THE BOOK OF THE DEAD; Chanzo na mwanzo wa kila tunachokifahamu kuhusu imani mbalimbali ulimwenguni

Undava King

JF-Expert Member
Aug 11, 2017
3,181
5,321
THE BOOK OF THE DEAD ni jina linalo-mislead ukweli fact ni kuwa hili ni jina la kubambikiwa tu na lilianza kutumika katika karne ya 19, vitabu au kurasa za maandishi haya yalikuwa yakiandikwa kwenye msahafu au scrolls na kuwekwa pembeni ya wafu wanapokuwa wamepumzishwa katika nyumba zao za milele (chanzo cha kuitwa vitabu vya wafu),

Tunatambua kuwa wenzetu walitumia sana mapiramidi kuzika watawala wao ambao ndiyo hasa walikuwa walengwa wa maandishi haya kwa nia ya kujitwalia maisha mazuri soon wakifika huko afterlife waendako wapokelewe vyema na wenyeji wao.

Iliaminika kuwa nguvu za uovu(power of evil) uwinda roho za wafu pindi wawapo njiani kuelekea kuzimu katika ufalme wa mtawala wa huko yaani mungu OSIRIS.

Miungu wakuu hata wao waliofia kukumbwa na uovu huu hivyo nao walijilinda dhidi yake kwa manuizi (spells) na magical names pamoja na maneno yenye nguvu ambayo yalibuniwa na kuandikwa na mungu THOTH.

Iliaminika kuwa mungu jua Ra (the sun god Ra) alikuwa na neno la siri alilopewa na THOTH ambalo halilitumia kupambana kipindi cha machweo ya jua kuyakabili mapepo hayo au great devil hili kuweza kuleta nuru yake mchana.

Book of the Dead iliwezaaminika kuwa ingeweza kumpa mwanadamu uwezo wakushinda duniani na katika ulimwengu mwingine, itamwakikishia usalama na kupenya kwa urahisi kuzimu(underworld) na itampa Uhuru wa kuingia na kutoka kuzimu na kumzuia kufa mara ya pili, hili liliwezekana tu kwa mwanadamu huyu kuweza kuyaelewa na kurecall maneno yote yaliyopo ndani ya kitabu hiki kabla na hata baada ya kwenda huko aendako akifa.

Na hili kufanikiwa ilipaswa kujitakasa kwanza kwa kutoshiriki tendo la ndoa na wanawake, usile samaki wala nyama na uhakikishe unakuwa msafi kimwili na kiroho.

MIUNGU WAKUU

Amen Ra "King of the gods" Mungu wa miungu, "The lord of all the gods" Bwana wa Mabwana"

Osiris " the giver of evalasting life" huyu ndiye mungu mtoa uhai na mpaji.

THOTH mwandishi na mtunzi wa kitabu cha wafu; kimisri wanamtambua kama Tehehuti au Tehuti.

Kitabu cha Wafu inahaminika kuwa ni moyo na akili ya muumba, pia huitwa Pautti na wenyeji huku wageni wakikitambua kama Ra.

THOTH pia ni ulimi wa muumba usemao kwa sauti juu ya kusudio lake na kuamua kila kilicho juu ya mbingu na nchi vipate tokea. Thoth aliumba vyote vya angani na duniani ikiwemo jua, mwezi,maandishi, designs, Sanaa, mahesabu na milinganyo yake.

Kupitia sifa yake ya utunzaji wa kumbukumbu za Mungu aliitwa pia "Recording Angel" yeye ndiye inventor wa physical and moral law inayompa personification of JUSTICE (mtenda haki) na hili linatokea kufuatia kundi la miungu mbinguni, duniani na sehemu zingine za ulimwengu kumtawadha/kumtunuku uwezo wa kusema na kutekeleza juu yao na hakika Neno lake halitiwi shaka wala kuulizwa kama liko sahihi maana hakika ni kweli na ukweli mtupu.

"They appointed him to weigh the words and deeds of men, and his verdicts were unalterable, he become more powerful in other world than Osiris himself."

Osiris alijitwalia ushindi wa nguvu dhidi ya Set katika ukumbi mkuu wa hukumu ya miungu kupitia msaada wa Kinywa cha busara na hekima cha THOTH kama wakili au advocate na pia kwa ushawishi aliokuwa nao kwa miungu wa mbinguni.

Na kila amfatae OSIRIS hana budi kumwamini THOTH ili kuwa salama na kujiepusha na adhabu kali siku ya hukumu na kuhakikishiwa makazi ya milele katika ufalme wa OSIRIS.

Kama ambavyo THOTH aliweza kumtetea OSIRIS katika kesi yake na akashinda vivyo hivyo wamisri pia utegemea atawatendea vivyo hivyo pindi wakitangulia mbele ya haki.

OSIRIS mungu wa taratibu na kanuni(sheria), uzazi wa Nile, alikuwa incarnate(alizaliwa tena) duniani kama mtoto wa GEB, "mungu wa dunia" na NUT "mungu mke wa anga" Ana dada zake wawili ambao ni ISIS na NEPHTHYS na kaka yake mmoja SET.

OSIRIS alimuoa ISIS na SET alimuoa NEPHTHYS. GEB akamteua OSIRIS kukaa kwenye kiti cha ufalme wa misri na akafanikiwa kutawala kwa ustadi na ubora uliotukuka kiasi kwamba nchi ikastawi na kuwa yenye furaha kipindi chote cha utawala wake.

SET kwa kuliona hili akaingiwa na wivu dhidi ya kaka yake na akatamani kumchinjilia mbali ili haweze kujitwalia kiti cha ufalme na ISIS ambaye reputation yake kama mke mwaminifu na mwenye mapenzi ya dhati kwa mumewe na mwangalizi yaliujazia sifa utawala wa mumewe OSIRIS. Hivyo kwa namna moja au nyingine suala la kumwangamiza lilikuwa haliwezi kuzuilika jambo ambalo SET alilifanikisha kwa kumuua nduguye kwa kumzamisha majini.

Stori nyingine katika kisa hiki hiki yadai kuwa ISIS akisindikizwa na dadaye NEPHTHYS walienda huko Nefat, wakafanikiwa kuuchukua mwili wa OSIRIS na kwa msaada wa ANPU, kijana wa mungu jua Ra. Walifanikiwa kumrejeshea uhai temporary kabla ya kufa tena na mkewe ISIS akatumia nafasi hiyo kujipatia mimba na akamzaa mwanae ajulikanae kwa jina HORUS.

Ilikumwepuka SET ambaye katika kesi moja aliwahi muua HORUS kwa kumtumia scorpion amng'ate, mama yake yaani ISIS alitumia muda mwingi sana kukimbia huku na huku akiwa pande za huko delta hili asiingie mikononi mwa adui.

Kwa kipindi chote hiki ambacho ISIS na mwanae HORUS wakitaabika bila furaha ni THOTH ndiye aliyekuwa akiwasaidia katika magumu yote, akiwapatia neno lenye nguvu na faraja iliyomrejeshea HORUS uhai wake nakuvuka baadhi ya vikwazo vya mamba na viumbe vya ajabu huko delta.

HORUS alivyokuwa mkubwa akaahidi kulipiza kisasi kwa kum-revenge baba yake OSIRIS. Siku ilipowadia akakutana na SET vita ikapiganwa haswa mpaka SET akazidiwa akiwa katika zile hatua za kuangushwa chini akawahi na kumchana katika jicho la kulia HORUS hivyo akalitunza na kuondoka nalo.

Hata baada ya vita hivi HORUS alikuwa na maumivu makali na akuweza kupata tena nguvu ya kumdhibiti SET hivyo SET akamchukua ISIS lakini THOTH akaingilia kati na kumfanya SET arudishe jicho la HORUS ambapo THOTH aliamua kulipachika katika paji la uso wa HORUS na kuliamuru lirejeshe nuru yake kama awali.

Kupitia maelekezo ya THOTH, HORUS aliambatana nae kwenda kuzuru alipozikwa baba yake(OSIRIS) na akamfufua. Katika kumfufua huko lile jicho la HORUS likang'olewa tena na kupewa OSIRIS baba yake alimeze na mara baada ya kufanya hivyo akawa na nuru ndani yake huku akiibuka na cheo cha ushindi dhidi ya kifo na kuwa Lord of the Dead and King of the Underworld "BWANA WA WAFU NA MFALME WA KUZIMU"

Hivyo kupitia hili OSIRIS akawa type na symbol of resurrection (ufufuo) kwa jamii ya wamisri kwa miaka yote, kwa sababu yeye ni mungu ambaye kiasili ni Immortal kwa kufufuka kutoka katika mauti.

NB: Ni imani yangu kuwa nje ya kuburudika na simulizi hili, kuna jambo au baadhi ya mambo umeyang'amua na yamekupa picha fulani au majibu juu ya maswali ambayo umekuwa ukijiuliza juu ya imani yako.

Nikusii usikose sehemu ya mwisho ya masimulizi haya marefu ambayo nitajitahidi kuyafupisha kwa kadri niwezavyo hili usikose uhondo na mtiririko muruwa wa stori hizi muhimu za kale.
 
SEHEMU YA PILI:

Katika sehemu iliyopita tunaambiwa tu kuhusu OSIRIS kuwa mfalme wa kuzimu.

Je kabla ya hapo ni maswahibu yapi alikumbana nayo?

Tunaelezwa kuwa OSIRIS alipitia mateso makali kutoka kwa SET nakupelekea kifo chake ambapo shtaka hili lilifikishwa kwenye baraza la miungu na SET mwenyewe akidai kuonewa na atendewe haki.

Makundi ya miungu wote walikusanyika huko mbinguni pajulikanapo kama ANU au HELIOPOLIS nakuagiza OSIRIS asimame ajitetee kulingana na madai yanayomkabili kama mshtakiwa.

ISIS na NEPHTHYS wakamleta SET mbele ya miungu huku upande wa mshtakiwa ukiwakilishwa na HORUS "the avenger of his father" ambaye yeye kwenye kikao hiki cha baraza kuu la miungu wote au mahakamani alikuja kushuhudia tu mwenendo wa kesi inayomkabili baba yake OSIRIS.

THOTH akiwa kama wakili na shuhuda wa yale yaliyomtokea OSIRIS aliamua kujitolea kumtetea OSIRIS nakuweka wazi maovu yote ya SET na kwamba yote aliyosema SET mbele ya miungu ni uongo,

hivyo NENO la THOTH likathibitika mbele ya baraza la Heliopolis kuwa ni kweli na kwamba OSIRIS hana hatia. THOTH akapendekeza kuwa kwa kitendo alichofanyiwa OSIRIS anapaswa kutambuliwa kama the "Great God" na apewe sehemu yake ya utawala ya kuwa The Kingdom of Underworld na SET lazima aadhibiwe vikali kwa makosa yake.

Hivyo kuanzia pale OSIRIS akatambuliwa rasmi kama "MA KHERU" true word (mnena kweli/mwenye haki) hapo miungu wote wakakubaliana kuwa hukumu hiyo na judgement ilivyofanyika ni sawa na hawana shaka yeyote na alichokiamua THOTH ni ukweli na haki. Hivyo SET akashikwa na kufungwa kamba kama beast au joka kisha akatupiliwa mbali na kusambaratika vipande vipande.

OSIRIS baada ya ushindi huo mnono alienda kutawala kwenye realm ya kuzimu kama ambavyo Ra mungu jua ni mungu wa anga. Na eneo hili la wafu au ardhi ya waliokufa huitwa "Tat" au "Tuat" lakini mahali ilipo hata wamisri wenyewe wapo njia panda.

Wachunguzi wa mambo udhani kuwa kuzimu yaweza kuwa ni eneo fulani ambalo haliko juu yaani angani wala chini yaani duniani ila pengine yaweza kuwa katika mipaka fulani nje ya upeo wa dunia isiyoonekana kwa macho yaani IN THE OUTER DARKNESS.

Inavyoelekea kuzimu siyo sehemu ya furaha, tukijudge kupitia kurasa za the Book of Dead wakati ANI the scribe alipowasili pale alisema kuwa,

"What is this to which I have come? There is neither water nor air here, it's depth is unfathomable, it is a dark as the darkest night, and men wander about here helplessly. A man cannot live here and be satisfied and he cannot gratify the craving of affection" chapter CLXXV.

Hivyo Egyptian umchukulia OSIRIS kama mtoa hukumu ya haki na maisha mapya baada ya yeye mwenyewe kuonesha mfano kwa kukishinda kifo, hivyo nyakati za mwisho atasimama nao mbele ya kiti cha hukumu nakuwatendea inavyostahiki waja wake kuurithi ufalme wake.

Under the early dynasties the priesthood of ANU (the ON of the Bible) strove to make their sun god Ra, preeminent in Egypt.

Jambo ambalo halikuzaa matunda kwa kuwa cult ya ibada ya mungu huyu aikukubalika machoni pa watu wote kuwa ni sahihi. Bali ilijikita zaidi katika kuwapa favor tabaka la kina pharaoh, maofisa na watu wenye nguvu au matajiri lakini hata watu wa materialistic wa misri hawakukubaliana nalo.

Hivyo katika kuakikisha kuwa watu wanaitekeleza hiyo cult kinguvunguvu, wapingaji wote walikamatwa na kukatwa vichwa mchana kweupe na miili yao kuteketezwa kama sadaka kwa kuchomwa moto hadharani wakati wa jua kali wakiamini kwa kufanya hivyo kutawafanya watu waofie kumpinga Ra mungu jua na vilevile watamfurahisha mungu wao. (chanzo na mwanzo wa ibada za kipagani na machukizo)

Ebu tuutazame muundo au structure ya kiti cha hukumu cha OSIRIS kilivyo;

Katika chapter ya CXXV ambazo hujulikana kama papyrus of ANI prefaced by Hymn to OSIRIS (sifa za utukufu kwa mungu osairas) OSIRIS huonekana kama aketie katika miisho ya ukumbi wa MAATI huku akiwa na miungu wa kike wawili mmoja ni SHERIA na mwingine ni TRUTH wakifuatiwa na miungu wa baraza hilo 42 ambao wapo pale kumsaidia.

Kila mmoja wa miungu hawa 42 ambao uwakilisha nomes of Egypt na symbolic name wakati ambao aliyekufa atakuwa amepatia kurudia kwa usahihi magical names za mlango wa ukumbi na ukafunguka kumruhusu aingie cha kwanza atalakiwa na miungu hawa ambao wamekaa kwa mtindo wa mgawanyiko wa mistari miwili kila mmoja ukiwa na miungu 21.

Mwisho kabisa jirani na aketipo OSIRIS, where the Great scales, under the charge of ANPU (ANUBIS) na monster AMEMIT, mlaji wa wafu mfano mioyo ya watenda dhambi ambao wamethibitika kuwa na hatia katika hukumu ya OSIRIS.

"Thou shalt be reported. (Tell me) Who is he whose roof is fire, whose walls are living serpents, and whose floor is a stream of water? "The deceased having replied. "OSIRIS"
Hivyo kama ulikuwa unajiuliza jukwaa kuu au kiti cha hukumu kinafananeje ndiyo hivyo.

Kwahiyo mfu usonga katikati ya ukumbi wa hukumu na kuwaelezea kila miungu kati ya wale 42 namna gani ajatenda dhambi ndipo mwisho hukumu uamuliwa.

Sasa ebu tutoke huko kwenye hukumu na tuangazie kuwafahamu kwa majina tu wale miungu wote 12 ambao uketi katika kikao kikubwa cha mbingu ANU au HELIOPOLIS ambao katika hawa kila mmoja ana historia yake, ibada na sifa zake ambazo haitoshi kuzielezea hapa:-

1. Harmachis 2. Tem 3. Shu 4. Tefnut 5. Geb 6.Nut 7. Isis 8. Nephthys 9. Horus 10. Hathor 11. Hu 12. Saa

Asanteni kwa wale mliothubutu kufatilia kuanzia mwanzo mpaka mwisho nina imani kuna kitu walahu mmekipata katika kunoa maarifa yenu kiroho.

Kwa wale wenye maswali au wenye utata mahali msisite kuuliza ntajibu kadri ya ufahamu wangu katika masuala haya ya kiroho nilivyoyaelewa pia wachangiaji watasaidia. Na kwa wale wenye kuongezea chochote, kurekebisha au kukosoa KARIBUNI.
 
Hicho ni Kitabu kinachofundisha Uchawi.
Vipo vingi sitaki kuviorodhesha hapa kwa kuchelea kutafutwa na watu na kuvisoma.

Stori za hicho kitabu zote ni za ukweli na wahusika wakuu ni Mashetani wengine wanayaita Maibirisi na malaika zao Majini Mizimu Nk.

Angalieni tu hayo majina sio yanayotumika kwa kuwaita Binadamu wa kawaida.

Nawatahadharisha watu wenye nia njema kuto kukisoma hicho kitabu.
 
Hicho ni Kitabu kinachofundisha Uchawi.
Vipo vingi sitaki kuviorodhesha hapa kwa kuchelea kutafutwa na watu na kuvisoma.

Stori za hicho kitabu zote ni za ukweli na wahusika wakuu ni Mashetani wengine wanayaita Maibirisi na malaika zao Majini Mizimu Nk.

Angalieni tu hayo majina sio yanayotumika kwa kuwaita Binadamu wa kawaida.

Nawatahadharisha watu wenye nia njema kuto kukisoma hicho kitabu.

Sawa Mkuu nashukuru kuwa walahu umekuwa mchangiaji wa kwanza kuonesha kuwa una ufahamu mzuri juu ya kitabu husika na ya kwamba kinazungumzia uchawi na ukatoa tahadhari watu wasikisome.

Japo ningependa walahu kukuuliza maswali machache nami nipate mwanga kidogo:-
1. Wewe waamini katika imani ipi? (Ni mkristo,muislamu,hindu,budhaa au hauna dini)

2. Umesema kuwa vinavyotamkwa hapo kwenye vitabu hivyo licha ya kuwa ni uchawi pia ni kweli kabisa.

Vipi ilishawahi kukutokea wakati uliposoma ukathibitisha ni kweli?

Je, kama ilikutokea au mwenzio unayemfahamu alikumbwa na mkasa wowote ilikuwaje?

Au waamini tu kuwa ni vitabu vya mashetani kwa kusimuliwa au kukatazwa kujiusisha navyo katika mrengo wa imani yako?
 
Sawa Mkuu nashukuru kuwa walahu umekuwa mchangiaji wa kwanza kuonesha kuwa una ufahamu mzuri juu ya kitabu husika na ya kwamba kinazungumzia uchawi na ukatoa tahadhari watu wasikisome.

Japo ningependa walahu kukuuliza maswali machache nami nipate mwanga kidogo:-
1. Wewe waamini katika imani ipi? (Ni mkristo,muislamu,hindu,budhaa au hauna dini)

2. Umesema kuwa vinavyotamkwa hapo kwenye vitabu hivyo licha ya kuwa ni uchawi pia ni kweli kabisa.

Vipi ilishawahi kukutokea wakati uliposoma ukathibitisha ni kweli?

Je, kama ilikutokea au mwenzio unayemfahamu alikumbwa na mkasa wowote ilikuwaje?

Au waamini tu kuwa ni vitabu vya mashetani kwa kusimuliwa au kukatazwa kujiusisha navyo katika mrengo wa imani yako?
Sio wote wanaoweza kusoma vitabu vya aina hiyo wanaweza kuhimili nguvu zilizomo kwenye hivyo vitabu.

Kama ilivyo kwa Sisi Wakristo Biblia ni Kitabu HAI.

Unapo kisoma Nguvu za Mungu zinakuzunguka na kukufuatilia na kama upo makini nacho basi Roho Mtakatifu anashuka kukaa ndani yako huku malaika wakikulinda ili upate manufaa ya hayo unayoyasoma humo.

Hali kadharika unaposoma Kitabu cha Ulimwengu wa Kuzimu nacho ni hai pia na kinafanya kazi muda wote.
Nguvu za Shetani akiwemo Shetani mwenyewe anakufuatilia kwa furaha sana na akiona unapendezwa na yaliyomo humo anakuja kuweka makazi yake kwako.
Hapo utakuwa umefungua Mlango wa Roho yako kukaliwa na Majini Maovu sana.

Kumbuka hicho kitabu kimeandika hadi Ibada halisi za Kishetani.
Mtu mwingine asiye imara anaweza kuvutiwa na hizo ibada na akajaribu kuzifanya, na hapo anaweza kujistukia usiku anahudhuria ibada halisi bila kujitambua na ni vigumu kujiondoa kwani unaweza pendezwa nazo hivyo kuendelea kuzifuatilia maana mambo mageni wakati mwingine yanapendeza kuyafanya machoni
Au anaweza kulazimishwa kuendelea kuzifanya kwakuwa keshazijua siri za Shetani.

Hapo tayari atakuwa ameshaingizwa kwanye ulimwengu wa Kishirikina.

Siku hizi uchawi haununuliwi bali unasoma tu vitabu kama hicho na kufanya vile kinachoelezwa humo na unakuwa Mchawi.

Ndio maana vitabu aina hiyo haviuzwi katika maduka ya vitabu vya kawaida.

Ila ukiwa na nguvu za Kiroho za Ki-Mungu, unaweza kuvisoma ila haimpendezi Mungu, kwani vinaweza kukushawishi pia na ukajaribu kufanya mambo yaliyoandikwa humo na ukaingia kwenye nguvu za Giza.

Unajua Shetani ukimwomba kitu anakujibu haraka sana ili akunase haraka haraka, na nivigumu sana kujinasua tena.
Ukimwomba pesa leo, kesho anakupatia au hata leoleo. Na kutokana na maisha ya sasa hivi watu wanataka maisha mazuri ya haraka haraka.

Hivyo mimi nimetoa kama tahadhari tu. Ili atakaye penda kusoma hicho kitabu atambue matokeo yake ambayo siyo mazuri.

Kwa kukujibu swali lako mimi nilishawahi kuvisoma vitabu vya aina hiyo tena vingi tu.
Na binafsi viliniathiri.

Nilishachukuliwa bila kujua hadi katika sherehe za Kichawi usiku na kuhudhuria mwanzo mwisho
bila hiari yangu.

Uzuri baada ya kama mwezi hivi ya kuhudhuria mambo ya Kichawi niliwaeleza Wazee wangu na wakafanya juu chini kunitoa huko.

Mara ya kwanza nilipelekwa kwa Waganga wazito wa mambo ya Kishirikina mmoja yupo Morogoro kijiji kinaitwa Kiberege kabla ya kufika Kilombelo. Mwulize mtu yotote wa Morogoro anamfahamu ni maarufu sana kijijini hapi simtaji jina.
Wakachinjwa kuku huko na nikalishwa filigisi za kuku za dawa na mambo kemkem.

Haikutosha nikapelekwa kwenye Maombi ya Mwalimu Mwakasege Arusha na nikaishi huko kalibu Mwezi mmoja pale Kijenge ndio hali ikarudi sawa.

Kama naongopa basi wewe binafsi endelea kukifuatilia hicho kitabu alaf utaona mwisho wake utakuja kutupa mrejesho humu.

THE BOOK OF THE DEAD ni mojawapo ya vitabu hatari sana kwa watu wa kawaida kukisoma kila kurasa na kuki rudia rudia.

Yangu ni hayo.
 
Sio wote wanaoweza kusoma vitabu vya aina hiyo wanaweza kuhimili nguvu zilizomo kwenye hivyo vitabu.

Kama ilivyo kwa Sisi Wakristo Biblia ni Kitabu HAI.

Unapo kisoma Nguvu za Mungu zinakuzunguka na kukufuatilia na kama upo makini nacho basi Roho Mtakatifu anashuka kukaa ndani yako huku malaika wakikulinda ili upate manufaa ya hayo unayoyasoma humo.

Hali kadharika unaposoma Kitabu cha Ulimwengu wa Kuzimu nacho ni hai pia na kinafanya kazi muda wote.
Nguvu za Shetani akiwemo Shetani mwenyewe anakufuatilia kwa furaha sana na akiona unapendezwa na yaliyomo humo anakuja kuweka makazi yake kwako.
Hapo utakuwa umefungua Mlango wa Roho yako kukaliwa na Majini Maovu sana.

Kumbuka hicho kitabu kimeandika hadi Ibada halisi za Kishetani.
Mtu mwingine asiye imara anaweza kuvutiwa na hizo ibada na akajaribu kuzifanya, na hapo anaweza kujistukia usiku anahudhuria ibada halisi bila kujitambua na ni vigumu kujiondoa kwani unaweza pendezwa nazo hivyo kuendelea kuzifuatilia maana mambo mageni wakati mwingine yanapendeza kuyafanya machoni
Au anaweza kulazimishwa kuendelea kuzifanya kwakuwa keshazijua siri za Shetani.

Hapo tayari atakuwa ameshaingizwa kwanye ulimwengu wa Kishirikina.

Siku hizi uchawi haununuliwi bali unasoma tu vitabu kama hicho na kufanya vile kinachoelezwa humo na unakuwa Mchawi.

Ndio maana vitabu aina hiyo haviuzwi katika maduka ya vitabu vya kawaida.

Ila ukiwa na nguvu za Kiroho za Ki-Mungu, unaweza kuvisoma ila haimpendezi Mungu, kwani vinaweza kukushawishi pia na ukajaribu kufanya mambo yaliyoandikwa humo na ukaingia kwenye nguvu za Giza.

Unajua Shetani ukimwomba kitu anakujibu haraka sana ili akunase haraka haraka, na nivigumu sana kujinasua tena.
Ukimwomba pesa leo, kesho anakupatia au hata leoleo. Na kutokana na maisha ya sasa hivi watu wanataka maisha mazuri ya haraka haraka.

Hivyo mimi nimetoa kama tahadhari tu. Ili atakaye penda kusoma hicho kitabu atambue matokeo yake ambayo siyo mazuri.

Kwa kukujibu swali lako mimi nilishawahi kuvisoma vitabu vya aina hiyo tena vingi tu.
Na binafsi viliniathiri.

Nilishachukuliwa bila kujua hadi katika sherehe za Kichawi usiku na kuhudhuria mwanzo mwisho
bila hiari yangu.

Uzuri baada ya kama mwezi hivi ya kuhudhuria mambo ya Kichawi niliwaeleza Wazee wangu na wakafanya juu chini kunitoa huko.

Mara ya kwanza nilipelekwa kwa Waganga wazito wa mambo ya Kishirikina mmoja yupo Morogoro kijiji kinaitwa Kiberege kabla ya kufika Kilombelo. Mwulize mtu yotote wa Morogora anamfahamu ni maarufu sana kijijini hapi simtaji jina.
Wakachinjwa kuku huko na nikalishwa filigisi za kuku za dawa na mambo kemkem.

Haikutosha nikapelekwa kwenye Maombi ya Mwalimu Mwakasege Arusha na nikaishi huko kalibu Mwezi mmoja pale Kijenge ndio hali ikarudi sawa.

Kama naongopa basi wewe binafsi endelea kukifuatilia hicho kitabu alaf utaona mwisho wake utakuja kutupa mrejesho humu.

THE BOOK OF THE DEAD ni mojawapo ya vitabu hatari sana kwa watu wa kawaida kukisoma kila kurasa na kuki rudia rudia.

Yangu ni hayo.
Nipende kukushukuru kwa mchango wako ambao wengi umetufumbua macho, maana ukipewa ushuhuda na aliyefikwa na jambo katika uhalisia ni bora zaidi ya nadharia.

Japo ninakuomba uweze kukipa kitabu hiki pia jicho la tatu la mtizamo tofauti kama mimi nilivyojaribu kukiundia picha hii,

then tutafakari pamoja uniambie kupitia huu mtizamo unaelewa nini, kwa maana yasemekana vitabu hivi vilikuwako miaka mingi kabla ya uwepo wa Biblia na vitabu vingine vitakatifu tunavyotumia kuamini leo hii.

Na uwezekano pia wa waandishi kukopi stori au wahusika wa The Book of the Dead ni mkubwa. Na kama ndivyo ilivyokuwa basi hata hivi vitabu vya sasa vina uhalakini ndani yake.

Mfano neno;

HOLY BIBLE linatokana na neno la Kigiriki:

HELIOS=JUA na BIBULOUS=KITABU

hivyo neno HOLY BIBLE = KITABU CHA JUA

mungu jua huko misri aliitwa Amun Ra na huko Canaan alijulikana kama Shemesh, na katika bible kuna mji waliuteka waisrael kwa jina la bethshemu (bethshemesh) au mji wa makao ya jua. Ni ukweli usiopingika kuwa imani nyingi zilianzia kwenye ibada hii ya mungu jua kabla ya kuja kwa idea zingine na practises kumuhusu mungu.

Wahusika katika stori ya the book of dead kwa uhusika wao, tukiwapa scenes katika Bible basi watafiti ifuatavyo kwa mujibu wa mfanano wa visa vyao:-

AMEN RA(the sun god)- MUNGU (Bwana wa mabwana na mungu wa miungu)

THOTH- NENO(ndiye sauti ya mungu, moyo na kusudi lake pasipo yeye akikufanyika kitu akitamka ujiumba na neno lake kamwe halina dosari, ndiye mtunza kumbukumbu zote)

OSIRIS- YESU ( mwenye haki machoni pa AMEN RA na miungu, alikishinda kifo na hivyo kupewa kiti cha ufalme, ndani yake yupo NENO(thoth) na NENO ni uzima, ndiye mwenye mamlaka na funguo za kuzimu, atawahukumu wafu na maombi yote ya uzima afterlife uelekezwa kwake)

SET- SHETANI/DEVIL

Shetani ni sawa na neno "Mshitaki" na kwenye stori hii SET ndo aliyemshtaki aliyemkosea.
Alitaka pia kujiinua hili kumpokonya mwenzake ufalme ambapo alifanikiwa lakini baadae akapokonywa na kuharibiwa.

Alipigana vita kubwa na Horus(malaika Gabriel ila utofauti wa hapa na kwenye bible ni kuwa alishindwa lakini alimjeruhi jicho Horus) na mwisho tunaona akiitwa kwa jina ambalo hata YESU kwenye Biblia alimwita nalo shetani yaani The father of lies au "Baba wa uongo")

HORUS- (Kama malaika mkuu au mkuu wa majeshi ya Amen Ra, na mwana wa pekee wa OSIRIS na ISIS (uonekana kiroho katika umbile la kichwa cha Tai) huyu ni msimamizi mkuu wa anga huku akiangaziwa pande zote na jicho la Ra( mwangaza wa jua)

Kwenye Biblia huyu character hazungumziwi kiundani ila kwenye Quran kuna muhusika anatajwa kwa waislamu kuchukua tahadhari dhidi yake wakimwita masihi dajjal au mwenye jicho moja au chongo (kwenye bible wanamwita mpinga kristo) huku kwenye stori tunamwona hana hatia yeye ni Avenger wa kifo cha baba yake OSIRIS sasa yupi anaongea ukweli katika haya maandiko yote matatu ya waisraeli, waarabu au wamisri hapa nami sijuhi.

Kupitia huo uchambuzi mfupi nilioufanya kupitia kuoanisha matukio hayo na vitabu vingine vya imani hili kupata walahu logic moja, wewe binafsi una mtizamo gani katika hili?

Je, wafikiri niwazavyo ni sahihi au siyo sahihi? Na kwanini wasema hivyo?
 
Nipende kukushukuru kwa mchango wako ambao wengi umetufumbua macho, maana ukipewa ushuhuda na aliyefikwa na jambo katika uhalisia ni bora zaidi ya nadharia.

Japo ninakuomba uweze kukipa kitabu hiki pia jicho la tatu la mtizamo tofauti kama mimi nilivyojaribu kukiundia picha hii,

then tutafakari pamoja uniambie kupitia huu mtizamo unaelewa nini, kwa maana yasemekana vitabu hivi vilikuwako miaka mingi kabla ya uwepo wa Biblia na vitabu vingine vitakatifu tunavyotumia kuamini leo hii.

Na uwezekano pia wa waandishi kukopi stori au wahusika wa The Book of the Dead ni mkubwa. Na kama ndivyo ilivyokuwa basi hata hivi vitabu vya sasa vina uhalakini ndani yake.

Mfano neno;

HOLY BIBLE linatokana na neno la Kigiriki:

HELIOS=JUA na BIBULOUS=KITABU

hivyo neno HOLY BIBLE = KITABU CHA JUA

mungu jua huko misri aliitwa Amun Ra na huko Canaan alijulikana kama Shemesh, na katika bible kuna mji waliuteka waisrael kwa jina la bethshemu (bethshemesh) au mji wa makao ya jua. Ni ukweli usiopingika kuwa imani nyingi zilianzia kwenye ibada hii ya mungu jua kabla ya kuja kwa idea zingine na practises kumuhusu mungu.

Wahusika katika stori ya the book of dead kwa uhusika wao, tukiwapa scenes katika Bible basi watafiti ifuatavyo kwa mujibu wa mfanano wa visa vyao:-

AMEN RA(the sun god)- MUNGU (Bwana wa mabwana na mungu wa miungu)

THOTH- NENO(ndiye sauti ya mungu, moyo na kusudi lake pasipo yeye akikufanyika kitu akitamka ujiumba na neno lake kamwe halina dosari, ndiye mtunza kumbukumbu zote)

OSIRIS- YESU ( mwenye haki machoni pa AMEN RA na miungu, alikishinda kifo na hivyo kupewa kiti cha ufalme, ndani yake yupo NENO(thoth) na NENO ni uzima, ndiye mwenye mamlaka na funguo za kuzimu, atawahukumu wafu na maombi yote ya uzima afterlife uelekezwa kwake)

SET- SHETANI/DEVIL

Shetani ni sawa na neno "Mshitaki" na kwenye stori hii SET ndo aliyemshtaki aliyemkosea.
Alitaka pia kujiinua hili kumpokonya mwenzake ufalme ambapo alifanikiwa lakini baadae akapokonywa na kuharibiwa.

Alipigana vita kubwa na Horus(malaika Gabriel ila utofauti wa hapa na kwenye bible ni kuwa alishindwa lakini alimjeruhi jicho Horus) na mwisho tunaona akiitwa kwa jina ambalo hata YESU kwenye Biblia alimwita nalo shetani yaani The father of lies au "Baba wa uongo")

HORUS- (Kama malaika mkuu au mkuu wa majeshi ya Amen Ra, na mwana wa pekee wa OSIRIS na ISIS (uonekana kiroho katika umbile la kichwa cha Tai) huyu ni msimamizi mkuu wa anga huku akiangaziwa pande zote na jicho la Ra( mwangaza wa jua)

Kwenye Biblia huyu character hazungumziwi kiundani ila kwenye Quran kuna muhusika anatajwa kwa waislamu kuchukua tahadhari dhidi yake wakimwita masihi dajjal au mwenye jicho moja au chongo (kwenye bible wanamwita mpinga kristo) huku kwenye stori tunamwona hana hatia yeye ni Avenger wa kifo cha baba yake OSIRIS sasa yupi anaongea ukweli katika haya maandiko yote matatu ya waisraeli, waarabu au wamisri hapa nami sijuhi.

Kupitia huo uchambuzi mfupi nilioufanya kupitia kuoanisha matukio hayo na vitabu vingine vya imani hili kupata walahu logic moja, wewe binafsi una mtizamo gani katika hili?

Je, wafikiri niwazavyo ni sahihi au siyo sahihi? Na kwanini wasema hivyo?
Maelezo yanaweza kuwa mengi sana kutokana na mtizamo wa mtu.
Ila ukweli ni kwamba washirikina wenyewe wale wazito wamekiri kuwa Book of The Dead, ni Kitabu chao wanachokitumia kwenye ibada zao za Kishirikina.
Vitabu vya Kishirikina mara nyingine vinawatumia wahusika wale wale wa kwenye Biblia.

Ukisoma "The Free Masonic Bible" utamkuta Yesu na Mitume wake wote kumi na wawili.
Ukisoma "The Sixth and Seventh Book of Moses" utamkuta Nabii Musa na baadhi ya Manabii wote wa Agano la Kale, lakini ni Kitabu cha Kishirikina pia.
Satanic Church nao wanatumia Biblia yao ya "The Satanic Bible" nayo wapo Manabii karibu wote wa Agano la Kale na Jipya.
Lakini ukivisoma utakuta Maudhui yake hayamlengi Mungu wa kwenye Biblia, wana mungu wao, na Ibada zao.
Lengo halisi ni kuwazuga tu wasomaji wasione kasoro katika Vitabu hivyo.
Hivyo ni jukumu tu la wasomaji kusoma kwa umakini kuchambua
Lengo halisi la hivyo vitabu.

Mtoa Mada.
Je unaweza kutueleza lengo halisi la Kitabu cha THE BOOK OF THE DEAD ni nini ?
Kama umekisoma na kukielewa ?

Kitabu cha Wafu.
Wakati Mungu anasema sio Mungu wa Wafu.

Mathayo 22:32
Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo? Mungu si Mungu wa wafu, bali wa walio hai.

Luka 20:38
Naye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai; kwa kuwa wote huishi kwake.

Marko 12:27
Yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai. Hivyo mwapotea sana.

Mnaojishughurisha na kusoma vitabu vya Wafu.
"Mwapotea sana"
Kwa Mungu, neno kupotea nadhani linafahamika vizuri.
 
Hicho ni Kitabu kinachofundisha Uchawi.
Vipo vingi sitaki kuviorodhesha hapa kwa kuchelea kutafutwa na watu na kuvisoma.

Stori za hicho kitabu zote ni za ukweli na wahusika wakuu ni Mashetani wengine wanayaita Maibirisi na malaika zao Majini Mizimu Nk.

Angalieni tu hayo majina sio yanayotumika kwa kuwaita Binadamu wa kawaida.

Nawatahadharisha watu wenye nia njema kuto kukisoma hicho kitabu.
asant kwa tahadhari
 
Maelezo yanaweza kuwa mengi sana kutokana na mtizamo wa mtu.
Ila ukweli ni kwamba washirikina wenyewe wale wazito wamekiri kuwa Book of The Dead, ni Kitabu chao wanachokitumia kwenye ibada zao za Kishirikina.
Vitabu vya Kishirikina mara nyingine vinawatumia wahusika wale wale wa kwenye Biblia.

Ukisoma "The Free Masonic Bible" utamkuta Yesu na Mitume wake wote kumi na wawili.
Ukisoma "The Sixth and Seventh Book of Moses" utamkuta Nabii Musa na baadhi ya Manabii wote wa Agano la Kale, lakini ni Kitabu cha Kishirikina pia.
Satanic Church nao wanatumia Biblia yao ya "The Satanic Bible" nayo wapo Manabii karibu wote wa Agano la Kale na Jipya.
Lakini ukivisoma utakuta Maudhui yake hayamlengi Mungu wa kwenye Biblia, wana mungu wao, na Ibada zao.
Lengo halisi ni kuwazuga tu wasomaji wasione kasoro katika Vitabu hivyo.
Hivyo ni jukumu tu la wasomaji kusoma kwa umakini kuchambua
Lengo halisi la hivyo vitabu.

Mtoa Mada.
Je unaweza kutueleza lengo halisi la Kitabu cha THE BOOK OF THE DEAD ni nini ?
Kama umekisoma na kukielewa ?

Kitabu cha Wafu.
Wakati Mungu anasema sio Mungu wa Wafu.

Mathayo 22:32
Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo? Mungu si Mungu wa wafu, bali wa walio hai.

Luka 20:38
Naye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai; kwa kuwa wote huishi kwake.

Marko 12:27
Yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai. Hivyo mwapotea sana.

Mnaojishughurisha na kusoma vitabu vya Wafu.
"Mwapotea sana"
Kwa Mungu, neno kupotea nadhani linafahamika vizuri.

Nafikiri wote tuko sawa kulingana na majibu yako umeonekana kuegemea unachoamini zaidi kuliko kujenga hoja juu ya maswali yangu muhimu.

Moja nilitaka kujua kwanini kitabu hicho chaitwa kitabu cha jua?

Pili suala la mfanano wa stori za bible kulandana na za the book of the dead licha ya gepu kubwa la miaka ya utunzi kati ya vitabu hivyo viwili.

Nakubali kuwa kuna kasumba ya shetani kujifananisha na Mungu kwa kumwigiza ili kuwadanganya wengi wanase kwenye mtego wake.

Ila sikubaliani nawe kwenye suala moja tu lakuamini kuwa huyo Mungu uliyeandikiwa habari zake kuwa ndiye sahihi basi hatupaswi kumwakiki kama ndiye kwa kusoma maandishi mbalimbali nakuchimba kiundani tujue mbichi na mbivu.

Vipi kama wamwabudu shetani yule yule kupitia kitabu chako kitukufu cha Biblia au Quran?

Sasa naomba nikujibu maswali yako kwa kifupi: unataka kujua malengo ya The book of the Dead ni yapi?

Kwani ulishajiuliza malengo ya Biblia ni yapi?
Bila shaka jibu nikupata uzima wa milele baada ya kuvuka hukumu ya moto kwa kutenda mema sawa na maagizo ya Mungu.

Kwanini wafikiri kitabu cha wafu kina ajenda tofauti sana na hii ya kwenye bible?

Je, siyo kweli kuwa wote (walengwa ukiwemo wewe) wanaogopa "KIFO" au sintafahamu yake?

Swali lako la mwisho ni je Mungu ni wa wafu au walio hai?

Jibu ni Mungu (yeye yu hai na wanaomwabudu wapaswa kuwa hai ndiyo tafsiri ya vifungu ulivyo-quote) ni wa wote kwa maana kama anabagua wafu kwanini YESU afe na kwenda kuzimu (kuwahubiria wafu pia nyakati za mwisho aende kuwafufua) na kitendo cha kufufuka nakuhurudia uzima wake(ishara ya kukishinda kifo) na ndiye ambaye kitabu cha ufunuo kinamtambua kama mrithi wa kiti cha ufalme na pia ndiye mwenye funguo za mbingu na kuzimu na uidhinisha hukumu.

Je, character ya OSIRIS ina utofauti gani na hii ya YESU? (Nijibu kwa utashi na siyo kwa kuegemea dini yako tu)
 
The Book of The Dead. Ni kitabu kinachotisha sana.
Ni Kitabu cha Kuzimu.

Hata mtoa mada nina uhakika hakifahamu vizuri

Kama kuna mtu mwenye Roho Ngumu basi na akisome tu.

Mimi nimemaliza kazi.
Naona umejivika uhusika kana kwamba uliyekisoma kitabu hiki dunia nzima ni wewe peke yako..sikukatalii kukataza watu nakuwapa onyo ni jambo zuri pia hili mtu anapojitosa kusoma awe amejipanga kuyakabili vyema anayoyasoma.

Maana daima naamini unaposaka maarifa fulani kama haya yenye usintofahamu ndani yake huwa kuna risk lazima ukubaliane nazo na siyo busara kabisa kwa msomi kutisha wengine hili wasipate ufahamu bali abaki kujua mambo hayo mwenyewe.

Kumbuka mpaka mtu aamue kuresearch nakusoma vitabu vya kizamani vyenye lugha ngumu na stori zisizoeleweka kirahisi nakama za kufikirika vile huwa anakuwa amefanya maamuzi binafsi na pia ana interest au hobby na anachotaka kufanya hivyo si vyema kutisha wenzio kwani wewe ulijuaje na wao kwanini waendelee kuwa gizani.
 
Naona umejivika uhusika kana kwamba uliyekisoma kitabu hiki dunia nzima ni wewe peke yako..sikukatalii kukataza watu nakuwapa onyo ni jambo zuri pia hili mtu anapojitosa kusoma awe amejipanga kuyakabili vyema anayoyasoma.

Maana daima naamini unaposaka maarifa fulani kama haya yenye usintofahamu ndani yake huwa kuna risk lazima ukubaliane nazo na siyo busara kabisa kwa msomi kutisha wengine hili wasipate ufahamu bali abaki kujua mambo hayo mwenyewe.

Kumbuka mpaka mtu aamue kuresearch nakusoma vitabu vya kizamani vyenye lugha ngumu na stori zisizoeleweka kirahisi nakama za kufikirika vile huwa anakuwa amefanya maamuzi binafsi na pia ana interest au hobby na anachotaka kufanya hivyo si vyema kutisha wenzio kwani wewe ulijuaje na wao kwanini waendelee kuwa gizani.
Sasa wewe kitabu cha Wafu kinakuhusu nini.
Au na wewe ni Mtu Mfu pia ?

Ushaambiwa
is The Book Of The Dead.

Jibu sahihi ni lazima tulipate toka kwa watu Wafu

Yaani tusubiri Maiti ndizo zitusibitibishie ukweli wa hicho kitabu.

Basi tufanye wewe ndiye mtu Mfu tuambie Wafu wanasemaje?

Vitabu vinasema.
Kama cha Sekondari kinatuambia na darasa lake ama form one au two.

Kama cha chuo kinasema na mwaka husika.

Sasa wewe bado uko mzima unataka uelezee habari za waliokufa.

Huoni kwamba huna mantiki ya kukisemea hicho kitabu ?

Au macho yangu hayaoni ?
 
Back
Top Bottom