ya Lowassa yabadilisha staili

Timu ya Lowassa yabadilisha staili

habipty

New Member
Joined
May 4, 2015
Posts
2
Reaction score
1
KUNDI linalomuunga mkono Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, katika harakati zake za kuingia Ikulu Oktoba, mwaka huu, linalojulikana kama ‘Friends of Lowassa', limeandaa tukio kubwa la kihistoria wiki hii.

Kwa mujibu wa taarifa za ndani ya kundi hilo zilizolifikia gazeti hili mwishoni mwa wiki, wakati wowote wiki hii, makada wastaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), watakusanyika jijini Arusha kutoa tamko la ‘kumshawishi' Lowassa kutangaza nia ya kugombea urais.

Katika wiki chache zilizopita, waratibu wa shughuli za kampeni za Lowassa walibadili mbinu za kumshawishi kada huyo mkongwe agombee urais; na sasa badala ya ‘mashabiki' wao kufunga safari kumfuata aliko, huita vyombo vya habari, hususan TV, na kutangaza kumuunga mkono wakiwa huko huko waliko.

"Sasa hivi mipango inaendelea ili kundi kubwa la Watanzania litakalojumuisha wazee wa kimila wa Kimasai kutoka kila kona ya Arusha, siyo wa Monduli peke yao, pamoja na wenyeviti na makatibu wastaafu wa CCM wa mikoa ya Kanda ya Kaskazini wakusanyike hapa Arusha mjini kumuomba mzee atangaze haraka nia ya kugombea urais.

"Hii ya Arusha si mchezo, maandalizi yake ni makubwa mno kwa kuwa ndipo anapotoka mzee. Tukio hili litakuwa kubwa na baada ya hapo, basi! Hakutakuwa na makundi mengine tena yatakayotoa matamko kumshawishi mzee," alisema mmoja wa waratibu ndani ya Friends of Lowassa ambaye hatuwezi kumtaja gazetini kwa sababu za wazi kabisa.

Raia Tanzania linafahamu kuwa mipango yote kuhusu kufanyika kwa mkutano huo imekamilika na kwamba tukio hilo awali lilipangwa kufanyika wakati wa Sikukuu ya Pasaka, lakini likaahirishwa kutokana na wadau muhimu kuwa katika shughuli za mazishi ya mfanyabiashara mmoja wa Tanzanite aliyeuawa wiki iliyopita.

Majina ya baadhi ya wazee wa kimila na makada wastaafu wa CCM waliopewa taarifa za mkutano huo tunayo.

"Mbali na makada hao, pia wapo wazee maarufu wa Arusha na wazee kutoka vyama vya upinzani (hakutaja majina). Hii shughuli itakuwa kubwa kuliko zote zilizowahi kufanyika," alisema mtoa taarifa wetu.

Alisema mkutano huo mkubwa jijini Arusha utatumika pia kuujulisha umma wa Watanzania kwamba ingawa Arusha ni ngome ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Lowassa anakubalika kugombea nafasi ya urais.

Taarifa zaidi zinadai kuwa baada ya mkutano huo, mambo yatasitishwa kusubiri Lowassa atangaze nia yake; na kwamba mbunge huyo wa Monduli anatarajiwa kufanya hivyo ndani ya wiki mbili zijazo.

Mipango ya Lowassa kuweka hadharani nia yake hiyo imekuwa ikiahirishwa kwa zaidi ya mara nne sasa kutokana na sababu mbalimbali za kimkakati, kubwa ikiwa ni Lowassa kuwa katika uangalizi wa Kamati Ndogo ya Maadili ya Kamati Kuu ya CCM kwa kipindi cha mwaka mmoja.

Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti, baadhi ya wadau wa siasa mkoani Arusha walisema harakati zinazofanywa na Friends of Lowassa ni dalili ya woga na kutojiamini hasa kukubalika kwa wanayempigani miongoni mwa Watanzania.

Mkazi wa Sakina jijini hapa, Haji Mseleka, alisema kwa Watanzania kulazimishiwa mtu kuwa Rais (kama wanavyofanya Friends of Lowassa) si sahihi na badala yake Watanzania waachwe wachague wenyewe muda ukifika.

"Kufanya kampeni si vibaya, lakini wanazofanya si kampeni bali ni kuwahadaa Watanzania na kuwalazimisha kuchagua chaguo la wachache; lakini ngoja tuone," alisema Msekela.

Hivi karibuni wanodaiwa kuwa ni Masheikh wa mkoa wa mwanza walitoa kauli kumtaka Lowassa kutangaza nia huku pia wakimpa fedha za kuchukulia fomu za kugombea urais mlango utakapofunguliwa rasmi.


Chanzo: Raia Tanzania
 
Hakuna lolote, mbwembwe za washereheshaji.

Raisi hatoki ccm hata kwa tingatinga!. Watanzania tumeshakataa, ila ninyi maigizo fanyeni tu!.
 
Hizi ni hadithi za kutunga! Lowassa alishasema imetosha.
 
hivi mimi nawauliza kipi cha ajabu ambacho lowasa amefanya hapa nchini mpaka kuwe na presha kubwa kiasi hicho.

waswahili wanasema: KIZURI CHAJIUZA KIBAYA CHAJITEMBEZA
 
  • Thanks
Reactions: 999
hivi mimi nawauliza kipi cha ajabu ambacho lowasa amefanya hapa nchini mpaka kuwe na presha kubwa kiasi hicho.

waswahili wanasema: KIZURI CHAJIUZA KIBAYA CHAJITEMBEZA
Nakubaliana na wewe Mkuu. Fedha za fisadi Lowasa zimewalewesha hawa wanaompamba
 
Pesa za mafisadi zinawayumbisha sana.
 
Siku moja Lowasa akiambiwa asitumie pesa atafunga mdomo make hana hoja ya kuzungumza zaidi ya kutumia pesa tu.
 
Naona atatumia siku hiyo kutangaza nia rasmi, lakini kwanini anajifichajificha sana?
 
Watabadili sana style mwaka huu. Magogono kamwe sio pango la wanyang'anyi!!
 
hivi mimi nawauliza kipi cha ajabu ambacho lowasa amefanya hapa nchini mpaka kuwe na presha kubwa kiasi hicho.

waswahili wanasema: KIZURI CHAJIUZA KIBAYA CHAJITEMBEZA
anatoa pesa kwa wapambe
 
Hilo gazeti la Raia Tanzania halina tofauti na udaku special ... Mwacheni Lowassa apumzike! ... Wananchi wanataka huduma yake maana amethibitisha kuwa ni yeye pekee mwenye uwezo wa kumwajibisha yeyote wakati wowote mahala popote kama ameshindwa kudeliver! Lowassa pekee ndo mwenye uwezo wa kuondoa tatizo la ajira hapa nchini, lowassa Pekee ndo mwenye uwezo wa kufuta mikataba ya kishenzi, Lowassa Pekee ndo mwenye uwezo wa kutekeleza miradi mikubwa kama ile ya KASHWASA, UDOM, Shule za kata ... Chini ya Lowassa tatizo la maji safi na salama Dar litakwisha, Miundo mbinu itaboreshwa ili kuzuia mafuriko... Hao wapiga deals wajiandae kukimbia nchi ... Mmemsingizia upuuzi mwingi sana LAKIN Watanzania wa leo si wajinga tena! Wanaona wanajua nani ninani na yupi atawafaa ...
 
KUNDI linalomuunga mkono Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, katika harakati zake za kuingia Ikulu Oktoba, mwaka huu, linalojulikana kama ‘Friends of Lowassa’, limeandaa tukio kubwa la kihistoria wiki hii.

Kwa mujibu wa taarifa za ndani ya kundi hilo zilizolifikia gazeti hili mwishoni mwa wiki, wakati wowote wiki hii, makada wastaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), watakusanyika jijini Arusha kutoa tamko la ‘kumshawishi’ Lowassa kutangaza nia ya kugombea urais.

Katika wiki chache zilizopita, waratibu wa shughuli za kampeni za Lowassa walibadili mbinu za kumshawishi kada huyo mkongwe agombee urais; na sasa badala ya ‘mashabiki’ wao kufunga safari kumfuata aliko, huita vyombo vya habari, hususan TV, na kutangaza kumuunga mkono wakiwa huko huko waliko.

“Sasa hivi mipango inaendelea ili kundi kubwa la Watanzania litakalojumuisha wazee wa kimila wa Kimasai kutoka kila kona ya Arusha, siyo wa Monduli peke yao, pamoja na wenyeviti na makatibu wastaafu wa CCM wa mikoa ya Kanda ya Kaskazini wakusanyike hapa Arusha mjini kumuomba mzee atangaze haraka nia ya kugombea urais.

“Hii ya Arusha si mchezo, maandalizi yake ni makubwa mno kwa kuwa ndipo anapotoka mzee. Tukio hili litakuwa kubwa na baada ya hapo, basi! Hakutakuwa na makundi mengine tena yatakayotoa matamko kumshawishi mzee,” alisema mmoja wa waratibu ndani ya Friends of Lowassa ambaye hatuwezi kumtaja gazetini kwa sababu za wazi kabisa.

Raia Tanzania linafahamu kuwa mipango yote kuhusu kufanyika kwa mkutano huo imekamilika na kwamba tukio hilo awali lilipangwa kufanyika wakati wa Sikukuu ya Pasaka, lakini likaahirishwa kutokana na wadau muhimu kuwa katika shughuli za mazishi ya mfanyabiashara mmoja wa Tanzanite aliyeuawa wiki iliyopita.

Majina ya baadhi ya wazee wa kimila na makada wastaafu wa CCM waliopewa taarifa za mkutano huo tunayo.

“Mbali na makada hao, pia wapo wazee maarufu wa Arusha na wazee kutoka vyama vya upinzani (hakutaja majina). Hii shughuli itakuwa kubwa kuliko zote zilizowahi kufanyika,” alisema mtoa taarifa wetu.

Alisema mkutano huo mkubwa jijini Arusha utatumika pia kuujulisha umma wa Watanzania kwamba ingawa Arusha ni ngome ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Lowassa anakubalika kugombea nafasi ya urais.

Taarifa zaidi zinadai kuwa baada ya mkutano huo, mambo yatasitishwa kusubiri Lowassa atangaze nia yake; na kwamba mbunge huyo wa Monduli anatarajiwa kufanya hivyo ndani ya wiki mbili zijazo.

Mipango ya Lowassa kuweka hadharani nia yake hiyo imekuwa ikiahirishwa kwa zaidi ya mara nne sasa kutokana na sababu mbalimbali za kimkakati, kubwa ikiwa ni Lowassa kuwa katika uangalizi wa Kamati Ndogo ya Maadili ya Kamati Kuu ya CCM kwa kipindi cha mwaka mmoja.

Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti, baadhi ya wadau wa siasa mkoani Arusha walisema harakati zinazofanywa na Friends of Lowassa ni dalili ya woga na kutojiamini hasa kukubalika kwa wanayempigani miongoni mwa Watanzania.

Mkazi wa Sakina jijini hapa, Haji Mseleka, alisema kwa Watanzania kulazimishiwa mtu kuwa Rais (kama wanavyofanya Friends of Lowassa) si sahihi na badala yake Watanzania waachwe wachague wenyewe muda ukifika.

“Kufanya kampeni si vibaya, lakini wanazofanya si kampeni bali ni kuwahadaa Watanzania na kuwalazimisha kuchagua chaguo la wachache; lakini ngoja tuone,” alisema Msekela.

Hivi karibuni wanodaiwa kuwa ni Masheikh wa mkoa wa mwanza walitoa kauli kumtaka Lowassa kutangaza nia huku pia wakimpa fedha za kuchukulia fomu za kugombea urais mlango utakapofunguliwa rasmi.


Chanzo: Raia Tanzania
BREAKING NEWS...

Kutoka ofisi ya mwenyekiti wa shughuli za nje za Bunge,

Napenda kutoa habari mpya kwa MARAFIKI wote wa Edward Ngoyai Lowassa.

Siku iliyosubiriwa kwa miaka imewadia, baada ya makundi mbali mbali kufuata agizo la Mhe rais Jakaya Kikwete alilolitoa siku ya sherehe za chama mkoani Ruvuma, na kumshawishi kwa hali na mali siku ya Mhe Lowassa. Ameshawishika na sasa anawatangazia wana safari ya matumaini wote kwamba,

Siku ya tarehe 16/05/2015. (humanizing) atatangaza nia ya kugombea urais wa awamu ya tano wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Hivyo anawaomba watu wote wenye mapenzi mema na Nchi yao wajitokeze kumuunga mkono pale uwanja wa Shekh Amri Abed Arusha.

Tuwajulisheni WADAU wote wa safari ya matumaini,
Imetoka kwa,
Ndug. Aboubakar Liongo,
Ofisi ya Edward N. Lowassa,
Mwenge, Dar es salaam.
 
Kavae pedi mtoa mada...damu ya hedhi inachuruzika nyuma
 
Chagadema kwa kujifariji kwa akili zenu mna ubavu wa kupambana na ccm
 
Back
Top Bottom