THRDC NA TLS Walani Mauwaji Na Ukandamizaji huko Tanzania

THRDC NA TLS Walani Mauwaji Na Ukandamizaji huko Tanzania

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
43,037
Reaction score
34,741
1762669812024.png




Muungano wa Shirika la Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania THRDC na Chama cha Wanasheria wa Tanganyika TLS, wamelaani vitendo vya mauaji na ukandamizaji wa raia wasio na hatia vilivyoshuhudiwa wakati wa maandamano ya uchaguzi.

Katika taarifa ya pamoja, mashirika hayo yamevitaka vyombo vya usalama kuheshimu haki za kiraia za kuandamana kwa amani na kushughulikia maandamano kwa weledi mkubwa ili kuzuia ghasia na uharibifu.

Taarifa ya pamoja imeelezea kuwa wakati wa maandamano kulikuwa na vitendo vya mauaji ya raia, ukiukwaji wa haki za binadamu, uharibifu wa mali, kuzimwa kwa mtandao wa Intaneti, ukamataji na vipigo.

Katika mapendekezo yao, mashirika hayo yamezihimiza familia zote ambazo zimepotelewa na jamaa kutoa ripoti kwa mamlaka au mashirika ya utetezi wa haki za binadamu.

Chanzo. DW Kiswahili
 
Back
Top Bottom