TFF wameturuhusu tusajili dirisha dogo, tutasajili..

Hussein Massanza

JF-Expert Member
Dec 26, 2012
918
1,994
Salaam watu wa soka,

Za masiku?

Naendelea kuwapatia taarifa muhimu kuhusu timu yetu ya Singida Big Stars na leo taarifa kubwa ni kuhusu uamuzi wa TFF kutufutia adhabu ya kutosajili dirisha dogo mwezi Desemba kama walivyotangaza awali.

Uamuzi wa TFF ulitokana na shauri lililowahi kupelekwa na Polisi Tanzania kwa kile walichodai tulimsajili mchezaji wao, Metacha B. Mnata, akiwa bado na mkataba nao, jambo ambalo tulikuja kulimaliza kwa makubaliano ya pande zote mbili japo kwa bahati mbaya shauri lililofikishwa TFF lilikuwa bado halijafanyiwa kazi hivyo kuja kuamuliwa tukiwa tayari tushamaliza mgogoro na Polisi Tanzania.

Kwa umakini mkubwa, Wakili wetu pamoja na jopo la wanasheria wetu walilazimika kuomba review (mapitio) ya adhabu ya TFF na hatimaye kupata nafasi ya kwenda kwenye Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji na kuwasilisha hoja nzito za utetezi zilizopelekea kutenguliwa kwa adhabu hii.

Niwahakikishie mashabiki wetu, Benchi la Ufundi la Singida Big Stars limeandaa ripoti maalum inayoainisha maeneo au safu ambazo tutaenda kuziboresha kwa kuzifanyia usajili makini punde tu dirisha dogo litakapofunguliwa mwezi Desemba.

Tunaishukuru TFF na Bodi ya Ligi kwa kusikiliza shauri hili na kutupatia haki yetu. Bodi na Menejimenti ya Singida Big Stars itaendelea kufanya kazi kwa weledi zaidi na kuhakikisha tunaleta ushindani wa kweli ili kuongeza ubora wa Ligi yetu.

WhatsApp Image 2022-11-29 at 17.10.08.jpeg

Taarifa si inatosha?
 
Asante kwa Taarifa mkuu.
Hussein Massanza afisa habari wa club.

Mikupongeze sana Kwa kuendelea kutupa taarifa Wana JF na wapenda soka wote kwa UJUMLA.

Ningependa nikushauri kuhusu jambo Moja tu kwa sababu ya Muda.

KWanini VILABU VYETU vinaendekeza sana usajili.???????

1. Kuna upigaji mkubwa. Wizi.
2. Kukosekana Academy za vijana.
3. Kukosekana kwa mikakati ya vilabu Katika uendeshaji wa timu.

Sijajua sigida Ina madhaifu kwenye SAFU Gani kiufundi.

LAKINI KWANGU USAJILI SI SULUHU YA MATATIZO.
 
Asante kwa Taarifa mkuu.
Hussein Massanza afisa habari wa club.

Mikupongeze sana Kwa kuendelea kutupa taarifa Wana JF na wapenda soka wote kwa UJUMLA.

Ningependa nikushauri kuhusu jambo Moja tu kwa sababu ya Muda.

KWanini VILABU VYETU vinaendekeza sana usajili.???????

1. Kuna upigaji mkubwa. Wizi.
2. Kukosekana Academy za vijana.
3. Kukosekana kwa mikakati ya vilabu Katika uendeshaji wa timu.

Sijajua sigida Ina madhaifu kwenye SAFU Gani kiufundi.

LAKINI KWANGU USAJILI SI SULUHU YA MATATIZO.

Asante sana mkuu. Kwa upande wetu tutakuwa na academy hapo baadae, kwa sasa tutafanya usajili na tutatumia pia vijana wetu wa timu za vijana (U20 na U17).
 
Ushauri wangu, sajilini vijana damu changa. Acheni wazee ambao umri umeenda kama Kagere, Tambwe, Wawa, Juma Abdul, Deus Kaseke na wengineo
 
Kwa usajili wenu nilitegemea muwe top 3. Lakini nashindwa kuwatofatisha na namungo

Wanashika nafasi ya ngapi, kwa tofauti ya alama ngapi? Seriously usajili wao na usajili wa azam upi ni usajili mkubwa? Nafasi waliyopo wamestahili
 
Hongereni kwa Hilo lakini pia napenda tu kuwashauri punguzeni idadi ya wazee kwenye klabu yenu
 
Wanashika nafasi ya ngapi, kwa tofauti ya alama ngapi? Seriously usajili wao na usajili wa azam upi ni usajili mkubwa? Nafasi waliyopo wamestahili
Wako nafasi ya nne lakini gape lao la points ukilinganisha na anaeshika nafasi ya 3 ni kubwa kuliko yule anaeshika nafasi ya 5,
 
Kwa usajili wenu nilitegemea muwe top 3. Lakini nashindwa kuwatofatisha na namungo

Sisi malengo yetu msimu huu ni TOP 4. Tukimaliza msimu nafasi ya 4, 3, 2 tutakuwa tumefikia lengo. Kwa sasa tupo nafasi ya 4. Tunasonga.
 
Ushauri wangu, sajilini vijana damu changa. Acheni wazee ambao umri umeenda kama Kagere, Tambwe, Wawa, Juma Abdul, Deus Kaseke na wengineo

Kagere ana goli 4 mpaka sasa. Wawa anasaidia sana kwenye safu ya ulinzi pamoja na Juma. Kaseke nae anasaidia kwenye mashambulizi. Hawa ni wachezaji muhimu sana kwetu.
 
Back
Top Bottom