Timu ya Kampeni ya Pinda Mizengo Wasambaza Waraka Makanisani

wadau ni matumaini yangu mpo salama

ni jambo lililo wazi kwamba mbio za urais zimefikia hatua kali sana hata wengine kudiriki kutumia makanisa kwa manufaa yao. Bila kificho timu ya kampeni ya mheshimiwa mizengo pinda (maarufu kama mzee wa kulia lia), wamesambaza waraka katika makanisa kuwa rais ajaye lazima awe ni mkatoliki (kitendo ambacho kimeshangaza watu wengi sana). Mwalimu nyerere katika uhai wake alilikemea jambo hili kwa nguvu zake zote na kwa ukali kabisa naomba kunukuu maneno ya nyerere "siyo sahihi kumchagua mtu kwa sababu ya dini yeka au dhehebu lake na vile vile siyo sahihi kutomchagua mtu kwa sababu ya dini yake au dhehebu lake, akitokea mtu wa namna hiyo hatufai hata kidogo".

waraka huu umeanza kusambazwa katika makanisa ya mikoa ya kaskazini mwa tanzania (mikoa ya kilimanjaro, arusha na manyara), na mimi kama muumini wa kanisa hili nilishangazwa sana jumapili hii iliyopita ya tarehe 26/10/2014, waraka huu uliposomwa kwa mara ya kwanza katika kanisa langu hapa manyara. Waratibu wa huu mkakati ni mdogo wake mkuu wa mkoa wa mwanza ambaye ni padri katika kanisa la katoliki na ni maarufu kwa jina la paroko (jina kamili ni emmanuel ndikilo) wakishirikiana na mpambe mkubwa wa pinda anayeitwa mwalimu m. Shilatu..


Katika hatua nyingine ya kuonyesha hali ya kisiasa ndani ya ccm imekuwa mbaya sana, mheshimiwa mizengo pinda kwa kujiimarisha kifedha amekuwa akiratibu michango mbali mbali kutoka kwa wakurugenzi wa mikoa na wilaya, na mratibu mkuu wa hili jambo ni dr.masaburi akishirikiana na wakurugenzi 5 wakiwa kama timu. Dr. Masaburi kapewa huu uratibu kutokana na nafasi aliyonayo kwenye alat (so unaweza kucconect the dots); nakumbuka hili swala la wakurugenzi kufungua account maalumu kwa ajili ya kampeni za pinda lilishawai kuletwa humu ndani na mdau mmoja ocampo four na kueleza jinsi wakurugenzi wanavyochangisha ela za umma kwa ajili ya kampeni.,jina maarufu ya hiyo account ni "akaunti ya nyau" au "akaunti ya simba"


nb: Jf ni chanzo kizuri cha habari hivyo, tunaomba serikali iiangalie hilo swala la wakurugenzi kuchangishwa fedha
kwa ajili ya kampeni, na ikibidi hatua zichukuliwe, mutambue wananchi wanajua hili jambo na wanapokosa huduma za kijamii kama madawa, maji, chakula nk wanaumia sana sana.

2). Uongozii wa juu wa katoliki tafadhali waraka kama hizo zisisambazwe tena na tena, zitaleta hisia za kidini.

Naomba kuwasilisha

ukipewa walaka usambaze na ukashindwa kusambaza ....:utapigwatu...na mimi na sema wewekama utaki kusikiza walaka utapigwa .maana hakuna namna
 
Mkuu Abunuasi, mimi ni mtafitit huru na nitabaki kuwa mtafitit huru wala usiwe na shaka kabisa
kama kweli kabisa wewe ni mtafiti huru basi fanya kazi kweli zionekane huru. maana kila nikiona uzi wako hapa najua ni wakumpamba lowassa na kuwatukana rivals wake kwenye kuteuliwa na ccm kukimbiza kijiti cha uraisi.
kwa kifupi mpaka sasa hivi huna tofauti yoyote na chaburuma a.k.a mahonda.
 
Mtoa uzi ni mzushi na ni kada, weka waraka hapa na utuambie umesainiwa na nani tarehe ngapi? PINDA anaweza kuwashangaza wengi wasiofuatilia historia ya nchi hii. WEKA WARAKA WENYEWE JF AU FUNGUA HUU MJADALA MWENYEWE
 
Waacheni wakatoliki katika hili, wao wanamipangilio katika kutafuta thamani ya binadamu katika dunia hii na si kuchagua rais awe nani , mmeanza kupakazia watu eti sababu tu ni wakatoliki wanahaki ya kugombea nafasi yoyote kama watatimiza vigezo na si ukatoliki wao. Ukatoloki wa pinda usiwe nongwa kama anautaka urais mwacheni. Aidha ana haki ya kuwa mgombea kama chama chake kitaona anafaa hakuna wa kupinga awe mlutheli, mkatoliki, au mkristo, hata asiye na dini hapa ukatoliki usihusishwe......
 
Wadau ni matumaini yangu mpo salama

Ni jambo lililo wazi kwamba mbio za urais zimefikia hatua kali sana hata wengine kudiriki kutumia makanisa kwa manufaa yao. Bila kificho Timu ya kampeni ya Mheshimiwa Mizengo Pinda (maarufu kama mzee wa kulia lia), wamesambaza waraka katika makanisa kuwa Rais ajaye lazima awe ni mkatoliki (kitendo ambacho kimeshangaza watu wengi sana). Mwalimu Nyerere katika uhai wake alilikemea jambo hili kwa nguvu zake zote na kwa ukali kabisa naomba kunukuu maneno ya Nyerere "Siyo sahihi kumchagua mtu kwa sababu ya dini yeka au dhehebu lake na vile vile siyo sahihi kutomchagua mtu kwa sababu ya dini yake au dhehebu lake, akitokea mtu wa namna hiyo hatufai hata kidogo".

Waraka huu umeanza kusambazwa katika makanisa ya mikoa ya kaskazini mwa Tanzania (Mikoa ya Kilimanjaro, Arusha na Manyara), Na mimi kama muumini wa kanisa hili nilishangazwa sana jumapili hii iliyopita ya tarehe 26/10/2014, waraka huu uliposomwa kwa mara ya kwanza katika kanisa langu hapa Manyara. Waratibu wa huu mkakati ni mdogo wake mkuu wa mkoa wa Mwanza ambaye ni padri katika kanisa la katoliki na ni maarufu kwa jina la Paroko (jina kamili ni Emmanuel Ndikilo) wakishirikiana na mpambe mkubwa wa Pinda anayeitwa Mwalimu M. Shilatu..


Katika hatua nyingine ya kuonyesha hali ya kisiasa ndani ya CCM imekuwa mbaya sana, mheshimiwa Mizengo Pinda kwa kujiimarisha kifedha amekuwa akiratibu michango mbali mbali kutoka kwa wakurugenzi wa mikoa na wilaya, na mratibu mkuu wa hili jambo ni Dr.Masaburi akishirikiana na wakurugenzi 5 wakiwa kama timu. Dr. Masaburi kapewa huu uratibu kutokana na nafasi aliyonayo kwenye ALAT (So unaweza kucconect the dots); Nakumbuka hili swala la wakurugenzi kufungua account maalumu kwa ajili ya kampeni za Pinda lilishawai kuletwa humu ndani na mdau mmoja Ocampo four na kueleza jinsi wakurugenzi wanavyochangisha ela za umma kwa ajili ya kampeni.,jina maarufu ya hiyo account ni "Akaunti ya Nyau" au "Akaunti ya Simba"


NB: JF ni chanzo kizuri cha habari hivyo, tunaomba serikali iiangalie hilo swala la wakurugenzi kuchangishwa fedha
kwa ajili ya kampeni, na ikibidi hatua zichukuliwe, mutambue wananchi wanajua hili jambo na wanapokosa huduma za kijamii kama madawa, maji, chakula nk wanaumia sana sana.

2). Uongozii wa juu wa katoliki tafadhali waraka kama hizo zisisambazwe tena na tena, zitaleta hisia za kidini.

Naomba kuwasilisha

Atakaye mpigia kura Pinda na yeye kapinda.
 
8. Akaunti ya NYAU
Hili jina la akaunti ya Nyau, ni jina geni miongoni mwenu, ila ni akaunti mahususu kwa ajili ya wakurugenzi wa halmashauri kumchangia mzee tajwa hapo juu.. hii akaunti imeanza kazi rasmi mwezi huu wa nane unaweza kujenga picha mpaka mwakani mwezi wa tano hii akaunti itakuwa na kiasi ngapi… Wadau wakubwa katika akaunti hii ni wakurugenzi wa halmashauri na majiji ili kuweza kufanikisha jambo la mkubwa.. kiasi hakijawekwa wazi ila wanaweza kuchangia kuanzia 10ml and above kwa mwezi kwa kila mkurugenzi. So kama wakichangia wakurugenzi 80 tu (80X10 mln =80 million per month), unaleta mchezo wewe watu wanajipanga sio January Makamba kelele kelele tu kwenye facebook na tweeter wakati mkakati sifuri.


January Makamba kwa sasa yeye anajaribu kujenga jina ila yeye ni team Lowassa.
 
kama kweli kabisa wewe ni mtafiti huru basi fanya kazi kweli zionekane huru. maana kila nikiona uzi wako hapa najua ni wakumpamba lowassa na kuwatukana rivals wake kwenye kuteuliwa na ccm kukimbiza kijiti cha uraisi.
kwa kifupi mpaka sasa hivi huna tofauti yoyote na chaburuma a.k.a mahonda.

Huyu naye ni msakaTonge tu hajawahi kufanya utafiti wowote
 
Pinda hafai katika hili Taifa kama mambo yenyewe ndiyo haya huyu jamaa hafai hafai, mkuu huyo Paroko namfahamu ni mpenda ela vibaya sana

Nakubaliana na wewe ndugu yangu. Huyu hafai na ile ya kujiita ntoto wa nkulima ni danganya toto. Hizo tuhuma kazima zifanyiwe kazi na majibu yatolewe haraka upesi.
 
hii tabia ya mwalimu nyerere alikazata huwa naichukulia sawa na akina mama kuwaambia watoto wao "acha hiyo tabia ya kupigana na wenzio, baba yako hataki kabisa kukona unafanya hivo" or "nitamwamia baba yako kama hauendi shule" Watoto hawa siku baba akiwa hayupo hawana cha kuhofia, maana tatizo kwao ni baba kuona na sio tabia hizo mbaya kuwaletea madhara ya kimwili, kiakili, kiuchumi nk.

Wanajamii tujenge hoja kwa nini tatizo kwenda kupiga kampeni makanisani au misikitini, siyo Nyerere alikataza, kafa sasa hawana wa kumuogopa tena ndo maana wanafanya. Kama lengo ni kutisha kwa kutumia jina la nyerere, watanzania wa sasa hawahofii marehemu tena.

Kwanza kuna vijana wengi siku ukisema mwalimu Nyerere, wao picha inakuja ya Mwalimu aliyechoka maisha, kila siku kulalamika kwa wanafunzi kama vile watamuongeza mshahara. Maana hawakuwahi kumuona Nyerere wala kuishi wakati mtu ukiwa mwalimu au police ni sifa kwa jamii, wanakiji wenzako wanakuja kwa ushauri, siku hizi mwalimu anakimbiwa kwa kukopa!
 
==> Hivi kuna watu hawajioni kweli...PINDA ANAWEZA UONGOZI JAMANI..!!? HANA UWEZO AU MVUTO KWA WANANCHI...PIA HANA MAAMUZI...sio kabisa huyo..astaafu akajipumzikie huko..!!!
 
Back
Top Bottom