honey bee
Senior Member
- Nov 23, 2021
- 139
- 236
Habari wana jamii forums,
Hivi ulishawahi kupambana na thread za mtu fulani zinazohusu mambo ya kiroho na miujiza!
Mfano:
•kutoka nje ya mwili
•kuondoa hofu kiroho
•kutengeneza ndoto za Lucid
•kumuona mke mtarajiwa kwenye kioo
•kufanya tahajudi
Mchezo wa kufanya jaribio la kutoka nje ya mwili lilisababisha kuamsha nafsi yangu kutoka kitandani kwa kasi zaidi pasipo kutumia nguvu bali kutumia mawazo yangu mimi mwenyewe, ingawaje nilivyopaa kufika mbele kidogo nikageuka nyuma, mwili sikuuona!! Wala ile Silver cord sikuiona pia! Baada ya kuligundua hilo, nilijiona kama mtu ambaye alishakufa zamani, nilijawa hofu sana kufikia hatua ya kushtuka nikiwa kitandani na jasho la kufa mtu!! Hali hiyo iliniharibu saikolojia yangu sana, ilifikia hatua ninawaza kufa tu! Sikutamani kuishi tena!
Mchezo wa kufanya jaribio la kutengeneza ndoto za Lucid ulisababisha kujihisi niko katika ndoto muda wote, hasa hasa nyakati za usiku nilipokuwa nikifikiri jambo, kisha nikazubaa tu, lilitokea! Niliposhtuka lilipotea! Kuna wakati nilipokuwa ninaamka usiku nilikuta baadhi ya vitu ambavyo havikuwepo kabla ya mimi kulala vimeongezwa ama vimepangwa tofauti, mfano foronya langu nililikuta miguuni badala ya kichwani, nilipojaribu kulirudusha, kumbu kumbu ilipotea ghafla na nisielewe nafanya nini! Ndipo niliamua kulala na asubuhi nilipoamka nilikuta vitu viko sawa tu!
Jaribio la kioo, kitana na apple usiku wa manane lilisababisha nikaona kiza kwenye kioo pale tu nilipozubaa!! Ghafla macho yangu kwenye kioo yalionekana mekundu, kisha taswira za ajabu zingeanza kupita kwenye kioo!!
Pindi nilipokuwa kwenye lucid dreaming halisi, nilizifurahia sana, make nilikuwa mtengenezaji wa character ambao nilihitaji kuwaona kwenye huo ulimwengu! Nilifanya chochote ninachojiskia, sikuweza kuona taswira yangu kwenye vioo!!
Ndoto ya mwisho ya lucid kunitokea, niliigundua mapema zaidi, make niliota nimeelekea shule niliyosoma advance kuchukua cheti, ila cheti hicho kilikuwa na picha ya cheti cha form four, nilipokitazama kwa umakini, niliona profile picture yangu ya facebook iko kwenye cheti! Nilipokitazama kwa ukaribu nilikutana na wall paper ya simu yangu iki pale, ndipo nilipotokeza kwenye voluntary mind, nilihisi raha ya ajabu ya kuwa kwenye austral plane kiasi kwamba sikutamani hata kidogo kuamka kutoka usingizini! Nilitamani nilale milele! Ndipo nilipojikuta nafumbua macho! Na Saikolojia yangu iliyokuwa imevurugwa ilirudi kuanzia pale, nikajihisi amani! Nilikuwa nikisumbuliwa na kichwa, kipanda usi! Lakini niliweza kujiambia kichwa pona, nikiwa ndani ya lucid, kichwa kikapona, hata nilipoamka hakikuuma tena!
Na mengi ya kuwaeleza,
Ila tu kama huna kifua cha kumudu mambo hayo, bora uachane nayo, yanawezekana kwa 100% na kila mtu unaweza fanya, ila inahitaji moyo!
Make kipindi naanza kufanya jaribio la kutoka nje ya mwili, kuna muda nilisinzia ingali najielewa! Ila naskia kabisa kuwa nimelala, hata kumeza mate nilishindwa! Niliziskia sauti za majirani wakipiga story japo kwa mbali!
Na hata nilipojaribu kuamka, niliweza kufumbua macho tu, mwili wote ukapigwa ganzi! Ni hatari wakuu!
Ngoja niishie hapa!!
Hivi ulishawahi kupambana na thread za mtu fulani zinazohusu mambo ya kiroho na miujiza!
Mfano:
•kutoka nje ya mwili
•kuondoa hofu kiroho
•kutengeneza ndoto za Lucid
•kumuona mke mtarajiwa kwenye kioo
•kufanya tahajudi
Mchezo wa kufanya jaribio la kutoka nje ya mwili lilisababisha kuamsha nafsi yangu kutoka kitandani kwa kasi zaidi pasipo kutumia nguvu bali kutumia mawazo yangu mimi mwenyewe, ingawaje nilivyopaa kufika mbele kidogo nikageuka nyuma, mwili sikuuona!! Wala ile Silver cord sikuiona pia! Baada ya kuligundua hilo, nilijiona kama mtu ambaye alishakufa zamani, nilijawa hofu sana kufikia hatua ya kushtuka nikiwa kitandani na jasho la kufa mtu!! Hali hiyo iliniharibu saikolojia yangu sana, ilifikia hatua ninawaza kufa tu! Sikutamani kuishi tena!
Mchezo wa kufanya jaribio la kutengeneza ndoto za Lucid ulisababisha kujihisi niko katika ndoto muda wote, hasa hasa nyakati za usiku nilipokuwa nikifikiri jambo, kisha nikazubaa tu, lilitokea! Niliposhtuka lilipotea! Kuna wakati nilipokuwa ninaamka usiku nilikuta baadhi ya vitu ambavyo havikuwepo kabla ya mimi kulala vimeongezwa ama vimepangwa tofauti, mfano foronya langu nililikuta miguuni badala ya kichwani, nilipojaribu kulirudusha, kumbu kumbu ilipotea ghafla na nisielewe nafanya nini! Ndipo niliamua kulala na asubuhi nilipoamka nilikuta vitu viko sawa tu!
Jaribio la kioo, kitana na apple usiku wa manane lilisababisha nikaona kiza kwenye kioo pale tu nilipozubaa!! Ghafla macho yangu kwenye kioo yalionekana mekundu, kisha taswira za ajabu zingeanza kupita kwenye kioo!!
Pindi nilipokuwa kwenye lucid dreaming halisi, nilizifurahia sana, make nilikuwa mtengenezaji wa character ambao nilihitaji kuwaona kwenye huo ulimwengu! Nilifanya chochote ninachojiskia, sikuweza kuona taswira yangu kwenye vioo!!
Ndoto ya mwisho ya lucid kunitokea, niliigundua mapema zaidi, make niliota nimeelekea shule niliyosoma advance kuchukua cheti, ila cheti hicho kilikuwa na picha ya cheti cha form four, nilipokitazama kwa umakini, niliona profile picture yangu ya facebook iko kwenye cheti! Nilipokitazama kwa ukaribu nilikutana na wall paper ya simu yangu iki pale, ndipo nilipotokeza kwenye voluntary mind, nilihisi raha ya ajabu ya kuwa kwenye austral plane kiasi kwamba sikutamani hata kidogo kuamka kutoka usingizini! Nilitamani nilale milele! Ndipo nilipojikuta nafumbua macho! Na Saikolojia yangu iliyokuwa imevurugwa ilirudi kuanzia pale, nikajihisi amani! Nilikuwa nikisumbuliwa na kichwa, kipanda usi! Lakini niliweza kujiambia kichwa pona, nikiwa ndani ya lucid, kichwa kikapona, hata nilipoamka hakikuuma tena!
Na mengi ya kuwaeleza,
Ila tu kama huna kifua cha kumudu mambo hayo, bora uachane nayo, yanawezekana kwa 100% na kila mtu unaweza fanya, ila inahitaji moyo!
Make kipindi naanza kufanya jaribio la kutoka nje ya mwili, kuna muda nilisinzia ingali najielewa! Ila naskia kabisa kuwa nimelala, hata kumeza mate nilishindwa! Niliziskia sauti za majirani wakipiga story japo kwa mbali!
Na hata nilipojaribu kuamka, niliweza kufumbua macho tu, mwili wote ukapigwa ganzi! Ni hatari wakuu!
Ngoja niishie hapa!!
