The Shocking Information against CHADEMA

The Shocking Information against CHADEMA

Hivi uthibitisho wa ZZK kutumiwa na TISS ccm ndo ule waraka wa siri?mbona mbowe aliukataa mbele ya press conference?
Mnatuchanganya sisi wafuata mkumbo huku,mbona propaganda nyingi?

Aidha hukuwepo kwenye press au hukuelewa...Alichokikataa Mbowe ni ule waraka wa siri za ZZK na si huu wa mpango wa mabadiriko...Lakini naendelea kugundua kwamba hata Kiswahili bado ni lugha ngumu kueleweka...Watu mnajichanganya sana
 
Acha uongo wa kitoto wewe ule waraka wa kutunga kabisa umetungwa na wazee ndani ya cdm ukasambazwa na akina yericko humu jf halafu unasema zitto anaujua alikwambia wapi.

Sawa msemaji wa ZZK!
Naona amegeuka lulu!
Kweli, ukiona shetani anamsifia Mungu.....
 
Na ndiyo sababu kubwa ya hizi juhudi zilizotia fora na za kushangaza sana hata kutaka kufanya maandamano. Walidhani CHADEMA haitaweza kufanya maamuzi mazito ili kukinusuru chama sasa imekula kwao wanatapatapa huku na kule katika juhudi zao za mwisho maana wanajua fika juhudi hizi chafu zikishindwa basi CHADEMA itazidi kujiongezea umaarufu mkubwa sana nchini kuelekea 2015 kama chama ambacho kimeonyesha ukomavu wa hali ya juu wa kutoogopa kuchukua maamuzi maziti kwa manufaa ya chama, viongozi wake na wanachama wake na pia kwa faida ya Tanzania na Watanzania, ukilinganisha na MACCM, "sasa tunalivua gamba"

Hata katika kundi la ng'ombe, mbuzi nao hupatikana. Tatizo ni namna gani watavuka mto huu. On the other hand, move hii ya kumfukuza Zitto na Katila imewachanganya sana CCM na TISS.
 
Kiukweli CCM kwa nguvu ya serikali wameunda mfumo wa kuiua CDM ambao kwa muda uliobaki namna yoyote ya kuvunja huo mfumo utaacha mpasuko utaokidhoofisha.
CDM wapo kwenye kipindi kigumu kuliko wakati wowote.
 
Kuwaondoa elites wa hii nchi inahitaji nguvu kubwa,bora tufanye alichofanya(museveni)bushwar,kwani madudu ni mengi katika hii nchi ni mengi mno,umaskini Wa kutisha huku ubadhilifu aupimiki.Watu wanaweza kuwa vichaa pale ambapo CCM itashinda tena uchaguzi ujao(psychological torture).Watanzania runabidi kufikiria otanativu mbadala ya kuondoa hili zigo lilituibia pesa na kuonga mama zetu kushinda chaguzi.
 
ukiona giza linazidi ujue kunakaribia kucha. cDM jipangeni barabara kuchukua nchi sasa njia ni nyeupe kabisa.
 
Harakati zinaendelea na wananchi wa tz si wajinga wa kupambanua mambo CCM MUST GO TO HELL BEFORE 2015. REST IN HELL CCM.
 
Hivi uthibitisho wa ZZK kutumiwa na TISS ccm ndo ule waraka wa siri?mbona mbowe aliukataa mbele ya press conference?
Mnatuchanganya sisi wafuata mkumbo huku,mbona propaganda nyingi?

Waraka wa siri upo kwenye blog ya Henry Kilewo.....sio huu wa maamuzi!
Usichanganye
 
heading na content haviendani....heading inalenga facts, content inalenga utabiri...
 
Uthibitisho mwingine ni wakati wa uchaguzi mkuu 2015 pale gazet la Mwanahalisi lilipofungiwa kwa miezi 3 baada ya kuchapisha mawasiliano kati ya Zoka wa TISS na Zitto kupitia simu zao za mikononi. HGabari za gazeti hilo lilikuwa la kushtua sana na Zitto alishindwa kueleza 'uswahiba' huo ulikuwa ni wa nini hasa wakati wa kipindi hicho cha uchaguzi.

Tangu hapo binafsi sikumuamini tena Zitto ingawa alikuwa na hero wangu mkubwa -- tangu pale alipofukuzwa Bungeni kutokana na sakata la mkataba wa buzwagi kusainiwa hotelini London.
Siasa siyo fair game kama mlikua hamlijui, zitto aliingia kwenye siasa akiwa mtu wa kawaida tu, leo hii anaukwasi wa kutosha tu nyie mnajua, kaupataje? siasa ndo inalipa kihivyo?, mtu yoyote mwenye akili hawezi kumwamini mwanasiasa kwa asilimia 1oo%, lengo lao la kwanza ni kusaka kura wakipata usaka pesa na sifa, akipata hivyo kinafata kiburi ndo zitto.
tuko watz millioni 44, zitto, zitto inamaana yeye ndo ana akili peke yake? au mmekosa shughuli za kufanya? miji yetu michafu mkajitolee kuzoa taka badala ya kukaa na kujadili mtu mmoja yy nani bana?, cdm wajipange upya maana hata sera zao ss zina utata mkubwa mf. hili la serikali tatu, mnataka kutuvunjia muungano? sidhani kama kupinga kila kitu cha ccm ndo upinzani,tunataka vitu mbadala ili tuweze kufika siyo kusubiri ccm wafanye makosa ili muitishe press conference hizo ni siasa nyepesi, iwe zitto katumwa au ajatumwa cdm nayo inapoteza mwelekeo, haiwezekani chama kiwe lissu, zitto na mnyika, chama gani hicho.
 
natabiri umwagaji wa damu wa hali ya juu katika tanzania 2015! Lakini baada ya hapo wanasiasa wengi watapambana na hukumu huku icc!!!!

ushindwe na ulegee kwa jina la Yesu Kristo. Kama ni damu kumwagika basi hiyo damu itakuwa ni ya kwako. Usitutakie balaa mwanaizaya wewe. Ustutabirie balaa la vita. Hivi unafikiri nini wewe. Kama umekosa la maana bora ungekaa kimya badala ya kutuletea habari za umwagaji damu
 
Hiyo chadema ni parokia mnatapatapa.watz wameshaisoma janja yenu kutaka kupanda mbegu za kibaguzi
wewe ndiyo mbaguzi mkubwa,ina maana CDM hakuna waislam?,sitaki kuamini kwamba wewe unafikiri kwa kutumia kiungo cha kutolea uchafu.
 
Hivi uthibitisho wa ZZK kutumiwa na TISS ccm ndo ule waraka wa siri?mbona mbowe aliukataa mbele ya press conference?
Mnatuchanganya sisi wafuata mkumbo huku,mbona propaganda nyingi?

NINI mwekundu ?. hilo la TISS , WALA HALINA UBISHI, Kuna copy moja ya gazeti la mwanaharisi liliwahi kutoa taarifa za mawasiliano kati ya zzk na JACK ZOKA, NA Pia ROSTAM AZIZ.
 
Hivi uthibitisho wa ZZK kutumiwa na TISS ccm ndo ule waraka wa siri?mbona mbowe aliukataa mbele ya press conference?
Mnatuchanganya sisi wafuata mkumbo huku,mbona propaganda nyingi?

Hii siyo propaganda tafakari

Subject: Fw: kazi nzuri
Date: Sunday, November 17, 2013 20:28
From: " Mwigulu Nchemba " <shimbi85@gmail.com> >
To: “Emmanuel Nchimbi” < nchimbie@yahoo.com >

On Sunday, November 17, 2013 6:15:44 PM, Mwigulu Nchemba <shimbi85@gmail.com> wrote:

sawa boss,,jumatano saa moja imekaa safi kabisa. tuchape kazi. ntakupa update nikitoka kuonana na zzk. mh. Lukuvi namtafuta punde

MN

2013/11/17 Emmanuel Nchimbi < nchimbie@yahoo.com >

bila shaka vijana wamefanya kazi nzuri sana. mapambano yanaendelea, hakuna kulala, hapa sasa tume lote livunjwe na huyo waryoba apumzishwe. mtafute mh. Lukuvi ana mazuri ya kuongea na wewe. kuna mapya pale ufipa, nimeshaongea na mh. zitto na amenipa brifieing .. tukutane jumatano basi jioni ya saa1 pale pale cheer,, Emma

Sent from my ipad

On Sunday, November 17, 2013 5:55:02 PM, Mwigulu Nchemba <shimbi85@gmail.com> wrote:

Naona vijana wametekeleza shuguli vizuri, na cham imewakilishwa vizuri sana. Msangi jembe, sasa tutaipata katiba tunayoitaka hicho kikwazo kikishaondolewa bila shuruti. Alafu upande wa pili (cdm) inabidi tuongeze dau ili shujaa zzk abakie ndani, nasikia kuna mkakati wa kumtoa kwenye kinyang'anyiro. tujitahidi sana sana kumsaidia kujenga mtandao wa ndani apate u wenyekiti. taarifa zaidi za ndani zinasema wkamba wanajaribu kumfukuza kabla ya mwisho wa mwaka, tuendeleze vita hilo lisitokee, naona kundi ndani ya bavicha hasa hiyo mitoto inafanya sana mashambulizi lakini hawataweza. inabidi wadhibitiwe. rockup wiki mbili itawasambaratisha. Tuongeze kasi kwa wajumbe wa kamati kuu. wengi wao ni njaa sana nazani 5mil kila moja inatosha kabisa.wananifata sana kuomba hela ili wasaidie nakutana na ZZK baadae plae pa siku ile, unaweza kufika saa 1 jioni

MN
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom