thirteen06
Senior Member
- May 17, 2021
- 137
- 120
Hivi karibuni Naibu Waziri wa Afya alipokuwa akijibu swali kuhusu Umuhimu wa kurudishwa kwa TFDA alitoa majibu Yenye kuleta matumaini juu ya kurudishwa kwa taasisi hii muhimu ambayo ni mahususi kwa ajili ya usalama chakula. Kwa kuwa tayari tuna taasisi ya TMDA. Binafsi naona taasisi hii ambayo serikali imeonesha kukubali Umuhimu wake na kufikiria kuirejesha nafikiria iitwe TFA,, Yaani ijihusishe na bidhaa za vyakula tu.
Mathalan, hivi karibuni imebainika 43% ya chumvi inayotumika Tanzania haina madini joto. Madini joto Ni muhimu kwa ukuaji wa mwili na afya ya akili. Ukosefu wa madini haya hupelekea kupata ugonjwa wa goita, udumavu wa mwili na akili, na pia tatizo la kujifungua watoto njiti kwa akina mama wajawazito. Hivi Sasa ugonjwa wa goita umekuwa ukiongezeka miongoni mwa jamii ya watanzania siku baada ya siku.
Je Ni kwa kiasi gani jamii itaweza kuepukana na Uwepo na matumizi ya bidhaa hizi ambazo kwa kiasi kikubwa zimekuwa zikiingizwa kinyemela sokoni?
Hapo ndipo Umuhimu wa taasisi hii imara itakayowezeshwa kwa vitendea kazi madhubuti vinavyoendana na wakati unapoonekana.
Mathalan, hivi karibuni imebainika 43% ya chumvi inayotumika Tanzania haina madini joto. Madini joto Ni muhimu kwa ukuaji wa mwili na afya ya akili. Ukosefu wa madini haya hupelekea kupata ugonjwa wa goita, udumavu wa mwili na akili, na pia tatizo la kujifungua watoto njiti kwa akina mama wajawazito. Hivi Sasa ugonjwa wa goita umekuwa ukiongezeka miongoni mwa jamii ya watanzania siku baada ya siku.
Je Ni kwa kiasi gani jamii itaweza kuepukana na Uwepo na matumizi ya bidhaa hizi ambazo kwa kiasi kikubwa zimekuwa zikiingizwa kinyemela sokoni?
Hapo ndipo Umuhimu wa taasisi hii imara itakayowezeshwa kwa vitendea kazi madhubuti vinavyoendana na wakati unapoonekana.