-Kwanza CHADEMA hakitaki marekebisho ya katiba
Halafu mkuu huu ujasiri wa kusema uongo hadharani huoni aibu?Ghana na Nigeria zilipopata katiba mpya vigezo vyako vilitimia?Maana umesema haijawai kutokea Duniani na pia majority Bungeni ndiyo determinant factor ya kupata katiba Mpya
-Mzee Mtei na waasisi wa chama waliposajili chama walishinikiza mabadiliko ya katiba lakini marekebisho ya katiba yakafanyika
-Nimeshangazwa na msomi mkubwa kama wewe unayetoa ushauri wa chama kuiba kura kwenye uchaguzi badala ya kusimamia demokrasia na nidhamu kwa kanuni tulizojowekea.Ndio silaha pekee ya chama chako katika siasa za nchi hii?
Ukiminya demokrasia kwa kuiba kura ndani ya chama chako ni kitu gani kitakachozuia kuchakachua kura katika siasa na chaguzi za kitaifa?Ndio mbinu kali za kujenga demokrasia ya kisasa ndani ya taifa linalo-aspire kuwa taifa kubwa?
-Inashangaza pia unapotoa mawazo kuwa eti CHADEMA kiache kuchukua maamuzi eti kwa kuhofia mtu au kiwango cha usomi.Hayo yanafaa kwa chama chako bro na ndiyo maana CHADEMA hatufanani na CCM
Umesahau siku chache zilizopita ulikua ukilalama huku kuwa ni kwanini chama chako hakimchukulii hatua Lowassa na kutoa ushauri kuwa JK afanye kama Clinton kwa yule kigogo wa Marekani ambapo alipindisha sheria na kumfunga?Sasa CHADEMA hakiwezi kuhofia na kufikia huko kilipofikia chama chenu
Kama ni usomi nchi hii wapo wasomi wengi.Hakuna bifu lolote la vijana wala wasomi.
Wasomi wameunga mkono msimamo wa kamati kuu.Ukiona msomi anayesimama na mtu badala ya misinhi ya kitaasisi na principles ujue huyo sio msomi maana hata Maprofesa wanaweza kuwa so naive ndio maana hata nikiwa shule mara nyingi nikigundua baadhi ya wahadhiri wababaishaji kwenye nondo nilikua na-walk out.Misimamo na hoka nzito ndizo zinazoweza kulisaidia taifa letu
-Pia nikukumbushe kitu.Neno Timming kwenye siasa unalitumia na kulitafsiri vibaya.Kuna vitu ambavyo chama makini cha siasa hakiwezi ku-compromise.Utovu wa nidhamu na usaliti
Uoga ndio uliozalisha vyama vya kihuni hadi leo hii tuna serikali ya kihunihuni tu.Hatuwezi kujenga taifa lenye maadili au serikali yenye nidhamu kwa mawazo haya ya kuvizia
Kamati kuu ya CHADEMA imesimamia nidhamu na kufanya uamuzi Full Stop!
Kiulize chama chako kilichoshindwa mradi wa kujivua gamba.Walioanzisha CCJ wapo ndani ya chama.Ukiandaa mazingira ya kusaliti chama unaandaa mazingira ya kusaliti serikali na taifa kwa ujumla.Leo tunajadili EPA,MEREMETA ambazo zilipata fursa kwa sababu ya nguvu ya the so called vigogo na wasomi wakubwa wakati huo AG akiwa msomi mkubwa wa Sheria kutoka Harvard.
Leo unalaumu CHADEMA kuchukua hatua dhidi ya wasomi ambao ni watovu wa nidhamu waliokiri na kujikosha kuomba waruhusiwe kujiuzulu?
Dude,Please!