TFF tokeni zama za mawe za kati

TFF tokeni zama za mawe za kati

Shakala

Member
Joined
Sep 30, 2024
Posts
13
Reaction score
11
Wasalaam,

Soka la Tanzania limekua kwa kasi sana hivi karibuni kiasi cha kuvutia watu kadhaa kuanza kuwekeza kwenye mpira wetu,Azam tv, Vodacom,nbc,sportpesa,GSM,MO na wengineo.watanzania wengi wamekua wakijipatia kipato kupitia soka;wachezaji,wauza jezi,watu wa usafirishaji,wenye nyumba za kulala wageni,wenye viwanja,wauza ving'amuzi,wenye vibanda umiza, serikali pia imenufaika.

Pamoja athari chanya kama hizo lakini dhahifi inaonekana TFF wenyewe wanataka kuudidimiza huu mpira kutokana na aidha kua na upeo mdogo wa kufikiria ama wana kusudi jingine tusolijua.

Kwanza ni ishu ya waamuzi:wamekua wakiboronga makusudically na hakuna hatua stahiki zinazoendana na makosa yao zikichukuliwa.

Pili;miaka ya hivi karibuni mechi zenye mvuto wa aina yake/derby kuahirishwa kienyeji tu tena siku ya tukio bila kujali ni kiasi gani mashabiki wametoa sadaka muda na fedha zao kuja kuinjoi ladha ya soka la Tanzania.wengine wanatoka nje ya nchi huko lakini ndo hivyo wanarudi mioyo ikiwa na kinyongo.Rejea derby ya 2021 na hii ya juzi 2025.

Kwa staili hii kweli wanawajengea picha gani wadau?
Wamawatia hasara kiasi gani wadhamini?

Itakuaje siku mashabiki wakisusa kuhudhuria viwanjani?
Azam TV ataathirikaje pindi watapoacha kulipia ving'amuzi vyao?

TFF BADILIKENI ACHENI KUTUHARIBIA KIUNGANISHI PEKEE KAMA TAIFA MAANA SIASA ILISHATUPARAGANISHA🙌🏿
 
Hao tff sijuwi nani! hata hiyo ligi yenu wakiishusha mi hayanihusu, mi nashabikia ugomvi wa kuku na hauonyeshwi azam tv.
 
Tff na bodi ya ligi ya Tanzania wapo nyuma ya muda na ni slow leaner, wamekaa kizamani sana na hawaendani na mpira wa sasa. Inatakiwa waachie ngazi na wapewe wenye uwezo wa kisasa.
 
Tatizo lipo kwa hawa wazee wanaoziongoza hizo Taasisi mbili za soka..
 
MSIKWEPE TATIZO LA WAZI WANASIASA NI KIDONDA KINGINE KISICHOONEKANA
 
Back
Top Bottom