The Bold & Nifah: Happy Six Months "Anniversary"!

Habibu B. Anga

JF-Expert Member
May 7, 2013
6,557
25,671
Nchi za mashariki mwa bara la Asia kuna falsafa ya kale sana wanayoiamini kuhusiana na muunganiko na mahusiano ya binadamu. Falsafa hii inaitwa Red String Of Fate (Yīnyuán hóngxiàn).

Kwamba, kuna 'uzi' usioonekana unawaunganisha watu tangu siku wamezaliwa, watu ambao maishani wanatakiwa kuja kukutana, au kusaidiana au kuwa pamoja.

Uzi huu usioonekana unalindwa na kusimamiwa na aina ya Mungu/roho anayeitwa Yuè Xià Lãorén (au kwa kifupi Yuè Lão).

Tafsiri rahisi ya jina la "mungu/roho" huyu ni "matchmaker god"
Yeye anasimamia uzi huu unaowaunganisha watu hawa usikatike daima mpaka pale watakapokuja kukutana.

Nchini china wanaamini uzi huu unafungwa kwenye viwiko vya mkono, na nchini Japan wao wanaamini uzi huu unafungwa kwenye kidole kidogo cha mwisho na kwamba uzi huu unaowaunganisha watu hawa, unaweza kupinda (tangle) au kunyooka zaidi (stretch) lakini kamwe hauwezi kukatika mpaka watu hawa wakutane.

Kwa kifupi, imani hii ya watu Asia inarandana na imani ya watu wa magharibi kuhusu 'Soulmate'.

Mimi na Nifah: Historia fupi

Nikiwa sekondari nilikuwa naisikia sikia kitu kinaitwa "jambo forums" na 'kasheshe' zake lakini sikuijua sana kwa undani.

Baadae mwaka 2009 nikiwa kidato cha tano nikaichungulia ndani kujua yaliyomo, kipindi hiki ilikuwa imeanza kuitwa "Jamii Forums".

Kipindi hiki kulikuwa na mijadala 'mizito mizito' sana na karibu yote ilihusu siasa.
Japokuwa nilikuwa 'mtoto wa sekondari' nilivutiwa nayo sana, napenda sana mijadala, hasa mijadala mizito (yenye hoja sio matusi).

Mwaka 2011 nikajiunga rasmi (kwa ID nyingine) lakini baadae nikasahau password ya ile ID. Ndipo hapa mwaka 2013 nikafungua ID hii ya The bold.
Mwanzoni nilikuwa nasoma tu, sikuwa mchangiaji sana, lakini kuanzia 2014 nikaanza kuwa active zaidi na hata kuanzisha threads.

Kwa sababu zangu binafsi, nikaepuka mijadala ya jukwaa la siasa, na nikajikuta navutiwa zaidi na Jukwaa la Jamii Intelligence. Na nikitaka kupumzika nikawa naingia Celebrities Forums… na huko ndiko mambo yalikoanzia.

Binafsi nina maslahi fulani fulani na pia ni shabiki mkubwa wa vijana wa WCB. Huko Celebrities Forum nikakutana na bibie Nifah mkosoaji mkubwa wa WCB.
Taratibu tukaanza kukwaruzana kwenye mijadala. Ugomvi huu ukawa mkubwa zaidi na kufikia pabaya mwaka 2015 na mwanzoni kwa 2016. Ulikuwa ni ugomvi mkubwa haswaaa kiasi kwamba tulikuwa tunatoleana lugha Kali za aibu kabisa. Ugomvi huu ukaendelea na kukua siku baada ya siku, kiasi kwamba Nifah akawa adui yangu namba 1 humu JF na mimi nikawa hivyo kwake.

Lakini ukweli ni kwamba rohoni nilikuwa namkubali sana huyu bibie na nilikuwa navutiwa nae sana, IQ yake, ujengaji hoja wake na niliamini ni mtoto mrembo haswaaa!!

Kwahiyo mara kwa mara nilikuwa nafanya ule mchezo wa kutembelea profile yake na kuanza kuangalia replies zake kwenye threads mbalimbali. Nikazidi kuvutiwa naye zaidi na nikajikuta naanza kulike posts za huyu "adui" yangu.

Pasipo mimi kujua, kumbe naye anafanya mchezo huu wa kutembelea profile ya mimi "adui" yake na ghafla nikaanza kuona likes kutoka kwake.
Baadae tension kati yetu ikaanza kupungua na tukawa tukikutana kwenye threads yoyote lazima tuchit chat.
Kipindi cha uchaguzi wa marekani nakumbuka tulibet, yeye akaweka 100K kwa Clinton, mimi nikaweka 100K kwa Trump, .. Alijuta

Chit chat kwenye threads zikaendelea…

Kisha tukahamia PM. Huko PM kilichoendelea sitaki kuwasimulia… ila kwa ufupi mwana wane sikutaka ujinga, nikajitutumua, nikafanya yangu… and the rest is history.!

Tangu hapo… we have been crazily in love together!

Najivunia kumpata mwanamke wa dizaini yake, ana heshima, mnyenyekevu, big IQ, beautiful, anajua kukalangiza jikoni na mwenye kujua haswa mapenzi ya dhati… bila kusahau usiku tukizima taa huwa najihisi tumeenda kutalii sayari ya Mars!! Mashallaaahh…

Nafurahi pia ndugu zake wanajivunia mimi kuwa na binti yao, na ndugu zangu pia wanajivunia mimi kuwa na huyu binti.!

Mwenyezi Mungu akutunze white masai wangu… na wakuu mtuombee soon tunataka kufanya halal..

Imekuwa six months sasa tuko pamoja… let's make it to six more years, and then 60 years na hatimaye 600 years!! Let's make this forever...

Happy six months anniversary soulmate...
Nakupenda sana Cheupe!

The Bold
-----------

Mungu wanguuuuuu! Hivi tumeshafikisha miezi 6 baba?
Umenifanya nikapekue diary na uko sahihi kabisa,hadi tarehe kumbe bado unaikumbuka? Umetisha kichwa wangu.

Well,nashukuru kwa kila kitu mpenzi wangu. Nashukuru kwa kunipenda kiasi ambacho sikuwahi kudhani kama nitakuja kumpata mwanaume wa kunipenda hivi!
Yani unanipenda hadi kila wakati najihisi ni mwenye deni,nitaulipa vipi upendo huu? Naona hakuna njia nzuri zaidi ya kukulipa kwa upendo my sweetlove...yaani ni upendo kwa upendo

Napenda kutumia fursa hii kuwapa ushauri wale wote wanaovutiwa na sisi kama couple.
Jamani mapenzi ya wazi yana changamoto nyingi mnoooo,sio mchezo.
The bold ni mwanaume haswa,mvumilivu kwelikweli.
Kapambana na mengi/wengi sana juu yangu na mapenzi yetu kiujumla.

Kaambiwa na bado anaambiwa mengi,lakini I thank God he is smart enough,hajatetereka ndio maana hadi sasa tuko pamoja.

Achana na maneno ya watu,ni wengi sana hawaamini kama sisi ni wapenzi.
Katika maswali ninayokumbana nayo humu (na hata kwa ndugu jamaa na marafiki wanaoijua ID yangu ) ni "Wewe na Bold ni wapenzi kweli?"
Nawaelewa sana kwanini wananiuliza swali hili. Sababu kuu ni HAWAAMINI kama inawezekana watu mkajuana kupitia mitandao/mtandao na mkapendana kweli.

Jamani,this is serious,sio maigizo wala hakuna chochote kile zaidi ya mapenzi.
Na haya mambo yanawezekana kabisa.

Ila sasa (naomba radhi kwa wale nitakaowakwaza) wale wanaoandika kabisa posts za kutafuta wachumba/wapenzi au wenzi ndio wanaotia ukakasi na kuondolea credibility ya mapenzi ya mitandaoni maana wengi hawako serious.

Haya mambo yanawezekana endapo yakijijenga yenyewe (kama mimi na Bold tulivyopendana)
Hii ndio ile wenzetu wanasema "Let love lead"

Baada ya kusema hayo naomba nihitimishe kwa haya;

"Nakupenda sana Bold wangu,asante kwa kunipenda namna hii,asante kwa kunivumilia,asante kwa vita zote zile ulizopambana na bado unaendelea kupambana kwa ajili yangu na mapenzi yetu kiujumla.
Mara nyingi huwa nakuambia kila wakati naumiza kichwa nikiwaza nikukeep vipi,natamani nifanye zaidi ya yale uniambiayo ndiyo pekee unayoyahitaji.
Nitakupenda Daima,that's a promise"

Happy six months anniversary my love
 
images.jpg
 
Back
Top Bottom