Time Heist and Time Apocalypse: Jinsi muda unavyoathiri Maisha ya ulimwengu na vilivyomo

Time Heist and Time Apocalypse: Jinsi muda unavyoathiri Maisha ya ulimwengu na vilivyomo

Da'Vinci

JF-Expert Member
Joined
Dec 1, 2016
Posts
36,007
Reaction score
108,554
125281938-travel-through-a-wormhole-through-time-and-space-filled-with-millions-of-stars-and-n...jpg

(Picha ikionyesha Warmhole na Nyota mbalimbali)

Salute Comrades.
Kwa references ya vitabu vya imani za dini mbalimbali zinasema kua hapo zamani Mungu aliumba ulimwengu, akaumba vyote vilivyomo ndani ya siku sita. Upande wa tafiti za kisayansi zinasema kua hapo zamani miaka billion kadhaa iliyopita kulitokea mlipuko mkubwa huko angani ambao wanauita The big Bang, mlipuko huo ulipelekea kutengenezwa kwa sayari na kuleta uhai wa viumbe mbalimbali kwenye sayari hizo (Earth) kupitia Evolution. Mimi ni muamini sio mwanasayansi, hivyo mada yangu itaegemea kwenye imani kwa kiasi Fulani.

Inasemekana Mungu aliumba kila kitu ndani ya siku sita tu na kukabidhi yote aliyoyaumba mikononi mwa mawanadamu (Kiumbe wake pendwa zaidi). Moja kati ya vitu ambavyo vitabu vya imani havielezi kama viliumbwa na Mungu ni MUDA, hakuna sehemu yoyote utakuta wameeleza muda uliumbwa, lakini logically muda uliumbwa.

Fundamental physical quantinty inasema kwamba SI-unit ya muda ni Second, minute,year,months etc. Ili muda uwepo inatakiwa kuwe na solar system, katika soler system sayari zinazunguka jua..zinapozunguka jua tunapata matokeo ya musiku na mchana. Katika usiku na mchana huo ndio tunaweza hesabu sekunde,dakika mwezi au mwaka. Jua ndio linasababisha ruweze kuhesabu muda au tuseme kwamba ndio inafanya existence ya muda. Since jua likizima basi muda utapotea pia uhai wa viumbe vilivyopo kwenye dunia unaweza kuwa extincted/toweka. Jua limepewa dhamana ya kushikilia uhai wa viumbe vilivyopo kwenye sayari hizi (Earth), ndio maana baadhi ya jamii huabudu Jua wakiamini ni Mungu,wengine huenda mbali zaidi wakisema kua hallo ambazo zimechorwa kwenye picha ya yesu ni jua..Hallo ni dura ambalo lipo juu ya kichwa cha picha ya yesu ikimaanisha “Aliye mtakatifu”

Time Apocalypse
Ushajiuliza inakuaje hasa mpaka mtu anakufa?ushajiuliza kwanini wanasema muda utatuambia?au time is a healer? Ipo hivi. Kuna vitu vikuu vitatu ambavyo ndio huleta athari either chanya au hasi katika maisha ya mwanadamu vitu hivyo ni Nature,subconscious mind na Time. Subconcious mind ni shemu kuu ya mind ya mwanadamu ambayo inaratibu taarifa zote zinazohusu mtu husika katika nafsi/soul yake, nature ni mazingira haya tunayaishi, na muda sasa ndio husimama kama hakimu katika kufanikisha mambo yaliyoratibiwa na subconscious mind na mind, hivi vitu vitatu vinafanya kazi simultaneously.

Kwa mfano Moja ya Law of nature ni kua Kila binaadamu lazima afe, so mtu anapokaribia kufa muda ndio huwasiliana na subconscious mind, kisha S mind inaiambia nature kua muda umefika wa mtu huyu kuondoka..nature sasa itakachofanya itachagua aina ya kifo anachotaka muhusika aondoke nacho kutokana na mazingira /hali i/aliyopo. Watu husema muda utatuambia/muda utatupa majibu tuwe na subira kwakua wenyewe ndio hua amua ni wakati gani kitu Fulani kilichoombwa kitokee.

Kuna watu hua wanajiuliza kwamba je unapomuomba Mungu mambi yako yeye huyajibu moja kwa moja au lah? Ukweli upo hivi kuna mambo amabayo Mungu hushughulika moja moja lakini pia yapo mengi sana amabayo huyashughulikia bila yeye kuhusika nayo directly. Mungu alichofanya aliweka kanuni zake amabazo huratibu kila maombi na matakwa yetu yote. Subconscious mind,Nature na Time ndio vitu vinavyoratibu matakwa yetu mengi vikiwa vimewezeshwa na Mungu. Iko hivi unapohitaji kitu mind inakipeleka kitu kile kwa Time, Muda sasa ndio unaamua kitu kile kikufikie kwa wakati gani.

Kwa mantiki hiyo kila kitu kinachotokea maishani mwako ni muda unakua umeamua kitu hicho kikutokee kwa wakti gani. Vile vile kitu pekee ambacho kinafanya kila binaadamu afariki ni muda, muda ndio chanzo cha kifo tukiweza kuudhibiti muda basi tunaweza kudhibiti kifo. Kuna wengine husema kua miaka 1000 duniani ni sawa na siku 1 hapa duniani, hicho kitu ni uongo uliotuka mbinguni hakuna Muda. Muda ili uwepo inatakiwa kuwe kuna sayari zinazunguka jua, mbinguni Mungu hua anawasha taa ikifika usiku kisa giza limeingia?hapana. Kwa Mungu hakuna muda, kama kuna muda basi Mungu atakufa malaika atakufa. In eternal dimension muda haupo ndio maana viumbe walioko huko huwa vile vile maisha yao yote, ndio maana ukifa leo ukafufuka baada ya miaka 50 utajua ulikua umefumba macho nano second kadhaa zilizopita maana kule hakuna muda. Kila kitu kipo Present hakuna future wala past ndio maana vitu vinaishi milele…ndio maana tunaambiwa tutachomeka motobi milele bila kufa maana hakuna muda kule…..So Muda ndio Controller wa hatima ya maisha yetu akiwa amepewa access hiyo na mwenyezi.

Time Heist
Wanasayansi na wanafalsafa wengi kama Einstein,Hawking,Tesla,Newton wamekua wakifanya tafiti juu ya nadharia za muda waone kama wanaweza kwenda beyond a time, wakagundua kwamba muda ni mwendo kasi (Speed) hivyo basi kama wataweza kuwa na speed kubwa basi wanaweza kuutawala Muda. Inasemekana kitu chenye speed zaidi duniani ni mwangu, hivyo kama tukiweza kutengeneza kitu chenye mwendo kasi zaidi ya mwanga tunaweza kuumiliki muda (bending/manipulate). Hapa sasa ndipo linakuja suala la time Traveling

Einstein- Rosen Bridge(warmhole)Hili ni tundu lenye muundo wa kipande cha pipe chenye pande mbili ambazo zinatenganisha muda. Mfano pande/point A inaweza ikawa ipo Tanzania ambayo kwenye point hiyo inaonyesha ni mwaka 2020 halafu pande B inaeza kua Kenya ambapo muda wake unaweza kua ni 2015 au pande hizo zinaweza kua sehemu moja au zikawa na muda unaofanana. Warmholeinaeza kuunganisha vitu vilivyo umbali mrefu kama miaka billion ya mwanga/light years , umbali mfupi au universe moja na nyingine ndani ya muda mfupi tu. Labda unasafiri sehemu yenye umbali wa miaka 500 ndani ya dakika kadhaa, ndio maana ukirudi kule ulikotoka utawakuta wale uliowaacha wamezeeka au wamekufa. Humu kuna masuala mengi ya kisayansi ambayo nikielezea nitawachanganya mliosoma General relativity theory mnaelewa Einstein Field Equation (EFE) mambo ya Gab = KTab Au Cosmological constant Gab + Agab = KTab (tumia Web ndio zitaonekana vizuri)

Kwakua kifo kinasababishwa na muda na muda unaathiriwa na Speed basi ili tukidhibiti kifo inabidi tuuudhibiti muda kwa speed,Hapo ndipo Time travelling inakuja kuchukua nafasi yake. Ili Time traveling (kwenda mbele ya muda au kurudi nyuma ya muda) ikamilike inahitaji chombo cha kusafiria ambacho ni Time Machine. Time machine ili ifanye kazi inabidi kuwe na warmhole, hapo sasa ndio wanasayansi wanaumiza vichwa ni kwa namna gani wataweza kutengeneza Warmhole ili ku-power up time machine.Time traveling inaweza kufanyika spiritually, physically au mentally. Wengi wetu hapa hua tunafanya mental time travelling na baadhi hufanya mental time travel, si ulishawahi kwenda sehemu ukahisi labda hilo eneo ushafika kila tendo linalotendeka unaona kama liliwahi tokea..Hapo unakua ulifanya spiritual time travel bila kujijua roho yako iliwahi kufika bila wewe kujijua, nyie mnaita Dejavu.

Kitu kinachoumiza kichwa ni jinsi gani watafanikisha physical time travelling mtu aweze kwenda zake mwaka 2025 huko akwepe Corona,au arudi 2015 huko. Tukifanikisha timetravellingi itakua ni mwendo wa kukwepa incident zinazopelekea watu kufa..Mtu akifa unaswitch muda unarudi nyuma Yule mtu aliyekufa unamuepusha na ile incident iliyopelekea kufa.

Wanasayansi wengi hasa Stephen Hawking wanasema time travelling haiwezekani, na watu humu JF wanaamini kabisa hua naona wanaongea hivo. Wanasahau kua ubongo wa mwanadamu ni Infinity yaani hauna ukomo, ukomo wa bongo wa mwanadamu upo kwenye baadhi ya vitu Fulani umekua disabled kuweza kungamua vitu hivyo kama Usingizi,maisha mtu akifa,Mungu yupoje na mengineyo. Mwanadamu ana uungu ndani yake kutokana na pumzi aliyowekewa kutoka kwa muumba wake ndio maana anaweza kufanya big invetions kama zote hizi tunazoziona duniani. Kama Stephen hawking alihjaribu akashindwa basi haiamanishi kua Time travelling haiwezekani, yeye hakua mwanadamu pekee na wa mwisho ambao wanaakili kuliko wengine. Ipo siku natumani atatokea giant mwingine katika kufikiria aje approve wrong maneno ya wanasayansi walioshindwa time travelling (Naweza kua hata mimi nikipewa nafasi)

Mimi fikra zanituma kua hichi kitu ni real na inawezekana kuna watu wanafanya hii mambo kwa manufaa yao wenyewe ndio maana mtu anaweza kutabiri vitu tata vitakavyokuja mwaka Fulani, au wanafanya Dark Prophesying? Inawezekana wanasubiri muda watakaoona unafaa waje wailete kwetu nasi tuitumie. Kama tutaweza maana hata 4G tumeshindwa kuimudu ipasavyo.

-Unworthy, Useless
~Da’Vinci
 
Muda utaongea, muda ni hakimu wa haki... ni kweli kabisa ‘muda’ ni kitu kilichoumbwa.

Well, ni sayansi na dini kwa mbaaalii kama ulivyotanabaisha hapo awali.... kwa haraka haraka nimewaza kitu kimoja muhimu naomba kuuliza:

Mungu aliumba ulimwengu na vyote vilivyomo kwa siku sita, akaona vyote ni vema na siku ya Saba akapumzika na kustarehe.

Baada ya uumbaji huo, [au hata kabla ‘ukiweza’] siku ya nane Mungu alifanya nini.?

Ni kwamba tayari siku [muda] zilikuwa ‘scaled’ into weeks au zilikuwa zikihesabiwa kuendelea.?
 
Dhana ya muda ni pana sana.

Binafsi muda nautazama ktk namna ya space jinsi ilivyo kwa maana space is time!.. no space no time.
The way space still the way we are in time!

Kwangu nauelewa muda kuwa hauendi mbele wala haurudi nyuma!

Kinachotokea ni action!,jinsi unavyochukulia reaction kwenye space ndivyo ambavyo unaitumia so hivyo unavyoitumia ku reaction plus kumbukumbu ndio unaona muda una past na future!!

Namaanisha unazaliwa,unakuwa kijana unakuwa wa makamo na baadae mzee.. this is how your body use space to reaction.. and that we call it time.

Hauendi mbele wala haurudi nyuma time remain there..

Muda unaweza kuuelezea kwa concept nyingi mfano kwa kutumia jua na dunia kunavyokuwa usiku,mchana na asubuhi but what if we remove those things..??????

Je,hiyo itamaanisha pia kuwa muda haupo..?

My answer is no! Muda bado ungali upo hata ukitoa vyote hivyo maana space still there and space is time..

Ukitaka kuuzuru muda zuru space.

Nakubaliana na Einstein muda unaweza kuwa affected na gravity pia na speed..

Utata wangu ni sehemu ya kurudi nyuma ya muda..!

Sioni hatua yoyote unayoweza ichukua na ukarudi nyuma ya muda!

Kama ukiweza kurudi mwaka 2015 hii itamaanisha space inakuwa na historia ina record ama inakila taarifa juu ya kinachotokea!!

I mean ni kuwa kila kitu kimeshachorwa sasa ni tunapita tu!!
Hainingii akilini swala la kurudi nyuma ya muda!!

Ila la kwenda mbele ya muda naweza lielezea ktk mantiki hii mfano wa barafu..

Chukulia mfano huu unasamaki ambae ukimuweka ktk mazingira ya kawaida itachukua muda fulani huyo samaki mpaka kuharibika ila ukimuweka kwenye barafu ataweza kukaa kwa muda mwingi zaidi tofauti na akiwa ukawaida.. this is what I call it time travel na naielewa kushinda hizo concept za kusafiri kwa dk mbili na kutua mwaka 2059 huko 😂😂..

Ikiwezekana kumzimisha mtu leo na akaja zinduka miaka Mia ijayo hiyo ndio nitaiita time travel na ninaielewa kwa wepesi zaidi..

Hivyo ndivyo nielewavyo muda.
 
Muda utaongea, muda ni hakimu wa haki... ni kweli kabisa ‘muda’ ni kitu kilichoumbwa.

Well, ni sayansi na dini kwa mbaaalii kama ulivyotanabaisha hapo awali.... kwa haraka haraka nimewaza kitu kimoja muhimu naomba kuuliza:

Mungu aliumba ulimwengu na vyote vilivyomo kwa siku sita, akaona vyote ni vema na siku ya Saba akapumzika na kustarehe.

Baada ya uumbaji huo, [au hata kabla ‘ukiweza’] siku ya nane Mungu alifanya nini.?

Ni kwamba tayari siku [muda] zilikuwa ‘scaled’ into weeks au zilikuwa zikihesabiwa kuendelea.?
Mkuu hayo maneno yanayosema aliumba kwa siku sita ni kutungwa tu ili kuonyesha ukuu wake kwetu jinsi anavyoweza kufanaya mambo makubwa katika muda mdogo kwa mtazamo wa kibinaadamu. Kama kweli Mungu aliumba kwa siku 6 basi kwa hesabu za kidunia itakua aliumba kwa miaka elfu 6 maana kwake siku moja sawa na miaka 1000.

Hivyo Mungu aliumba na hakuhesabu siku, alipomaliza kuumba alipumzika maana aliweka mifumo ambayo inafanya vitu alivyoumba vinajiendesha vyenyewe kwa msaada wake.

Unahisi Mungu bado anaendelea kuumba mtu mmoja mmoja? Jibu ni No.
 
ni maendeleo ya kuishi milele na matukio ambayo hufanyika katika mfululizo dhahiri usiobadilika kutoka zamani, kupitia sasa, hadi siku zijazo
Kuna mitazamo mingi sana kuhusu muda, na mtazamo nilionao kuhusu muda unaweza kuwa tofauti kidogo. binafsi naamini kuwa muda ni kama mstari ambao matukio hutokea. Muda upo, hauna mwanzo na hauna mwisho. Muda upo lakini muda unakuwa na maana zaidi pale ambapo kuna tukio. Lakini ili vyote hivi vionekane kwa binadamu kunahitajika ufahamu (consciousness).
Hivyo mimi ndivyo ninavyouelewa muda.
 
Mkuu hayo maneno yanayosema aliumba kwa siku sita ni kutungwa tu ili kuonyesha ukuu wake kwetu jinsi anavyoweza kufanaya mambo makubwa katika muda mdogo kwa mtazamo wa kibinaadamu. Kama kweli Mungu aliumba kwa siku 6 basi kwa hesabu za kidunia itakua aliumba kwa miaka elfu 6 maana kwake siku moja sawa na miaka 1000.
Hivyo Mungu aliumba na hakuhesabu siku, alipomaliza kuumba alipumzika maana aliweka mifumo ambayo inafanya vitu alivyoumba vinajiendesha vyenyewe kwa msaada wake.
Unahisi Mungu bado anaendelea kuumba mtu mmoja mmoja? Jibu ni No.

Nakubaliana na wewe kuwa hayo ni ‘maneno’ kutungwa kwa lengo maalumu, lakini napingana na hesabu za ‘kidunia’ kuwa siku sita ni miaka elfu sita.... kwa maneno hayo ya kutungwa yalipima muda kwa mzunguko wa dunia kuwa “ikawa jioni ikawa asubuhi siku moja”. Rejea

Lakini kwa habari hizi muda bwana KENZY kahusisha space na time, nilitaka kuhoji kuwa kabla ya uumbaji [hasa wa usiku na mchana] ingawa space ilikuwepo, muda uliweza vipi kuhesabiwa.?
 
KENZY
Mkuu umeongea mengi na mazuri kwenye nadharia yako kuhusu space na time, ila umejipigia mstari hapo mwishoni kuwa ikiwa utaielewa hiyo wanaita sijui ‘astral projections’ basi zitakuwa na ukweli.... huoni kama umejiaminisha kuwa wewe ni kizio cha werevu ya kwamba hadi kitu ukielewe wewe ndo kiwe kweli.?
 
KENZY
Mkuu umeongea mengi na mazuri kwenye nadharia yako kuhusu space na time, ila umejipigia mstari hapo mwishoni kuwa ikiwa utaielewa hiyo wanaita sijui ‘astral projections’ basi zitakuwa na ukweli.... huoni kama umejiaminisha kuwa wewe ni kizio cha werevu ya kwamba hadi kitu ukielewe wewe ndo kiwe kweli.?
Kweli ni ipi..??
Kweli ni ithibati ya kuthibitika.. kitu kinachoweza kuthibitika ni kweli hiyo
Haijalishi nimekielewa au sijakielewa!

Hapo sijazungumzia astral projection ila nachomaanisha ni mfano kama huo wa samaki.. Ni hivi ukiweza simamisha process za mwili zikatulia inamaana mwili ukawa haukui au unakuwa kidogo sana tofauti na inavyotakikana na ukaja kumuamsha mtu huyo (kurudi kwenye process zake) baada ya miaka mia mtu huyo atakuwa ame travel into the future!.. it means kama asingekuwa ktk koma kwa muda huo huenda angekuwa ameshakufa au amezeeka ila alipozimishwa kama alikuwa na miaka mitano na baada ya miaka mia akizinduliwa atakuwa na miaka ileile mitano!! Ndio maana nikaandika muda ni vile process zetu zinavyotumia space ku reaction!
 
Msomaji leo kwenye hii maada ntaandika maana sijaielewa kabisa hafu mbaya zaidi mwandishi kahusisha imani hii haijanikaa akilini ntarudi
 
....this is what I call it time travel na naielewa kushinda hizo concept za kusafiri kwa dk mbili na kutua mwaka 2059 huko ..

Ikiwezekana kumzimisha mtu leo na akaja zinduka miaka Mia ijayo hiyo ndio nitaiita time travel na ninaielewa kwa wepesi zaidi..

Hivyo ndivyo nielewavyo muda.

“This is what I call time travel”.

My concern is just there, maelezo yako yote shaka shida nayo whether nimeelewa au laah.... unaposema ‘I call’ ni kwamba hiyo theory kuhusu ‘time travel’ ni ufahamu wako.?
 
“This is what I call time travel”.

My concern is just there, maelezo yako yote shaka shida nayo whether nimeelewa au laah.... unaposema ‘I call’ ni kwamba hiyo theory kuhusu ‘time travel’ ni ufahamu wako.?
Namaanisha kwangu hilo limekuwa jepesi kulielewa kuandika "I call" hapo nimekazia tu..
Mkuu hayo ma wormhole kidogo kwangu naweza sema zinaniletea utata! Lkn haimaanishi kuwa ni uongo au vipi.. so kila mtu anachokielewa zaidi ndicho anachokipa nafasi zaidi that why I call...
 
Back
Top Bottom