The Real Hidden World

The Real Hidden World

Nianze kwa kusema nakumbuka nikiwa bado mdogo mdogo, nilikuwa na sifa moja kubwa sana mtaani kwetu ya ubishi.
Hata kama ulete fact za kiwango gani lakini niki-stickkatika msimamo wangu ni hapo hapo hamuwezi kunibandua hata mngekuwa mia.
Lakini kuna jambo moja aliligundua mzee mmoja siji kumsahau katika maisha yangu yote ningali bado mdogo kabisa miaka 8.
Aliniita na kuniambia
""Nikiamua kuwa na maarifa naweza kuwa nayo, nakuambia hivi si kwamba nimekuona unamaarifa bali nimegundua unaweza kujaza maarifa ukitaka, sasa nakupa kazi jifunze ulimwengu uliofichika ulivyo hautapata nafasi ya kubishana na wengine kamwe'''
Mzee nilimuelewa japo kwa ufupi sana, labda kutokana na umri wangu ulivyokuwa na kuambiwa jambo lililokuwa juu ya uwezo wa frikra zangu.
Nikiwa na miaka 14 ndipo mzee aliweza kunipa kitabu kilichokuwa na Tittle Hii
"Comfort That Kills" Nikitabu chenye page 36 tu lakini ndicho kikabadili ukurasa wangu wa maisha na kunipa hamu zaidi ya kuujua ulimwengu uliofichika.
Nilikisoma kwa kufanya mirejeo mingi sana katika kamusi ya kufasiri maneno ya Kiingereza kwenda kiswahili,
kwanza kilikuwa na maneno mengi ya kiingereza cha zamani sana, kilinipa shida kidogo lakini niliweza kukielewa na kufunguliwa ukurasa mpya wa kusoma Maandishi.
Si kwamba sikuwa msomaji toka mwanzo ila nikwamba usomaji wangu uliegemea sana katika kusoma hadithi za nadharia zaidi zilizoandikwa na waandishi mbalimbali mahiri.
Sasa hapo ndipo nikaaznza kuufukunyua ulimwengu uliofichika kwa fujo zote.
Sio katika Upande wa Dini au Historia tu, bali niliweza kuyajua mabo mengi sanakwa muda mfupi.
Na kadri nilivyozidi kusoma ndivyo nilivyozidi kujua na kutambua ya kuwa katika asilimia 100% huenda nimeijaza asilimia 0.001%(Kwa wasomaji wavitabu wananielewa vizuri hapa maana kadri unavyosoma ndivyo unaona hauna kitu na unahitaji kujaza vitu)

Nilikuwa napitia Thread Za mtu mmoja humu(jina kapuni)
Niligundua jambo moja wengi wanaompinga katika thread zake ni wale wanaoangalia muvi na video za youtube juu ya uhalisia wa ulimwengu tunaoishi, lakini hawezi kuwa na mrejesho hata mmoja juu ya maandishi aliyoyasoma.
Huyu jamaa ameandika vitu vingi ambavyo huenda sikujua kama naweza kukutana na mtu kama huyo hapa, lakini ndipo nikajua kumbe JF ina watu wengi sana wa kila namna (Viva JF)
Sijaja Hapa kuueweka hadharani ulimwengu uliofichika ila ukihitaji kuujua unajulikana kabisa, tena kwa urahisi sana.

Labda unaweza ukakosa Mzii mahala pa kuanzia lakini nakupa kidogo jambo moja.
Jaribu kujifunza mambo kama haya hapa.

Kwa watu wa Imani hasa wakristo na waochimba masuala ya tulikotoka,kwanini iko hivi,kwanini iko vile,imekuwaje,ilikuwaje,jaribu kupitia mambo haya.
-Ni vitabu gani vilimeondolewa katika Biblia
Unaisoma Biblia Leo lakini inavitabu zaidi ya vitano havijawekwa humo
Tafuta kwanini havimo, vinafundisha nini, nk

-Ni nani alikuwa mmiliki wa kwanza wa America(Usiniambie wahindi wekundu nabaadhi ya maneno yaliyopo kajifunze ulimwengu uliofichika)

Naomba niishie hapo kwa Leo, lakini nikipata mda mzuri na nafasi nitaweza kuleta hoja mbalimbali juu ya ulimwengu uliofichika kwa kadiri ya jinsi nitakavyokuwa na muda.


Updates Ipo Page 30 Kitabu Chenye Utata (Kina Uwezo Wa Kujua Wakati Wako Ujao)

Upadates Ipo Page Ya 95 Nguvu Za Asili Alizonazo Mwanadamu Kumshinda Mchawi


Upadates Ipo Page Ya 128 Nguvu Za Asili Alizonazo Mwanadamu Kumshinda Mchawi Sehemu Ya Pili Na Mwisho

Unaweza kututhibitishia kwamba hayo uliyoaona au kuyajua kuhusu ulimwengu wa uliofichuka ni ya kweli?
 
[HASHTAG]#mwendelezo[/HASHTAG] The Real Hidden World
Kitabu Chenye Utata (Kina Uwezo Wa Kujua Wakati Wako Ujao)
Habari Zenu Ndugu?
Naamini kila mtu ameweza Kusherekea Vizuri Na tunajiandaa kupokea sherehe zingine za kuukaribisha mwaka mpya Kwa amani kabisa.
Kabla sijaanza kuweze kueleea hiki kitabu cha leo naomba nianze kwa kusema kuna kitu kimoja ni hatari sana katika maisha ya mwanadamu endapo kikiweza kuamshwa.
Hiki kitu kinaitwa Jicho La tatu(Third Eye) kazi ya hili ni kwamba unaweza kuona mambo ambayo hayawezi kuonekana kwa macho ya kawaida(baadhi ya wahenga husema jicho la kisogoni)
Mara nyingi unaweza ukakutana na watu ambao wao ni wanajimu/mtabiri/waganga/manabii(hasa false prophet) na wengine wengi sana.
naweza ukaiba kisha ukaumbuliwa ukapewa dili nzima ulivyoicheza kama ulikuwa unaangaliwa vile na CCTV.
Lakini haina maana kuwa kila mwenye uwezo huo anakuwa anafanyia kazi hilo jicho la tatu la hasha Bali ni kwamba wengine huwa wanatumia nguvu fulani yaweza kuwa ya Mungu au ya kishetani.
Ndio maana waweza kuta mtu anamapepo/mashetani akipandisha anamuongelea mtu fulani mamabo ambayo yeye mwenyewe hakuwepo na inakuwa ni sahihi.
Au wengine ni watu wanaotumiwa na Mungu kwahiyo Mungu anawawezesha kuweza kujua jambo ambalo limefichika.
Sasa uhalisia wa jicho la tatu ni kwamba unafunguliwa mlango wako wewe mwenyewe moja kwa moja wa kuweza kufanya hivyo(Kila mtu anauwezo huo ila ni lazima ile nguvu iweze kuamshwa""Activation"")
Hii ni ile tunaita nguvu ya asili(Super Natural Power) sasa ubaya wake ni huu hii kitu ikifunguliwa haiwezi ikafungwa kamwe hata ukiokoka ni kwamba haiwezi kufungwa kamwe.
Ndio maana ni vigumu sana kwa mchawi kuacha uchawi sababu kuna milango inakuwa imefunguliwa ambayo ni vigumu kufungwa.(Nitaleta somo kwanini mchawi ni vigumu kuacha uchawi hata akiokoka wasomaji wa Biblia wanaelewa fika hili)
Nimeanza kwa utangulizi huu kwa ufupi ili tuweze kuwa sawa juu ya jambo hili ninalokwenda kulieleza hapa usije ukatamani sana kujua mambo yako ya wakati ujao kunamadhara makubwa sana(Omba Mungu akujulishe ila usiforce wewe binafsi kujua)
Kuna mambo mengi sana ya kujifunza ila acha tuanze kidogo kidogo.


Wakati wa zamani miaka ya 1769 Alizaliwa jamaa mmoja Aliyekuwa ni mpiganaji mahili sana huyu jamaa aliitwa NAPOLEON BONAPARTE(unaweza uka-google kumjua zaidi)Alizaliwa nchini Ufaransa japo waazi wake walikua ni watu wa kutoka italia na asili yake inabakia kuwa huko.
Katika mojawapo ya vita ambayo aliweza kushindwa Ilikuwa ni katika mji wa Leipzip(huko ujerumani) ambapo walicha vitu vyao vingi sana huko na mojawapo ya kitu kilichokuwa kimeachwa ilikuwa ni "The Book Of Fate" na hiki ndicho kilikuwa kikimilikiwa na huyu jamaa hata ikapelekea kikaitwa Napoleon Book/Napoleon The Book Of Fate.
Kwa uasili hiki kitabu kilikuwa kinamilikiwa na watu fulani ugirikiambao walikua wakiabudu miungu fulani (Search google oracle in Greece utapata kuelewa mengi sana juu ya watu hawa)sasa hiki kitabu walikuwa wakikitumia katika kutatulia matatizo mbalimbali yaliyokuwa yanawakumba watu na Kilikuwa na nakala si zaidi ya tano japo mpaka sasa kumeweza kuwepo kwa nakili nyingi sana katika lugha tofauti tofauti duniani.
Kipindi Napoleon anashindwa vita ndipo kilipatikana hiki kitabu japo kuna uvumi pia unaonyesha kilianza kupatikana miaka kumi kabla ya hapo.
Nimeanza na Napoleon Bonaparte ili tujue kwanini kiliitwa Napoleon maana aliweza kukitumia kitabu hiki kushinda vita kila mara na vita ya mwisho anapigwa hakuwahi kusimama tena.(Uki-google utajua Mengi)
Sasa twende kwenye pointi
Kwa hapa tanzania naamini zipo nakala nyingi sana japo nikwamba kila aliye na hizi nakala anakuwa ni mtu wa kujificha nayo sana.
Nikiwa na miaka 16 nakumbuka baba aliwahi nipa simulizi ya ndugu yetu mmoja aliyeweza kumsaidia jirani yake kujua nini hatima ya watoto wake waliokuwa wanaumwa.
Alisumbuka sana kuwatibia hata ikampekelekea kumdhorotesha sana kiuchumi, Siku moja huyu ndugu angu akamfuta jirani yake akimwambia anaweza kumsaidia kutambua hatma ya watoto wake.
Jirani alikubali japo hakujua nini ataweza kuambiwa, huyu ndugu alichukua kitabu chake (Napoleon Book) Akafanya hesabu zake kama kilivyokuwa kinamuongoza huku akimuuliza maswali yule jirani.
Mwisho wake akaambiwa huyu mtoto aliye mahututi atakufa hataweza kupona, ilichukua siku moja tu maneno yale yakatimia.
Baada ya mda kidogo ikatokea mtoto mwingine kazidiwa jirani kabla ya kwenda hospital japo hakuwa na uhakika kama ataweza kupata msaada maana hawakuweza kutatua tatizo toka mwanzo, Ikabidi amuulize ena ""Kitabu chako kinasemaje juu ya huyu tena?"
Baada ya mahesabu ya mda kidogo ndipo akaambiwa na huyu yatampata kama yule wa mwanzo, wakiwa njiani akaaga dunia pia,
sasa huyu jirani akabeba panga na kumfuta huyu jamaa akisema ndiye mchawi wake juu ya wanae.
Kwa miaka ile kashfa hii ilikuwa ni mbaya sana maana ingeweza hata kumpelekea mtu kifo, akaamua kuondka na kuhamia eneo jingine.
Sasa nilivutiwa sana juu yakukijua hiki kitabu nikaamua kuomba likizo kwa baba nikamsalimie huyu ndugu yetu(Mimi namwita Babu)
Kwake anamaktaba kubwa sana ya ndani nikiwa huko nilipakanyua karibu maktaba nzima sikuweza kupata hiki kitabu(Lakini kumbe yeye alisha nishitkia akiniona kuna kitu cha ziada nakitafuta)
Hakutaka kuniamsha akaniacha ajue nini hatma yangu kila nikienda maktaba yeye anakaa mahali ambapo yeye angeweza kuniona pasipo mimi kujua.
Wiki iliisha nikiwa nimekosa tumaini na tayari nikaanza kukata tamaa lakini niliogopa kuuliza sababu ya kutokana na maudhui ya kitabu husika.
Siku nikaamua kunyata na kuingia chumbani kwake kupekua.
NIlipekua sana tena sana pasipo kukiona lakini kumbe babu yupo bafuni (Chumba chake self) akiniona mda wote nafanya pilika pilika zangu.
kama baada ya lisaa hivi nikaweza kuvuta sanduku moja la mboa lilikua zito sana kwakweli likiwa limejaa vitabu vingi mno na hapo ndipo nikawa nimevutika na sanduku husika.
Nakumbuka nilikaa juu ya kitanda chake huku nikiwa naangaliana na mlango wa bafu jambo lililofanya anione vema sana nini nilikuwanafanya.
Nilitoa kitabu kimoja baada a kingine na kila kitabu nikikipitiaContent zake
Hamadi macho yalitua moja kwa mojaa juu ya kitabu chenye ukubwa kama tenzi za rohoni(wakristo wanazijua) kikiwa na ujazo wa kadri, niliganda kidogo bila kuelewa nini nafanya huku jasho zikinichuruzika,
Gafla babu akakohoa Sikushitushwa wala sikuogopa akaja hadi kitandani nilipo akaniambia umeisha kiona najua utanisumbua sana na sasa nakichoma moto mbele yako usije nisumbua tena,wakati wote huo sikuongea akakibeba na kwenda kukitia moto.
Akarudi kisha ndipo nikapata kujua uhalisia wa hicho kitabu ninini kwa masimulizi yake.

Nikitabu chenye mwongozo wa nyota na namba Na herufi
KInamaelezo fulani namna ya kukitumia
mfano.
Unaingia katika mtihani unataka kujua utafeli au utafaulu kina kupa majibu kama utafeli au unafaulu
Kama unafeli kuna kanuni tena namna ya kufanya ufaulu kinakupa majibu pia
Lakini nikwamba mwongozo wa hizo namba zinatoa jibu la namba ambalo ndilo ukipeleka katika kitabu tena utajua ile namba inamaana gani.
Kuna maswali hua najiulia mpaka kesho nakosa majibu ni nguvu gani ipo katika hizo namba?
Ni Mambo gani yanasababisha haswa iwe vile?
Sina majibu kabisa, hata kama unakesi unataka kujua ufanye nini ili ushinde kinakupa majibu kama huwezi kushinda kinakupa majibu.
Lakini jambo la ajabu nikuwa ni mwongozo wa namba tu.
Lakini pia ajabu yake kubwa sana ni Hii
Kuna Majira hakipaswi kusomwa kabisa, Na kila mwezi una siku kadhaa hakipaswi kusomwa kabisa
Sasa hapo ndipo pia nashindwa uelewa kwanini kinakuwa hivi.
Lakini ni Mengi sana unaweza ukayajua ukihitaji japo katika mitandao kumejaa nakala nyingi a uongo zinazouzwa.
Nami Naamini Hakiwezi uzwa kwa namna kama hiyo kutokana na jinsi kilivyo.

Huyu babu yangu mimi alikuwa ni Rastafalian kasafiri sana nci za wenzetu huko, na ndiko aiwea kukipata hiki kitabu japo aliniambia alikijua akiwa norway ila alikuja kupewa bure kabisa na mzee mmoja kutoka Egypt.

Kumbuka Sio Lazima Kuamini Mambo kama haya japo wale wanaojua ndio huwa wanajua.
Pia sipo hapa kufanya wewe uamini ninachozungumza (Fukua,Fukua,Tafuta mirejeo Utajua nawe)
Pia Mimi ni Mkristo ndio maana natumia baadhi ya maeneo ukristo maana ndio niujuao japo mada hizi hazihusiani na mambo ya dini.
Kumbuka Ulimwengu Uliofichika ni sawa na Propaganda tu Mara nyingi ukweli unakuwa hauonekani ila uhalisia upo wazi kabisa.
Nasisitia tena Sio Lazima wala silazimishi mtu kufuata jambo kama hili
Ila wanaohitaji kujua karibuni sana kujifunza.

Next Mada Itakuwa Kwanini Mchawi Ni Vigumu kuacha Uchawi hata akiokoka?

Kaka naona mambo madogo sana umeyapa hadhi isiyo stahili.

Mada nzima ni Uchawi,na kitu ulichokosea ni kutokujua asili ya hiyo elimu uliyoisoma humo na kujua ni elimu gani.

Hili swali nakuachia au naweza kukupa ziada,babu yako achilia mbali alikichoma kitabu hicho,lakini ukweli Uchawi huwa unateketezwa kwa moto yaani kuchomwa.

Elimu ya nyota yaani unajimu,kiistilahi ya kielimu ni Falaki/Falaqi hizi ni elimu za kishirikina zenye kupata msaada wa karibu wa shetani na si vinginevyo. Hukumu ya elimu hii haipaswi mtu yeyote kujifunza kwani ni mtihani kwa mwanadamu na madhara yake ni makubwa sana hasa kwako mwenyewe mfanyaji au mwenye kujifunza elimu hiyo.

Umezungumzia suala la yule nduguyo aliyefatwa na jirani na kuulizwa kuhusu hatima ya wawili,jambo liko wazi hata bila ya kuwa na kitabu hicho,na kuna yale unayotakiwa kuyanya wagonjwa wakiwa katika hali hizo.

Lakini,je unaweza kutuhakikishia ya kuwa je ni kwa kiasi gani tusimtuhumu ndugu yako juu ya kuhusika na vifa vya hao ndugu wawili,kwa yeye kujihusisha na elimu ya uchawi ?

Hitimisho juu ya kitabu hicho.

Je unaweza kuniambia muandishi wa kitabu hicho na mwaka alio kiandika kitabu hicho yaani kutoka kwa mara ya kwanza na kuanza kutumika ?

Nipo ....
 
Kaka naona mambo madogo sana umeyapa hadhi isiyo stahili.

Mada nzima ni Uchawi,na kitu ulichokosea ni kutokujua asili ya hiyo elimu uliyoisoma humo na kujua ni elimu gani.

Hili swali nakuachia au naweza kukupa ziada,babu yako achilia mbali alikichoma kitabu hicho,lakini ukweli Uchawi huwa unateketezwa kwa moto yaani kuchomwa.

Elimu ya nyota yaani unajimu,kiistilahi ya kielimu ni Falaki/Falaqi hizi ni elimu za kishirikina zenye kupata msaada wa karibu wa shetani na si vinginevyo. Hukumu ya elimu hii haipaswi mtu yeyote kujifunza kwani ni mtihani kwa mwanadamu na madhara yake ni makubwa sana hasa kwako mwenyewe mfanyaji au mwenye kujifunza elimu hiyo.

Umezungumzia suala la yule nduguyo aliyefatwa na jirani na kuulizwa kuhusu hatima ya wawili,jambo liko wazi hata bila ya kuwa na kitabu hicho,na kuna yale unayotakiwa kuyanya wagonjwa wakiwa katika hali hizo.

Lakini,je unaweza kutuhakikishia ya kuwa je ni kwa kiasi gani tusimtuhumu ndugu yako juu ya kuhusika na vifa vya hao ndugu wawili,kwa yeye kujihusisha na elimu ya uchawi ?

Hitimisho juu ya kitabu hicho.

Je unaweza kuniambia muandishi wa kitabu hicho na mwaka alio kiandika kitabu hicho yaani kutoka kwa mara ya kwanza na kuanza kutumika ?

Nipo ....


Umenena vyema mkuu ni uchawi totaly sikupingi ulichokiongea,
Ila naomba nikurudishe tena urudie kusoma, utakaposoma mara hii jaribu kuzingatia pande mbili zote nilizozieleza,
Jaribu kuangalia upande wapili niliouandika japo haujauzingatia soma kama haujui kitu utaelewa nini namaanisha, ukisha maliza kusoma rejesha maarifa yako tena.

Pia mkuu jifunze Kwa mfano huu
Sio wote wanaofanya kazi katika kiwanda cha bia ni walevi,
Sio wote wanaolima tumbaku basi huvuta sigara,
Sio kila wanaosoma hukichukua kile walichosoma,

Kwahiyo unapojaribu kuzungumzia baadhi ya hoja zingatia ya kujua kazi za matamshi yaliyotumika katika uandishi ili kujiepusha kumpa mtu uhusika ambao hana,
Unauelewa mzuri ila huwa unaharakisha kuelewa jambo badala ya kutulia na kutafakari,
Hizi post wamesoma wengi sana lakini wengine wameacha kama yalivyo na wala hajawasumbua.

Pia ukiangalia hicho kitabu unachohitaji kujua mwandishi na mwaka kiliotolewa iko hivi,
Sio kila kitabu huwekwa kwa ajili ya kuuzwa na kusomwa na kila mtu,
labda nikupe ukweli kidogo kuhusu hicho kitabu
Ukigoogle namna ya kukisoma mtandaoni huwezio kupata ukweli hata siku moja, wala hautakuja kupata mtu mwenye maelezo sahihi namna ya kusoma,
Watu wamekuja inbox wanataka kujifunza kujua kukisoma nimewapa athari zake kwanza na nimewaambia mimi sijawahi kujaribu kusoma hata siku moja wala sihitaji nikisome.

Pia kilipoandikwa ilikuwa ni kama diary ambayo ilitumika kwa miaka mingi sana kabla hawajaanza kufanya copy so usiwe unakariri mkuu jaribu kuwa mtu wa hoja za kujifunza sio za ujuaji
 
Unaweza kututhibitishia kwamba hayo uliyoaona au kuyajua kuhusu ulimwengu wa uliofichuka ni ya kweli ?
Laiti kama ungelielewa hoja nilizoziandika basi usingeliuliza swali kama hili
 
Pia mkuu jifunze Kwa mfano huu
Sio wote wanaofanya kazi katika kiwanda cha bia ni walevi,
Sio wote wanaolima tumbaku basi huvuta sigara,
Sio kila wanaosoma hukichukua kile walichosoma,

Huu mfano hapa umeubabatiza,mim siongelei hali hiyo,bali mimi nina ongelea kufanya. Hapa nakujuza sio kila elimu unapaswa kujifunza,kwani kuna elimu kujifunza kwake tu ni makosa na kuifanyia kazi ni kosa zaidi.

Mizani ya ukweli wa mambo iko hivi,tukianza kumtafuta mbaya tuna anzia nani wa kwanza katika kusababisha kisha tunakuja kwenye matokeo. Mizani ya haki hata watengeneza pombe na wassinywe wanaingia katika makosa ya kushiriki katika kudhoofisha afya ya akili ya wale wakusudiwa katika pombe hiyo,na mfano huu unaingia katika tumbaku vile vile. Huu sasa ndio ule upande wa pili wa elimu iliyosahaulika.

Bado mfano wako haujakidhi haja ya kudhoofisha hoja yangu.

Naendelea ....
 
Umenena vyema mkuu ni uchawi totaly sikupingi ulichokiongea,
Ila naomba nikurudishe tena urudie kusoma, utakaposoma mara hii jaribu kuzingatia pande mbili zote nilizozieleza,
Jaribu kuangalia upande wapili niliouandika japo haujauzingatia soma kama haujui kitu utaelewa nini namaanisha, ukisha maliza kusoma rejesha maarifa yako tena.

Pia mkuu jifunze Kwa mfano huu
Sio wote wanaofanya kazi katika kiwanda cha bia ni walevi,
Sio wote wanaolima tumbaku basi huvuta sigara,
Sio kila wanaosoma hukichukua kile walichosoma,

Kwahiyo unapojaribu kuzungumzia baadhi ya hoja zingatia ya kujua kazi za matamshi yaliyotumika katika uandishi ili kujiepusha kumpa mtu uhusika ambao hana,
Unauelewa mzuri ila huwa unaharakisha kuelewa jambo badala ya kutulia na kutafakari,
Hizi post wamesoma wengi sana lakini wengine wameacha kama yalivyo na wala hajawasumbua.

Pia ukiangalia hicho kitabu unachohitaji kujua mwandishi na mwaka kiliotolewa iko hivi,
Sio kila kitabu huwekwa kwa ajili ya kuuzwa na kusomwa na kila mtu,
labda nikupe ukweli kidogo kuhusu hicho kitabu
Ukigoogle namna ya kukisoma mtandaoni huwezio kupata ukweli hata siku moja, wala hautakuja kupata mtu mwenye maelezo sahihi namna ya kusoma,
Watu wamekuja inbox wanataka kujifunza kujua kukisoma nimewapa athari zake kwanza na nimewaambia mimi sijawahi kujaribu kusoma hata siku moja wala sihitaji nikisome.

Pia kilipoandikwa ilikuwa ni kama diary ambayo ilitumika kwa miaka mingi sana kabla hawajaanza kufanya copy so usiwe unakariri mkuu jaribu kuwa mtu wa hoja za kujifunza sio za ujuaji

Hapa nakupa akiba ya hili swali. Ushawahi kujifunza historia ya UCHAWI ?

Narudi kuendelea kujibu hoja yako ......
 
Hapa nakupa akiba ya hili swali. Ushawahi kujifunza historia ya UCHAWI ?

Narudi kuendelea kujibu hoja yako ......
Sio kujifunza nimesoma historia ya uchawi na makala mbalimbali za uchawi na hata vitabu mbalimbali
 
Huu mfano hapa umeubabatiza,mim siongelei hali hiyo,bali mimi nina ongelea kufanya. Hapa nakujuza sio kila elimu unapaswa kujifunza,kwani kuna elimu kujifunza kwake tu ni makosa na kuifanyia kazi ni kosa zaidi.

Mizani ya ukweli wa mambo iko hivi,tukianza kumtafuta mbaya tuna anzia nani wa kwanza katika kusababisha kisha tunakuja kwenye matokeo. Mizani ya haki hata watengeneza pombe na wassinywe wanaingia katika makosa ya kushiriki katika kudhoofisha afya ya akili ya wale wakusudiwa katika pombe hiyo,na mfano huu unaingia katika tumbaku vile vile. Huu sasa ndio ule upande wa pili wa elimu iliyosahaulika.

Bado mfano wako haujakidhi haja ya kudhoofisha hoja yangu.

Naendelea ....
Kujifunza sio kosa kosa ni kutenda jambo lililokinyume na misingi ya taratibu zinazotuzunguka
 
Kujifunza sio kosa kosa ni kutenda jambo lililokinyume na misingi ya taratibu zinazotuzunguka

Hapa ndipo tunapotofautiana mimi na wewe,na huu unaweza kuwa mjadala pweke au mada yenye kujitegemea.

Unaweza kuniambia au kunipa faida ya kujifunza UCHAWI ?

Ni ipi mizani yako juu ya kujifunza jambo au elimu ? Yaani kwako wewe ili jambo uweze kujifunza lazima liwe na sifa gani ? Ni upi uhhsiano kati ya faida,madhara na kujifunza elimu husika ?

Kwa mfano mimi kwangu mimi ni makosa kujifunza Uchawi,Falsafa,Elimu ya Nyota(Falaki),Muziki,Mantiki (Logic),je unaweza kunipa hoja za ulazima wa kujifunza elimu hizo nilizo zitaja ?
 
Hapa ndipo tunapotofautiana mimi na wewe,na huu unaweza kuwa mjadala pweke au mada yenye kujitegemea.

Unaweza kuniambia au kunipa faida ya kujifunza UCHAWI ?

Ni ipi mizani yako juu ya kujifunza jambo au elimu ? Yaani kwako wewe ili jambo uweze kujifunza lazima liwe na sifa gani ? Ni upi uhhsiano kati ya faida,madhara na kujifunza elimu husika ?

Kwa mfano mimi kwangu mimi ni makosa kujifunza Uchawi,Falsafa,Elimu ya Nyota(Falaki),Muziki,Mantiki (Logic),je unaweza kunipa hoja za ulazima wa kujifunza elimu hizo nilizo zitaja ?

Unaweza kuniambia au kunipa faida ya kujifunza UCHAWI ?


MKUU UNAUELEWA MKUBWA ILA SIJUI UNAFELI WAPI NIKUPE FAIDA ZA KUJIFUNZA UCHAWI KWANI MIMI NI MCHAWI?
AU UMESIKIA MIMI NAFUNDISHA UCHAWI?
TAFUTA MWALIMU WA UCHAWI KISHA MUULIZE MASWALI HAYO

NA NIMEKUAMBIA SIJAJIFUNZA UCHAWI ILA NIMESOMA MAKALA MBALIMBALI ZA UCHAWI HEBU TOFAUTISHA BASI MWANAFUNZI NA MSOMAJI


HAYA SWALI LAKO LA PILI
Ni ipi mizani yako juu ya kujifunza jambo au elimu ? Yaani kwako wewe ili jambo uweze kujifunza lazima liwe na sifa gani ? Ni upi uhhsiano kati ya faida,madhara na kujifunza elimu husika ?

MIZANI YANGU YA KUJIFUNZA JAMBO HUANZIA KATIKA SWALI KWANINI? BAADA YA HAPO NAANZA KUTAFUTA MAJIBU NINAPOANZA KUTAFUTA MAJIBU TAYARI NAKUWA NIMEJUA HILI JAMBO LAFAA KWA MAARIFA KWANGU NDIO MAANA NAENDELEA KULITAFUTIA MAJIBU.
PIA ILI JAMBO NIWEZE KUJIFUNZA NI LAZIMA LIWE LIPO KATIKA NJIA YA MISINGI NINAYOITUMIA (UNAWEZA USIELEWE SABABU NI KITU BINAFSI)
UHUSIANO WA FAIDA NA HASARA NI KWAMBA HUWA NAGUNDUA NAPATA HASARA NILIPOKUWA SILIJUI LILE JAMBO, NDIO NATAFUTA MAJIBU YAKE ILI NIANZE KUPATA FAIDA ZAKE


HAYA SWALI LAKO LA TATU
Kwa mfano mimi kwangu mimi ni makosa kujifunza Uchawi,Falsafa,Elimu ya Nyota(Falaki),Muziki,Mantiki (Logic),je unaweza kunipa hoja za ulazima wa kujifunza elimu hizo nilizo zitaja ?

SIWEZI NIKAKUAMBIA NI MAKOSA AU SIO MAKOSA KWASABABU NI JAMBO LAKO BINAFSI ILA NAWEZA KUSEMA KABLA HAUJAJIFUNZA JARIBU KUELEWA KWANZA KWA UNDANI NI NINI UNAHITAJI UJIFUNZE
KWAHIYO ULAZIMA WA KUJIFUNZA UNATOKANA NA SHAUKU YAKO BINAFSI WALA SIO MTAZAMO WANGU.

NB:ITIKA WITO KATAA NENO
 
MKUU UNAUELEWA MKUBWA ILA SIJUI UNAFELI WAPI NIKUPE FAIDA ZA KUJIFUNZA UCHAWI KWANI MIMI NI MCHAWI?
AU UMESIKIA MIMI NAFUNDISHA UCHAWI?
TAFUTA MWALIMU WA UCHAWI KISHA MUULIZE MASWALI HAYO

NA NIMEKUAMBIA SIJAJIFUNZA UCHAWI ILA NIMESOMA MAKALA MBALIMBALI ZA UCHAWI HEBU TOFAUTISHA BASI MWANAFUNZI NA MSOMAJI


HAYA SWALI LAKO LA PILI
Ni ipi mizani yako juu ya kujifunza jambo au elimu ? Yaani kwako wewe ili jambo uweze kujifunza lazima liwe na sifa gani ? Ni upi uhhsiano kati ya faida,madhara na kujifunza elimu husika ?

MIZANI YANGU YA KUJIFUNZA JAMBO HUANZIA KATIKA SWALI KWANINI? BAADA YA HAPO NAANZA KUTAFUTA MAJIBU NINAPOANZA KUTAFUTA MAJIBU TAYARI NAKUWA NIMEJUA HILI JAMBO LAFAA KWA MAARIFA KWANGU NDIO MAANA NAENDELEA KULITAFUTIA MAJIBU.
PIA ILI JAMBO NIWEZE KUJIFUNZA NI LAZIMA LIWE LIPO KATIKA NJIA YA MISINGI NINAYOITUMIA (UNAWEZA USIELEWE SABABU NI KITU BINAFSI)
UHUSIANO WA FAIDA NA HASARA NI KWAMBA HUWA NAGUNDUA NAPATA HASARA NILIPOKUWA SILIJUI LILE JAMBO, NDIO NATAFUTA MAJIBU YAKE ILI NIANZE KUPATA FAIDA ZAKE


HAYA SWALI LAKO LA TATU
Kwa mfano mimi kwangu mimi ni makosa kujifunza Uchawi,Falsafa,Elimu ya Nyota(Falaki),Muziki,Mantiki (Logic),je unaweza kunipa hoja za ulazima wa kujifunza elimu hizo nilizo zitaja ?

SIWEZI NIKAKUAMBIA NI MAKOSA AU SIO MAKOSA KWASABABU NI JAMBO LAKO BINAFSI ILA NAWEZA KUSEMA KABLA HAUJAJIFUNZA JARIBU KUELEWA KWANZA KWA UNDANI NI NINI UNAHITAJI UJIFUNZE
KWAHIYO ULAZIMA WA KUJIFUNZA UNATOKANA NA SHAUKU YAKO BINAFSI WALA SIO MTAZAMO WANGU.

NB:ITIKA WITO KATAA NENO

Hapa nakujibu kwa kauli fupi sana,hujawahi kusikia mtu akisema, "Nimesoma kitabu hiki nimejifunza mambo mengi sana"

Niliona tangu mwanzo kwamba tamko "Kujifunza" unalieelwa kwa uchache sana,yaani lina kutatiza,hulipi haki yake.

Naimani hapa umenielewa.
 
Hapa nakujibu kwa kauli fupi sana,hujawahi kusikia mtu akisema, "Nimesoma kitabu hiki nimejifunza mambo mengi sana"

Niliona tangu mwanzo kwamba tamko "Kujifunza" unalieelwa kwa uchache sana,yaani lina kutatiza,hulipi haki yake.

Naimani hapa umenielewa.
Nakurudishia kauli fupi Sana
Sio kila tunachosoma tunajifunza
 
Jana niliipitia sana hii thread na nikajikuta na kuwa interested to know more. Baadae nikaingia chimbo kutafuta kitabu cha “Napoleon book of fate” luckily nikakipata. Baada ya kukisoma kidogo nikajua namna ya kufanya nacho kazi na nikajianzia mimi mwenyewe ili nione namna kinavyofanya kazi. Majibu niliyoyapata yanebifanya niamini kwa zaidi ya 80%. Sasa tatizo sitakiwi kuuliza swali linalonihusu mwenyewe zaidi ya moja kwa siku.

Anayehisi anataka kujua issue yako anaweza kuniuliza nikamuangalizia ili kuthibitisha nilichothibitisha mimi.

Naendelea kutaka kujua zaidi kuhusu ulimwengu uliojificha


Sent using JamiiForums For iPhone App
 
Jana niliipitia sana hii thread na nikajikuta na kuwa interested to know more. Baadae nikaingia chimbo kutafuta kitabu cha “Napoleon book of fate” luckily nikakipata. Baada ya kukisoma kidogo nikajua namna ya kufanya nacho kazi na nikajianzia mimi mwenyewe ili nione namna kinavyofanya kazi. Majibu niliyoyapata yanebifanya niamini kwa zaidi ya 80%. Sasa tatizo sitakiwi kuuliza swali linalonihusu mwenyewe zaidi ya moja kwa siku.

Anayehisi anataka kujua issue yako anaweza kuniuliza nikamuangalizia ili kuthibitisha nilichothibitisha mimi.

Naendelea kutaka kujua zaidi kuhusu ulimwengu uliojificha


Sent using JamiiForums For iPhone App
Nielekeze Mkuu how inakitumia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
There are only two sources of spiritual power: God and Satan. Satan has only the power that God allows him to have, but it is considerable (Job 1:12; 2 Corinthians 4:4; Revelation 20:2). To seek spirituality, knowledge, or power apart from God is idolatry, closely related to witchcraft. First Samuel 15:23 says, “For rebellion is as the sin of witchcraft, and stubbornness is as iniquity and idolatry.” Witchcraft is Satan’s realm, and he excels in counterfeiting what God does. When Moses performed miracles before Pharaoh, the magicians did the same things through demonic power (Exodus 8:7). At the heart of witchcraft is the desire to know the future and control events that are not ours to control. Those abilities belong only to the Lord. This desire has its roots in Satan’s first temptation to Eve: “You can be like God” (Genesis 3:5).

Since the Garden of Eden, Satan’s major focus has been to divert human hearts away from worship of the true God (Genesis 3:1). He entices humans with the suggestions of power, self-realization, and spiritual enlightenment apart from submission to the Lord God. Witchcraft is merely another branch of that enticement. To become involved in witchcraft in any way is to enter Satan’s realm. Seemingly “harmless” modern entanglements with witchcraft can include horoscopes, Ouija boards, Eastern meditation rituals, and some video and role-playing games. Any practice that dabbles in a power source other than the Lord Jesus Christ is witchcraft. Revelation 22:15 includes witches in a list of those who will not inherit eternal life: “Outside are the dogs, those who practice magic arts, the sexually immoral, the murderers, the idolaters and everyone who loves and practices falsehood.”
No there is only one source of spiritual power and its GOD. But with two big qualities the Goods and Bads depending subject ommision action and object senses receiver buts all starts as equal and ends as one. Alpha and Omega.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimefuatilia thread zako, wewe ni mdadisi na unataka kujua, tunafanana kasoro wewe ni mwoga na hutaki achia ulichokwisha kukiamini. Imani ni jambo la msingi sana, huwezi fanikisha safari yako kama huamini njia uichukuayo ni sahahi kwa asilimia zote. Lakini pia kunaathali kubwa ya kuamini utafika kama hujaanza tembea kuelekea unakopaswa kuelekea, ni sawa na waumini fulani waliokuwa pale Airport wakifanya maombie wakiamini maombi yatawapeleka Ulaya.

Binadamu hakuzaliwa hapa pasipo sababu, kuna sababu, jaribu kumchunguza mtoto mchanga anavyojaribu kukuza fahamu zake, kujiwezesha, kujifunza na jiulize ile effort imeishia wapi?

**** nitaendelea ****
I don't even try to do it.
Kupitia maombi unaweza kujua mambo mengi(nafanya hivyo kutokana mimi ni Mkristo)
So najua ni mpaka pale Mungu anapoamua kunijulisha jambo nami ndipo najifunza.
lakini tofauti na hapo ni kwamba mtu anaingia katika uchawi na mambo ya kishirikina.
Siku nitaleta juu ya mtu ambaye nimefanikiwa hata kukutana na watu wake wakaribu ambaye alifanya hiyo kitu.
When you open it there is no way to close it

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom