China si mfano mzuri wa kufuatwa hasa na nchi zetu za kiafrika!!!
Mkuu Y,
Hao wa-China, wanapiga risasi hadharani viongozi wezi, huo ni mfano wa kuigwa mkuu, can you imagine Karamagi, akuwekwa shaba pale monument kwa mkataba wake mbuzi, unafikiri viongozi wetu wataiba tena? Subutu!,
Binafsi sizimii sana na wa-China, maana ninajua kuwa wao ni wahuni mno kuliko wazungu, lakini angalau wao wanajua kula na kipofu, angalau wanakupa kitu cha kuonyesha kwa wananchi wako kama uwanja mpya wa mpira wa taifa!
Ni kweli enzi za Mwalimu, waya ulikuwa mkali, lakini tuliweza kubanana humo humo, sasa mkuu tunajaribu hata kujikunja humo humo lakini damn! mambo ni mazito mkuu unajua bei ya petroli sasa mkuu?
jana mkuu mmoja aliniambia "..Sikiliza kijana tatizo sio mikataba ya Buzwagi, tatizo ni maisha yamekuwa magumu mno.."
UCHINA ilibadilika sana baada ya kifo cha mao. mtakumbuka kwamba mke wa mao na 'genge' lake la wazandiki waliwekwa ndani na mzee Deng Xiaoping ambaye ndiye anaaminika kuwa muasisi wa sasa wa 'Chinese economic miracle'. 'Free market socialism' imeleta maendeleo makubwa na ya haraka sana uchina ndani ya kipindi cha miaka ishirini tu! wachina sasa wanarusha sateleiti, wachina sasa ndio wakopeshaji wakubwa wa serikali ya marekani ( the value of US Treasury bills in chinese hands exceed 1trillion dollars. now that is very serious money!).
Icadon,
Thx kwa story hiyo ya BBC, kwani ime-paint picha nzuri ya China!!. Kitu kizuri ktk system ya China kama ilivyoonyeshwa ktk story ni kwamba muwekezaji wa kigeni lazima awe na partner wa kichina......tunaweza kuiga hiyo toka China. Vinginevyo tutafute formula yetu wenyewe,........
Three of China's most senior leaders, including Vice-President Zeng Qinghong, are to step down. Zeng and two other politicians, Luo Gan and Wu Guanzheng, were dropped from the Communist Party's central committee at its five-yearly congress. The announcement is seen as the first stage in a widely expected reshuffle in favour of a new generation of leaders.
The three men cannot now be elected to the standing committee on Monday when their replacements will be named. The nine-member standing committee is the country's supreme decision-making body. A fourth member, Huang Ju, died in the summer and will also be replaced. The congress also decided to include President Hu Jintao's "scientific concept of development" in the party constitution.
President Hu is widely expected to be given a second term as general secretary of the party when the central committee meets on Monday.
New generation
At the final day of the 17th Communist Party Congress in Beijing's Great Hall of the People, delegates elected a central committee of 204 full members. Vice-President Zeng, 68, was not amongst those named. His absence means he cannot be elected to the party's politburo or the smaller standing committee, whose members the central committee will elect on Monday.
Wu Guanzheng, in charge of party discipline, and Luo Gan, who oversaw national security as head of the party's politics and law committee, also stepped aside. Vice-Premier Wu Yi, Vice Premier Zeng Peiyan and Defence Minister Cao Gangchuan were also not named. Mr Zeng, whose father was a veteran revolutionary, was ranked fifth in the party hierarchy and has previously been linked with former President Jiang Zemin.
His retirement could be taken as a sign that President Hu is solidifying his grip on the country's political system, says the BBC's Michael Bristow in Beijing. The announcement prepares the way for the appointment of China's next generation of leaders.
There has been considerable speculation about who will be part of that new generation, our correspondent says. The congress was closely stage-managed from start to finish, with delegates singing the left-wing anthem the Internationale at the closing ceremony, says our correspondent.
But as delegates left the Great Hall of the People on the edge of Tiananmen Square, a shouting protester was bundled away by police.
'Princeling'
Mr Zeng is a Beijing-trained engineer who also took part in tough trade negotiations with the United States.
He belonged to the elite group of China's "princelings", the children of veteran Communist Party revolutionaries.
His father, Zeng Shan, was a Red Army veteran and went on to become vice-mayor of Shanghai in 1949 and minister of internal affairs in 1960. His mother, Deng Liuqin, was in charge of the Shanghai-based East China Kindergarten where the children of many senior officials were brought up.
Mr Zeng worked as an aide to Mr Jiang when he was Shanghai Party secretary in the mid-1980s. When Mr Jiang was transferred to Beijing after the 1989 pro-democracy student movement, the one adviser he chose to take with him was Mr Zeng. Mr Zeng was elected a member of the Communist Party's standing committee in November 2002, five months before he became vice-president under Mr Hu.
..UCHINA ilibadilika sana baada ya kifo cha mao. mtakumbuka kwamba mke wa mao na 'genge' lake la wazandiki waliwekwa ndani na mzee Deng Xiaoping ambaye ndiye anaaminika kuwa muasisi wa sasa wa 'Chinese economic miracle'. 'Free market socialism' imeleta maendeleo makubwa na ya haraka sana uchina ndani ya kipindi cha miaka ishirini tu! wachina sasa wanarusha sateleiti, wachina sasa ndio wakopeshaji wakubwa wa serikali ya marekani ( the value of US Treasury bills in chinese hands exceed 1trillion dollars. now that is very serious money!).
maendeleo ya kiuchumi yameleta kujiamini..china can now 'throw its wait around the world' na sio tena taifa la kusukumwa na kudharauliwa. one area where i have tremendous respect for china is the way they fight corruption.kosa la kula rushwa na ubadhirifu uchina..adhabu yake ni kunyongwa! we have seen the party boss in shangai executed, we have seen the head of the drug administration excecuted! HAYA NDIO YA KUJIFUNZA KUTOKA CHINA.
Naweza kuendelea kuandika mengi kuhusu china...ila inabidi watu wajue uchina ilikotoka.
Huko u-China, kamati kuu ya chama ndio yenye power ya kuongoza, ina wajumbe 22, rais wa nchi ni katibu tu wa chama hicho kinachotawala kuna mwenyekiti ambaye ni powerfull pia anweza hata kumuondoa rais kwenye chama,
Kamati hiyo hukutana kila mwezi mara moja as a mandatory, wanapokutana tqo top academics are ushered in to brief the committee on trends in ernegy supply, patterns of urbanization or intellectual-property rights, usually the discussions can last until the evening, sasa the thought of the entire kamati kuu sitting down the whole day, kusikiliza academics kwa msaaa na kuyafanyia kazi yaliyosemwa, it is amazing.
...tunachohitaji ni wananchi committed kwa maendeleo na pia viongozi walio-serious, na ni muhimu kuwa na heshima kwa The Rule of Law, huko China kiongozi akikamatwa kuwa ni mwizi, hupigwa risasi hadharani, hapa Tanzania kama alikuwa waziri wa Nishati, huhamishwa na kuwa waziri wa jumuiya ya Afrika mashariki!
Mungu Aibariki Bongo!
...BWM aliisha peleka watu China kuangalia jinsi jamaa hao walivyofanikisha na report kamili ilifikishwa kwake. Hiyo report inamhukumu yeye na sio kumsaidia kama ilivyokuwa report ya Warioba. Ziara ile imebaki historia kwa sababu alizosema Mzee ES.... wazee waliotakiwa kusimama na kuhakikisha sera mbovu hazipiti wamelala wenyewe usingizini na wamefungwa kamba za shingo utadhani mbuzi malishoni.
Hakuna kitu cha ajabu kabisa kwa China kufanikiwa na kama sisi tungeweza kutumia mirathi yetu - kwa kuanzia tu tungekuwa mbali kidogo. Mikoa ya Pamba yote ilikuwa na viwanda vya nguo lakini ilikosa mali ghafi, uzalishaji wa pamba ulipungua sana kwa sababu Tanzania tulitegemea soko la nje kuuza pamba yetu. Tazama basi ktk soko la nguo China, Afrika imeshika nambari mbili ktk waagizaji wake wakubwa na sasa hivi China imeshika namba moja kwa uzalishaji wa pamba (mali ghafi) ikifuatiwa na Marekani na India. Afrika tumetupwa nje kabisa kwa sababu pamba yetu pamoja na kuwa madhubuti na msemo wa kihuni Original lakini hakuna uhakika wa supply... mwaka hadi mwaka,pamba yenyewe adimu kupatikana kwani wakulima wetu maskini sana. Leo hii asilimia kubwa ya mashamba ya pamba miaka ya 70 ni mashamba ya mazao ya chakula. Wakulima can't afford life kusubiri mavuno ya mwaka mzima kupata malipo ya kazi ngumu. Na hadithi hii ipo ktk kila zao la kuuza...China walikuwa ktk position kama yetu na wameweza ku-reverse kutokana na kuwepo na UWAZI ndani ya chama tawala, wataalam na wanafunzi wa vyuo vikuu, Leo hii wananchi wake wana-enjoy matokeo.
!
Mzee Bob,
Ukweli uko hapo kwenye viongozi wa juu, tunacho kila kitu waChina walichonacho, maneno yote ya Uchina yako kwenye kamati kuu ya chama chao bro! Mwenyekiti hatoi uamuzi wa mwisho bila ya kushauriana na wenziwe, line of succession kwa viongozi wao ni very clear siku zote akitoka nani ataingia nani, na hao wote waliopangwa kwenye line ni viongozi walipimwa na kuchujwa kwa uangalifu mkubwa kwa kuzingatia uwezo na elimu, matokeo yake ni kuwa hakuna mwanya wa kiongozi mmoja kutumia ujanja ili apande, au kuchukua madaraka bila ya kupitia system kichama na kisheria,
Wapizani wa Nyerere wakati wote hawakuwa na nia nzuri. Kwanza kabisa hawakukubaliana na malengo yetu kitaifa - UJAMAA na KUJITEGEMEA. Na kibaya kuliko yote hawa wapizani hawakuwa na vision yeyote nje ya Ujamaa na kujitegemea... They had nothing to sale..
Walipinga Ujamaa kwa sababu, uliondoa kabisa nafasi yao kuwa watawala weusi wenye uwezo wa kujilimbikiza mali na vyeo..
...naupinga Ubepari kwa sababu wao wanaamini kwamba waafrika tunachohitaji ni just basic survival..I strongly discredit the notion. Waafrika tunastahili zaidi ya kupunguza umaskini ama kuondoa Umaskini....tunahitaji kuwa na vision mbele...to be able to make choices; to decide to do basic things without constraint, to live in a predictable environment, and have some control over what happens around us.
Mzee FD,
Heshima yako mkuu, katika society yoyote ile lazima kuwa na viongozi au kiongozi, sio kila wakati ni lazima kiongozi awahusishe wananchi katika maamuzi muhimu kwa ajili ya their future, Mimi sio kabisa fan wa JKN, lakini kwenye hili la Wachina ni lazima kumpa heshima yake kuwa alikuwa na vision ambayo ni moja kati ya important skill kiongozi anapaswa kuwa nayo,
Mwalimu aliwashirikisha wananchi na viongozi, tatizo ni wananchi wasio kuwa na mwamko wa kisiasa, elimu ndogo ya kuelewa faida na hasara ya maamuzi makubwa au ya kitaifa kisiasa, na viongozi waongo na wanafiki tena nitakutajia kwa majina viongozi waliokuwa karibu na Mwalimu ambao walipaswa kufa kabla ya kukubali kuona mambo ya Mwalimu yanaharibiwa,
...viongozi waliokuwa karibu na Mwalimu, na mpaka leo hawa bado wana influence kali katika siasa za bongo kwani hata JK mwenyewe asingeenda kokote katika uchaguzi bila ya kukubaliwa na 75% ya hawa wazee, hawa ndio waliopaswa kuweka mguu chini na kuwakatalia hawa kina BM maamuzi yao machafu. BM hayumo kwenye hilo kundi juu kwani he was never close to Mwalimu kabla ya uchaguzi wa 1995, BM siku zote alikuwa karibu na Butiku lakini sio Mwalimu kwa sababu elewa kwamba kabla ya kuwa rais BM hakuwahi kuchaguliwa hata NEC, kila alipogombea alikuwa akishindwa, kule Uchina kuna viongozi kama hao juu waliobaki katika chama hawayumbi hata siku moja katika kusimamia misimamo ya maendeleo ya nchi yao iliyowekwa china na Mao na mzee DeoPing!
Mzee FD Mwalimu alifanya ya kutosha, somebody had to take it to another level, badala ya kuvunja misingi yake bila kuwa na cha ku-replace, China ni mfano mkubwa wa kuigwa na sisi kwani kama walivyosema waliotangulia, ni kwamba at one point sisi na wao tulikuwa tunawekwa meza moja nao na wakubwa wa West!
Mkandara na Kyoma,
...tulilelewa kuuchukia Ubepari kama wa palestina wanavyochukia WaIsraeli. Ilitakiwa ifundishwe kuwa hapo Labour productivity imeongezeka mara 2.To me that was wrong approach, fundisha ubepari unafanyaje kazi, fundisha ujamaa unafanyaje kazi, elezea uzuri wa ujamaa. Convice people dont put ideology in their heads!, hilo linakuwa tatizo pale wanapoenda nje ya nchi na kujifunza mambo mengine!
Turudi sasa kuhusu China, Kwanza so far tumekubaliana kuwa ELIMU is a prerequisite, Elimu kwa wataalamu ambao wakimaliza ujue utafanya nao nini, tatizo elimu ilikuwa ikitolewa watu wanaishia nje, hatukuwa na mipango.
Pili Capital, tutapataje capital?, we can reduce Govt expenditures by restructuring Govt depts, tunaweza kuondoa mlolongo wa vyeo, Katibu tawala mkoa na mkuu wa mkoa = duplication. Mkuu wa wilaya, meya, mkurugenzi wa wilaya - mmoja aondoke. tupunguze wizara etc etc Nadhani wataalamu wataleta mbinu tu.
Tatu, kuwe na mikakati ya kuzungusha pesa humuhumu, Ukichukua sera za CUF na chadema unatekeleza hili bila taabu. Muheza kuna machungwa, tutumie TASAF au kama inaweza kuundwa chombo cha kuunganisha wananchi mwenye mtaji wa millioni au laki tano, ukipata kama 100, basi unawafungulia ka kiwanda kidogo cha kusindika matunda (kuna mtu alishatoa wazo hili hapo juu), wanakuwa wamiliki na wanafanya kazi hapo, unawasaidia wataalamu wa juu tu!
Nne, Wahandisi, hawa ni kiini cha kunyanyua uchumi, kama unataka kubadili kabisa mwelekeo wa uchumi basi inabidi uwatayarishe hawa na uwe na Labs za kutosha, yaani inatakiwa heavy investments on these guys. Pale Udsm kuna Bicco, sijui bado wapo?, hawa ndio watatengeneza mashine zote tutakazotumia kuwa wezeshea wananchi, How do they do that? peleka hata nje miaka mitatu wakaibe technologia, waibadili kidogo iendane na hali halisi.
...Naomba tukae chini kila mmoja atoe TUFANYE NINI KUELEKEA WALIPO WACHINA SASA HIVI. Once done mmoja anaweza kutoa summary, Mzee Es na wengineo wanaweza kuwakilisha kwa JK
FD
...Matokeo ya maendeleo ya China ni Uzalendo wao, hekima na Busara za watu kama kawawa hazikupuuzwa na wasomi. Hakuna Mchina anayeamini mzungu kuwa ni bora kuliko Mchina hata kama hakusoma. Wachina hawaamini kwamba elimu toka nchi za magharibi ndiyo nguzo ya maendeleo ama mafanikio kimaisha ila elimu ya darasa na ufundi (techonology)inaharakisha mafanikio hayo kwa ufanisi.
Bongo hatuna kabisa Uzalendo ndugu yangu na msomi ndiye Mungu wa mafanikio hali tunao matajiri wenye maisha mazuri hali hawana elimu ya darasa isipokuwa vision na elimu ya kuendesha shughuli yao. Nyuma ya utajiri wao ndiko wamesimama wenye elimu ya darasa. Bongo tunataka kiongozi msomi hata kama hana vision, busara wala hekima ya uongozi ili tupate kitu gani sijui!. Tanzania hata hiyo vision inaletwa na mzungu kupitia kwa akina Juda....Kwa hiyo vision muhimu sana kwa kiongozi.
Nakumbuka China kitu cha kwanza kilikuwa kukuza kilimo na mashamba yote yalipewa wananchi toka mikono ya serikali. Wakulima China walizidi population ya ajira zote combined kama Bongo vile, na iliposemwa serikali itawasaidia wananchi kupata zana za kilimo na pia kuwaambia wananchi zao gani linatakiwa toka sehemu fulani, kisha wakajenga viwanda sehemu hizo kuhakikisha mazao yanafika ktk finished product hukohuko vijijini!...
Looh nchi za magharibi walicheka sana, kwa sababu nchi za magharibi wakulima ni asilimia ndogo sana na nchi nzima viwanda vipo mijini sio mashambani.
Well it worked for Chinese kwa sababu viwanda hivyo hivyo vilivyojengwa mashambani ndivyo leo hii vinazalisha mali zote za Marekani na Ulaya. Viwanda hivyo vingejengwa mijini ambako maisha ni ghali na hakuna cheap labour leo hii China ingekuwa ni hadithi nyingine. Wachina waliyaona haya mapema kabla ya mzungu.. vijijini wananchi wake hawahitaji mshahara mikubwa. Chakula rahisi wanalima wenyewe, nyumba zao za kuezeka matumizi ya umeme sio makubwa wala mtu kuwa na gari sio hoja, baiskeli zinatosha...Na kubwa kuliko yote watu hawana haja ya kwenda mijini kutafuta ajira...
Mzee Es,
...Tumeingia Ubepari bila kuwa na fahamu akilini ni kitu gani kinachokuja na Ubepari. Wananchi na viongozi wote hawana elimu yake zaidi ya imani tu kama ilivyo imani ya dini.. Na kwa bahati mbaya hata haya tuliyoyapata ni mageni kwetu, hakuna aliyefahamu kinachokuja - hatukutegemea kupata kitu zaidi ya tulichokuwa nacho, hatukujiandaa kupokea kitu kwa hiyo basi haya tuliyo nayo ni maendeleo tosha kwa maskini mlalahoi. Wakati wenzetu wanaweka mikataba ya kiuchumi baina ya nchi sisi ndio kwanza tunalazimishwa kupokea misaada kwa kuweka rehani maliasili zetu. Kisha tunatafsiri globalization kuwa uwekezaji toka nchi, ubinafsishaji toka nje na hata wataalam toka nje ndio maana kamili ya globalization.
Tatizo kubwa alilokutana nalo Nyerere ni hawa wasomi wa bara ambao walikwenda Ulaya na kupenda waliyoyaona huko kisha wakaanza kuota ndoto za kubadilisha maisha yao wenyewe ndani ya Tanzania ili wao kuwa kama wazungu watawala..
Wasomi hawa ndio waliotaka madaraka baada ya uhuru wakimbilia majumba ya uzunguni na kuendesha serikali za nchi vibaya kuliko hata Mkoloni, hawakuwa na vision kabisa zaidi ya kuendeleza yale ya Mkoloni chini ya Utawala wa mweusi. Hesabu ya viongozi kama hawa Afrika ilizidi hesabu ya watu kama Nyerere ambao walijawa na uzalendo mbali na kuwa na vision ya hata mwaka mmoja mbele. Kati ya mataifa 42 ya wakati huo miaka ya sitini labda nchi sita tu ndizo zilikuwa zimeukubali Ujamaa ama niseme Uzalendo. Hapo dhahiri dalili ya kushindwa kwa Ujamaa Afrika ilikuwa kubwa sana.
...kwa matazamo wa kibiashara dunia ilikuw na maskini wengi kuliko hata middle class na hata hao middle class maisha yao yalikuwa ktk kulipa nyumba, magari na hawana akiba zaidi ya kutumia kwa vitu vya thamani kubwa. Kwa hiyo hapa Mchina akawa mshindi kwa biashara zote za retails ktk mataifa yote makubwa na madogo. Kikubwa zaidi China hawakubinafsisha mali ambazo walifahamu ndizo ngao yao kwa nchi za magharibi. Serikali ilitoa shares kwa wananchi kidogo kidogo na mamlaka mikoani yalipewa sauti na nafasi kubwa ktk kujiendeleza kiuchumi.
Hali Tanzania sisi tumeuza mashirika yote na badala ya shares za mashirika makubwa kuwekwa ktk soko letu la Dar-es-Slaam Stock exchange tumewaachia wazungu haohao wakishirikiana na wahindi kutafuta wawekeshaji na kuchukua shares za wananchi. Mali ambayo Nyerere aliiweka kama mirathi ya Watanzania baada ya kujifunga mikanda miaka ishirini na mitano ya Ujamaa. Leo hii mwananchi hana sauti kabisa kwenye miradi zaidi ya sigara, pombe na mingine michache. And we are opt to sale the all country!...
Kama ulivyo msemo wa baadhi viongozi wataalam kila wanapojadili swala la Uwekeshaji -Tunaiuza nchi... wakifikiri neno hili lini maana nzuri sana kwa taifa letu kiuchumi hali wamesahau kabisa kwa nini tuligombea Uhuru wetu 1960.